Hii ndo sinema ya Nazir Karamagi

ebaeban

JF-Expert Member
Jan 15, 2012
2,205
2,695


Alichaguliwa kuwa mbunge na kuteuliwa kuwa waziri katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, akiwa waziri wa nishati na madini mda mfupi tu akaumilikisha mgodi wa dhahabu wa buzwagi kwa wawekezaji, mkataba huo inasemekana ulikuwa mbovu kuliko yote iliyowekwa na serikali ya awamu ya nne ya Mhe. Kikwete , mkataba huo unaruhusu wageni wavune raslimali ya dhahabu kwenda nje na kuwaacha wazawa wakiwa ni maskini wa kutupwa, pia mkataba huo ulitiliwa sahihi nje ya nchi huko katika hotel moja Uingereza inasemekena mihuri mingine ya wizara ilisafirishwa kwenda Uingereza kufanikisha mkataba huo tata na kurudi tena Tanzania katika ofisi za wizara.

Uharaka wa kupitisha mkataba huo ulizua wingu la rushwa au 10% kiasi Mbunge wa Kigoma kusini Mhe. Zitto Kabwe kupeleka mswada binafsi bungeni kuhoji uhalali wa mkataba huo, bunge lilijadili hoja hiyo ambapo mwisho wa siku ikaonekana Mhe. Zitto Kabwe amelidanganya bunge na Mhe. Mzihir Mzihir mbunge wa Mkinga CCM akapendekeza Mhe. Zitto Kabwe afukuzwe kwenye bunge asimamishwe vikao vitatu.

Wakati Mhe.Zitto kabwe akitumikia adhabu yake na kumbuka ilikuwa mwezi wa Ramadhani mwaka 2007 Mhe. Mzihir Mzihir jioni moja hapo mjini Lindi katika eneo la SIDO barabara kuu itokayo mnazi mmoja kwenda mjini Lindi alipata ajali mbaya ya gari alilokuwa anaendesha mwenyewe kiasi mkono wake wa kulia ulikatwa na aliwekewa mkono wa bandia wakati amaelazwa akiuguza majeraha yake Mhe. Zitto Kabwe alimtembela hospitalini kumjulia hali. Baadae katika uchaguzi wa 2010 hakuweza kutetea nafasi yake na alihama kabisa mkoani Lindi akahamia Kinondoni DSM na alisema hana haja ya kumfanyia mtu kampeni yeyote tu achukue jimbo.

Haikupita muda ikabainika ule mkataba alioingia nao Mhe, Nazir Karamagi ulikuwa ni mkataba fake na alivunja taratibu fulani kuufikia basi Spika wa Bunge Mhe. Samwel Sitta akaifuta adhabu aliyopewa Mhe. Zitto Kabwe kwa kuwa alichomtuhumu Waziri Karamagi kilikuwa ni cha kweli basi Spika akaamulu Zitto Kabwe aanze kuhudhuria vikao vya kamati yake ya bunge na kwamba adhabu imefutwa kwa kuwa bunge ndio lilionekana kusema uwongo.

Muda si mfupi Nazir Karamagi uwaziri wake ulitenguliwa pamoja na Mhe. Msabaha na wengine katika lile sakata kuu la richmund hii ni pamoja na Waziri mkuu alipoteza wadhifa wake. Nakumbuka Mhe. Msabaha alikuwa anajazba wakati anatangaza kujihudhuru kwake bungeni alimwambia Mhe. Spika Sitta amejua kula wali wa nazi ndio shida, na Spika alimshukuru kwa comment hiyo.

Baadae Nazir Karamagi akawa tajiri mkubwa na kumiliki hisa nyingi kwenye kampuni ya TICT inayoshughurika na kutoa makontena bandalini pia alinunua magodawn ya kutunzia korosho huko wilaya ya Newala kwa ujumla mwenzetu ndo akawa ametoka.

Kudhihirisha umaskini uliotokana na mchezo mchafu wa Wazir Karamagi nenda kata ya Njengwa au Mnima huko Mtwara kwenye jimbo la Mhe. Hawa Ghasia utakuta watu maskini kweli kweli chakula wanachokula peke yake ni kivutio cha utalii maana ni unga wa mhogo mkavu aliosagwa hadi unakuwa kama mweusi hivi na mboga chilimundu dagaa zilizokaa mda mrefu , ukipita na kuwaona wanakula utaona kama wanachukua vitu vyeusi wanaweka mdomoni ni lazima utavutiwa usogee uone wanakula nini.

