Hii TAKUKURU ya mwaka huu imeota meno

Hii TAKUKURU ya mwaka huu imeota meno

Click Hapa

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2013
Posts
479
Reaction score
206
Heshima kwenu Wana JF.

Nimekuwa nikijiuliza hivi nini kimetokea this time kwenye Taasisi hii ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini kwa hili wimbi la kamatakamata ya watoa Rushwa kwenye mchakato Mzima wa uchaguzi unaoendelea nchini. Kinachoshtua zaidi wanaokamatwa au kuhusishwa na kutoa Rushwa ni makada nguri wa CCM, Hata Nape?

Mpaka sasa orodha imeshakuwa ndefu: Leo nimesikia Anna Kilango Malecela naye kanaswa, hivyo kaungana na wenzie kina Chambiri, Mwigulu, Nape na wengineo.

Kama zoezi hili linaloendeshwa na Takukuru ni kwa uhalisia basi tuungane kwa pamoja kuipongeza Taasisi hii iliyo chini ya ndugu Hosseah kuwa sasa imeota MENO na inapambana vilivyo na watoa Rushwa nchini bila kujali itikadi ya nyama. Big up Hosseah na Taasisi yako.

Kwa upande wa pili inatia Shaka kuwa je haya MENO ya ghafla yameotaje, isijekuwa danganya Toto.

Kamatakamata hii naelekea kuifananisha na lile wimbi la utitiri wa watia nia wa CCM kwenye nafasi ya urais. Wajuzi wa mambo wanasema eti utitiri ule ilikuwa ni malengo maalumu ili AKIKATWA basi asilalamike kwakuwa watakuwa wamekatwa wengi kwa hiyo itabidi awe mpole tu.

Mwanzoni iliniwia vigumu kuielewa Sanaa ile ila baadaye niliielewa kuwa ndo ilikuwa maana yake, na Leo nimesikia ile Audio records ya Paul MAKONDA akimponda EL akajisahau au kwa kutokujua akapita mlemle, eti anauliza "wamekatwa Waziri Mkuu Pinda, Makamu wa rais, Mark Mwandosya n.k hakuna aliye lalamika, iweje wewe ulalamike, kwani wewe nani" kwa akili hii ya MAKONDA ni dhahiri kuwa utitiri ule wa watia nia wa CCM ilikuwa ni mpango Mzima.

Sasa hili la TAKUKURU nalo linaanza kututia hofu, hivi ni MENO ya kweli au Sanaa zilezile?

Inaweza kuwa vigumu kuielewa Nina maana gani ila nahisi hizi ni Sanaa zilezile tu, yaani siku ikitokea ikitokea Watanzania tusishangae kwa kuwa TAKUKURU ya mwaka huu imeota MENO. Watakuwa wanatwambia kuwa tayari tulishawakamata kina Nape, Anna Malecela na wengineo leo itakuwa wewe!

Maana wanasema jamaa wanatumia fedha zake kuhonga watu ili wamfuate kwa wingi. Yaani wafuasi wote walonyuma yake ni kwamba anawahonga.

Nadhani kama TAKUKURU hii imekuja kwa mpango huu ili kumvizia na hatimaye kumchafua, nadhani tayari wamechelewa sana. Ingefaa sana kama wangemnasa na kumchafua akiwa bado yupo team ile ila kule alipoelekea huwa hakuna mchezo huo wa Rushwa kama ilivyo team x na ndo maana hadi Leo hii wanaonaswa ni team x tu.

Nashauri Taasisi hii isijiingize kwenye siasa hizi chafu, ifanye Kazi kwa weledi wake tu. Watanzania wa Leo wameamka kwa kiwango cha juu sana.

Chondechonde Team Y, mna maadui wengi mno kuliko inavyoweza kuelezeka. Rushwa ni adui wa haki.
 
Watanzania shitukeni hatudanganyiki tena eti takukuru wanajifanya wako busy kukamata na kuhoji wanasiasa wa ccm kwa rushwa,uongo na usanii mtupu,nani kapelekwa mahakamani?

