Hiki Kidori cha Masanja Mkandamizaji!

Makanyaga

JF-Expert Member
Sep 28, 2007
10,315
6,845
Kinaniuma sana. Kinakaa kinapigwa pigwa tu na kukaa kinafokewa fokewa ovyo ovyo tu kila mara bila sababu. Kwa mtizamo wangu hicho kipo kwa ajili ya kuburudisha na au kufundisha watoto. Mtoto anahitaji kupendwa, japo haimaanishi asikanywe au kuchapawa viboko, kama amekosea. Lakini sasa hiki kidori hakijakosea wala kufanywa unastukia kinaanza kuchapwa makofi au kufokewa! Sasa masanja anawafundisha nini watoto wetu hapa kama kidori alichokileta ili kiwaburudishe anakipiga au kukifokea bila hata kuwa kimemkosea? Mimi nadhani hapa hapa haki za watoto wetu zinakiukwa. Ningeshauri wakiondoe kwenye jukwaa au aache kuki-misstreat namna hiyo. Nadhani hata watoto walio wengi watakuwa hawafurahii kabisa hali hiyo!
 
Mimi sisemi, mtoto wangu has been complaining that Scooby Doo, anapigwa kila wakati! Nimebaki kumwambia tu, ok, you've been watching Masanja tena!
 
mze huna utani wewe eh...?
Hujawahi kusoma kitabu cha hadithi au kuangalia tamthiliya kwenye TV na ukaona huruma wakati unajua kabisa kuwa 100% ni fiction. Tatizo hapa ni kuwa walengwa wenyewe sasa ni watoto halafu I doubt kama wote watakuwa wanaelewa kuwa huo ni utani! In a similar, anaweza akitania ki-urafiki na siyo lazima awe harsh, na ndiyo atawafurahisha zaidi watoto!
 
Mtazamo wangu ni kuwa haki za wanyama zinakiukwa na si za watoto. Kwani kale ni kambwa na sio katoto.
 
kwani kumetokea nini? au ndo yule mtoto wake masanja anayekujanae pale kwenye luninga? alimzalisha mdada mmoja hivi wa tabasa sijui, sasa ni shida tupu, mtoto hata kufaidi upendo wa mama hana..muda wote jamaa anatembea naye kuzunguka akionyesha watu kuwa amepata mtoto..hahaha.
 
Mimi sisemi, mtoto wangu has been complaining that Scooby Doo, anapigwa kila wakati! Nimebaki kumwambia tu, ok, you've been watching Masanja tena!

Nadhani muda umefika wakirudishe tena, kuna haja hiyo badala ya kuwa wanapoteza mda zaidi ya dakika 10 kila mmoja kujitambulisha majina karibia 30, wautumie mda huo kuwaburudisha watoto na hicho kidori chao. Najua watoto watakuwa wamekimiss sana, na safari hii wawe wanaki-treat friendly, watoto huwa hawapendi violence,...., na hata kama wangekuwa wanapenda, bado wazazi hatupendi kufundisha watoto wetu violence. Wangekirudisha na staili mpya kwa watoto ili watoto nao wa-enjoy zaii the Original Comedy!
Maoni yangu
 
Back
Top Bottom