Huyo ndio Nazir Karamagi ashomile toka Kagera.
 
Alichaguliwa kuwa mbunge na kuteuliwa kuwa waziri katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, akiwa waziri wa nishati na madini mda mfupi tu akaumilikisha mgodi wa dhahabu wa buzwagi kwa wawekezaji, mkataba huo inasemekana ulikuwa mbovu kuliko yote iliyowekwa na serikali ya awamu ya nne ya Mhe. Kikwete , mkataba huo unaruhusu wageni wavune raslimali ya dhahabu kwenda nje na kuwaacha wazawa wakiwa ni maskini wa kutupwa, pia mkataba huo ulitiliwa sahihi nje ya nchi huko katika hotel moja Uingereza inasemekena mihuri mingine ya wizara ilisafirishwa kwenda Uingereza kufanikisha mkataba huo tata na kurudi tena Tanzania katika ofisi za wizara.

Uharaka wa kupitisha mkataba huo ulizua wingu la rushwa au 10% kiasi Mbunge wa Kigoma kusini Mhe. Zitto Kabwe kupeleka mswada binafsi bungeni kuhoji uhalali wa mkataba huo, bunge lilijadili hoja hiyo ambapo mwisho wa siku ikaonekana Mhe. Zitto Kabwe amelidanganya bunge na Mhe. Mzihir Mzihir mbunge wa Mkinga CCM akapendekeza Mhe. Zitto Kabwe afukuzwe kwenye bunge asimamishwe vikao vitatu.

Wakati Mhe.Zitto kabwe akitumikia adhabu yake na kumbuka ilikuwa mwezi wa Ramadhani mwaka 2007 Mhe. Mzihir Mzihir jioni moja hapo mjini Lindi katika eneo la SIDO barabara kuu itokayo mnazi mmoja kwenda mjini Lindi alipata ajali mbaya ya gari alilokuwa anaendesha mwenyewe kiasi mkono wake wa kulia ulikatwa na aliwekewa mkono wa bandia wakati amaelazwa akiuguza majeraha yake Mhe. Zitto Kabwe alimtembela hospitalini kumjulia hali. Baadae katika uchaguzi wa 2010 hakuweza kutetea nafasi yake na alihama kabisa mkoani Lindi akahamia Kinondoni DSM na alisema hana haja ya kumfanyia mtu kampeni yeyote tu achukue jimbo.

Haikupita muda ikabainika ule mkataba alioingia nao Mhe, Nazir Karamagi ulikuwa ni mkataba fake na alivunja taratibu fulani kuufikia basi Spika wa Bunge Mhe. Samwel Sitta akaifuta adhabu aliyopewa Mhe. Zitto Kabwe kwa kuwa alichomtuhumu Waziri Karamagi kilikuwa ni cha kweli basi Spika akaamulu Zitto Kabwe aanze kuhudhuria vikao vya kamati yake ya bunge na kwamba adhabu imefutwa kwa kuwa bunge ndio lilionekana kusema uwongo.

Muda si mfupi Nazir Karamagi uwaziri wake ulitenguliwa pamoja na Mhe. Msabaha na wengine katika lile sakata kuu la richmund hii ni pamoja na Waziri mkuu alipoteza wadhifa wake. Nakumbuka Mhe. Msabaha alikuwa anajazba wakati anatangaza kujihudhuru kwake bungeni alimwambia Mhe. Spika Sitta amejua kula wali wa nazi ndio shida, na Spika alimshukuru kwa comment hiyo.

Baadae Nazir Karamagi akawa tajiri mkubwa na kumiliki hisa nyingi kwenye kampuni ya TICT inayoshughurika na kutoa makontena bandalini pia alinunua magodawn ya kutunzia korosho huko wilaya ya Newala kwa ujumla mwenzetu ndo akawa ametoka.

Kudhihirisha umaskini uliotokana na mchezo mchafu wa Wazir Karamagi nenda kata ya Njengwa au Mnima huko Mtwara kwenye jimbo la Mhe. Hawa Ghasia utakuta watu maskini kweli kweli chakula wanachokula peke yake ni kivutio cha utalii maana ni unga wa mhogo mkavu aliosagwa hadi unakuwa kama mweusi hivi na mboga chilimundu dagaa zilizokaa mda mrefu , ukipita na kuwaona wanakula utaona kama wanachukua vitu vyeusi wanaweka mdomoni ni lazima utavutiwa usogee uone wanakula nini.

