Hii ni sawa kweli?

Hii ni sawa kweli?

jungle boy

Senior Member
Joined
Aug 6, 2015
Posts
107
Reaction score
27
Habari ya jumapili ndugu zangu,

Namshukuru Mungu mi ni mzima ila naamini hata nyinyi ni wazima na kwa wale walio wagonjwa nawapa pole Mungu awaponye.Naomba ndugu zangu tusaidiane katika hili navyojua mtu akiwa ndani ya mahusiano ni lazima kwanza ajitambue na atambue thamani yake na ya mwenzi wake(mume/mke) au hata kama bado ni wachumba.

Sasa nikizungumzia kwa upande wa hawa wanawake/mabinti.Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanawake/mabinti kuvaa nguo zisizowasitiri vema miili yao matharani utakuta msichana ana mtu wake(mchumba/mpenz) lakini nguo anazovaa jamani si za heshima, mtu anavaa kimini na bado kina mpasuo akitembea mapaja yote nje akikaa ndio usiseme.

Mpaka yeye mwenyewe anajistukia anaanza kuficha kwa mbele akitumia kitambaa lakini ukichunguza unagundua ana mpenz wake au ana mume wake sasa jamani hii ni sawa kweli hizo sehemu nyeti kwanini asifaid mumeo chumbani kuzitazama?

Wana jamvi naomba tusaidiane kwa nini hawa wanawake/mabint huvaa hivi licha ya kuwa ndani ya mahusiano? Na je hii ni sawa?Naomba niiweke mada mezani..michango yenu inahitajika.

Karibuni tuelimishane
 
Sio sawa,
Lakini wewe muhusika unaemiliki mchumba,mke unanafasi kubwa sana kwenye mavazi yanayomfaa mpenzi wako.
 
Ishhhhh kwani tunavaa vimini ili kutafuta wachumba?
 
Ni tabia ambazo wanakuwa nazo kabla hata hawajawa na hao watu wao. Kwa hiyo hata akipata mtu bado ataendeleza tabia zake zile zile.
 
Kuna wenzi wengine wanachangia mazingira hayo, wakati mwingine nguo hizo wananunua wenyewe. Wengine wanaona fahari kuonekana ana mwenza kifaa kwa kuonyesha maumbile yake.
 
Wakati unamfuata alikuwa anavaaje?? Why now umpangie?
 
Hivi hii tabia ya kufatilia mambo ya wengine WABONGO mtaiacha lini???

Wewe unashangaa KIMINI, mwingine anamshangaa anayevaa MADELA, mwingine anamshangaa
anayevaa BAIBUI.

Jali mambo yako bro, usiumize kichwa kwa jambo lisilokuhusu.
 
jungle boy

We ukiwaona fumba macho sisi twaangalia tu ����
 
Last edited by a moderator:
nimeelewa na nnauliza tena kwani kuwa na mchumba ndo tuvae madera? Kwani vimini tunavaa ili kutafuta wachumba?

Tusaidie huwa mna maana gani maana huku si kutafuta kupendeza wakati mwingine mschana anavaa nguo ambayo inaonyesha maumbile yake mpaka nguo ya ndani inajulikana rangi yake lakin uyo ni mpenz wa mtu sasa uku ni kutafuta kupendeza? Tusaidie tufahamu
 
Hivi hii tabia ya kufatilia mambo ya wengine WABONGO mtaiacha lini???

Wewe unashangaa KIMINI, mwingine anamshangaa anayevaa MADELA, mwingine anamshangaa
anayevaa BAIBUI.

Jali mambo yako bro, usiumize kichwa kwa jambo lisilokuhusu.

Kinachozungumziwa hapa si kufatilia mtu tunasaidiana na kupanuana mawazo ila kama una mpenz na anavaa ivo na wewe umeridhia haina tatizo but naamin wapo ambao wapenz wao wako ivo na hawapend wawe ivo na ndio maana tunajengana
 
Wakati unamfuata alikuwa anavaaje?? Why now umpangie?

Kila kitu kina kanuni tabia ni lazima zibadilike kutokana na muda na mazingira mambo uliyokuwa unayafanya wakati upo single siyo utakayofanya unapokuwa na mtu na ndiyo maana kuna kitchen party lazima ufundwe
 
jungle boy

We ukiwaona fumba macho sisi twaangalia tu ����

Nimewaona halaf nikafumba macho si sawa na buree si nakuwa nmeshaona....hata nikiona sinaga misisimko ya teenager
 
Last edited by a moderator:
Biashara ni matangazo dogo!
Vitendo vinaongea zaidi kuliko maneno!
 
Hii dunia maadili yalishatupwa chooni.cha msingi jali mambo yako
 
Back
Top Bottom