Wanawakamata wanawahoji kisha wanawaachia huru ,wanadhani tutadanyanyika ,nawaambia mnajidanganya wenyewe,Shame on you PCCB
 
Kama fisadi ndio anagombea urais tena kupitia upinzani ambamo ndio wananchi wanaimani nao itakuwa wagombea ubunge na udiwani? Watanzania tufanyeni kazi tuu tulipe kodi zao hawa wanasiasa lao moja wasitutanie
 
nashangaa mwenyewe nimefika moro mda c mrefu nimekuta wa magamba wachache wameshikiliwa wanahojiwa
 
Tusaidieni hii nchi itoke kwenye ugonjwa wa rushwa. Anzieni juu bwana siyo hao wadogo.tunasubiria fedha ya viroba vya stanbic bank vichunguzwe bwana Hosea. Ukimya unatutisha mno ninyi PccB.hiyo kinga ya viongozi ya kushtakiwa bwana yapaswa ifutwe kabisa. Huwezi kufanya uhalifu kisha useme unayo kinga. Bwana Hosea fanya kazi..au bajeti yako imeminywa na washkaji wa huko juuu.....
 
danganya toto we subiri uone kama kuna atakayechukuliwa hatua, Tz ni nchi inayoishi viumbe wa ajabu sana
 
Wamewakamata, sawa. Wamewafanyaje? Wamewahoji na kuridhika kuwa haikuwa rushwa na wamewaachia!! Karibu wote stori inafanana na hiyo!!
 
PCB ilikuwa bora kuliko PCCB. Hii ya siku hizi haijawahi kumshtaki mhusika mkuu wa ufisadi na rushwa kubwa. Unasoma tu katika magazeti wamemkamata samaki mdogo tu. Mapapa yanadunda tu tena bahari ya kina kirefu bila woga.wezi wakubwa walianzisha kampuni zilizonufaika na escrow. Yule kijana yuko wapi siku hizi....aaliposikia escrow tu akaenda nje.. yule mganda mtz wa mazeee huko juu
 
Mleta mada kachomelea kila kitu huu ni mpango mzima; jamaa wanapanga vifaa dola kusomba wagombea wa ukawa katika kapu kwa kisingizio chochote na hawatolewi ndani mpaka uchaguzi upite. Edo jipange wenzako hao unawajua fresh
 
Kama fisadi ndio anagombea urais tena kupitia upinzani ambamo ndio wananchi wanaimani nao itakuwa wagombea ubunge na udiwani? Watanzania tufanyeni kazi tuu tulipe kodi zao hawa wanasiasa lao moja wasitutanie

Mlishaambiwa kama mna evidence pelekeni mahakamani pia rais wenu ndo aliruhusu mkataba wa Richmond uendelee
 
Mleta mada kachomelea kila kitu huu ni mpango mzima; jamaa wanapanga vifaa dola kusomba wagombea wa ukawa katika kapu kwa kisingizio chochote na hawatolewi ndani mpaka uchaguzi upite. Edo jipange wenzako hao unawajua fresh

Hawa ccm wameshaona Watanzania Mazuzu, yaani wanatumia Taasisi hii kujipanga ili kuharibu mpango Mzima, hivi Nape kuna mtu mwenye jeuri ya kumkamata na kumuhoji eti mambo ya Rushwa.
Wamechelewa sana, huyu wangemkwatua akiwa kule, huku hakuna mchezo wa Rushwa. Ni Watanzania tu walishaamua kuamua ya kwao.
 
ila siyo ya mkoa wa DODOMA nasema HAPANA jimbo LA kibakwe kwa simbachawene tulikuwa tunapanga foleni unakula ten elfu kisha unaambiwa simbachawene anahitaji kula yako hata siye tuliokuwa kilomita 5 tulizifuata msangambuya tukapiga tena hapa Mtera staff ten nyingine ila tulimtosa kula zetu tulimpa mwenzake hatununuliki kwa buku20 takukuru walikuja na land cruiser hard top nyeupe ina namba za magumashi walikuwa wanaendelea na shughuri zao tu.
 
Hayo maigizo wameelekezwa kama walivyoelekezwa traffic barabarani,tra na machine
 
Back
Top Bottom