Huyo ndio Nazir Karamagi ashomile toka Kagera.
Hadithi yako inatufundisha nini?
 
Huyu ndio swahiba wa Lowasa, kama 2015 EL angeshinda Karamagi angepewa shavu jingine kuja kutupiga haswaaa.
 
Ile tume iliyoapishwa juzi na Mh.Raisi itafufua yote yaliyofichika likiwamo la Mgodi wa Buzwagi. Mafisadi wote waliohusika katika ufisadi wa madini na mjkataba yake mibovu ikiwamo na kufunguliwa akaunti za ferha NONO nje ya nchi waanze kujiandaa kwa vifungo virefu magerezani, na pengine wengi wao watafia huko Magerezani. JPM hana utani; Anzeni sasa kujiandaa kuishi maisha ya kishetani. Muda wenu wa kutanua umeishia pabaya, na hili liwe fundisho kwa Watanzania wote. Ninawashauri nyie Mafisadi wa Madini muanze kufanya booking kwenye magereza mtakayofungiwa, Anzeni sasa kutoa misaada ya huduma za jamii kwenye magereza kama vile magodoro, mablanketi, matrekta ili mtakapofungwa muitumie misaada mliyotoa. Matrekta yatawasaidia msitumie jembe la mkono labda kwenye kupalilia bustani msije mkapinda migongo yenu haraka mkafa mapema kabla ya KUHENYA!!!! Mawashauri nyie mafisadi msipite karibu na Mahakama, Magereza au kukutana na Majaji msije mkafa kwa Shinikizo la damu kabla hamjahukumiwa.
 
Baadae Nazir Karamagi akawa tajiri mkubwa na kumiliki hisa nyingi kwenye kampuni ya TICT inayoshughurika na kutoa makontena bandalini pia alinunua magodawn ya kutunzia korosho huko wilaya ya Newala kwa ujumla mwenzetu ndo akawa ametoka.
Kwamba Nazir Kalamagi ni moja ya mafisadi ya kutisha nchi hii ni jambo lisilo na mjadala!! Hata hivyo, umiliki wa sehemu ya TICTS haukutokana na ufisadi wa Buzwagi... hii aliipata enzi za Che Ben hata kabla hajawa mbunge!!!!

Moja ya mambo ya kushitusha ambayo Kalamagi aliyafanya kwenye Mkataba wa Buzwagi ni pale aliposafiri hadi London kwenda kuingia mkataba wa kuuziana mgodi!! Kwa mujibu wa ZZK, mkataba ulisainiwa hotelini!!!

Anyway, mwaka 2015 nilimuogopa sana Lowassa lakini sikuwa namuogopa Lowassa kama Lowassa bali nilikuwa nawaogopa watu wanaomzunguka Lowassa na huyu Kalamagi ni mmoja wao!! Kalamagi wala hana tofauti na Rostam... haya yote ni mafisadi yaliyokubuhu huku yakifuatiwa na fisadi mjanja na mwenye akili Joka la Makengeza... mtu anayeitumia akili yake kutuibia!!
 
Ile tume iliyoapishwa juzi na Mh.Raisi itafufua yote yaliyofichika likiwamo la Mgodi wa Buzwagi. Mafisadi wote waliohusika katika ufisadi wa madini na mjkataba yake mibovu ikiwamo na kufunguliwa akaunti za ferha NONO nje ya nchi waanze kujiandaa kwa vifungo virefu magerezani, na pengine wengi wao watafia huko Magerezani. JPM hana utani; Anzeni sasa kujiandaa kuishi maisha ya kishetani. Muda wenu wa kutanua umeishia pabaya, na hili liwe fundisho kwa Watanzania wote. Ninawashauri nyie Mafisadi wa Madini muanze kufanya booking kwenye magereza mtakayofungiwa, Anzeni sasa kutoa misaada ya huduma za jamii kwenye magereza kama vile magodoro, mablanketi, matrekta ili mtakapofungwa muitumie misaada mliyotoa. Matrekta yatawasaidia msitumie jembe la mkono labda kwenye kupalilia bustani msije mkapinda migongo yenu haraka mkafa mapema kabla ya KUHENYA!!!! Mawashauri nyie mafisadi msipite karibu na Mahakama, Magereza au kukutana na Majaji msije mkafa kwa Shinikizo la damu kabla hamjahukumiwa.
Anaenda mwaka wa pili sasa... hadi hapa tulipo amefunga wangapi?!
 
Back
Top Bottom