Hii ndo sababu kubwa ya kwanini ulevi hauwezi kuisha Rombo

Steven mushi mushi

JF-Expert Member
Jul 25, 2016
533
737
8cdf3357060d3796afbf7c78c4e2d974.jpg


Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro ni moja kati ya wilaya zinazoongoza kwa ulevi hapa Tanzania ikiwa pia ni wilaya inayoongoza kwa kuwa na aina nyingi ya pombe za kienyeji duniani kote.
Ukiachana na kinywaji chao cha mbege ambacho ndicho kinachojulikana zaidi kama pombe yao ya kienyeji, zipo pia aina nyingine nyingi za pombe kama kisesei, kimorali, kiboboso, sifa, na nyingine nyingi.
Wananchi wa wilaya hii wamejikita zaidi katika matumizi ya pombe badala ya kufanya kazi za kuwaingizia kipato na waathirika wakubwa wa pombe katika wilaya hii ni vijana ambao kutwa kucha hutumia muda wao kwenye mambo ya ulevi.

Licha ya kuchukuliwa hatua mbalimbali za kutokomeza ulevi wilaya hapa hatua hizo zimegonga mwamba na hii ni kutokana na kuwa viongozi wa wilaya hii ndio vinara wa kutengeneza pombe hizi na haohao viongozi hupewa rushwa na watu ili kuruhusu matumizi ya pombe hizi haramu ikiwemo chang'aa.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro bwana mek sadick pamoja na mkuu wa wilaya ya Rombo waliwahi kulikemea sana suala hili la ulevi pamoja na kuwashutumu viongozi kwa kuruhusu jambo hili kuendelea kushamiri katika wilaya hii. Na moja kati ya maeneo yanayoongoza kwa ulevi katika wilaya hii ya Rombo ni pamoja na Samanga,.

Ubetu, Kahe, Lesoroma pamoja na Msinga yakiwa ndiyo maeneo vinara ya ulevi katika wilaya hii. Hivyo basi kama serikali ina nia thabiti ya kupunguza na kutokomeza ulevi katika wilaya hii haina budi kuanza na viongozi wa wilaya hii kwani wao ndo vinara wakuu kuanzia balozi wa nyumba kumi, wenyekiti wa mitaa pamoja na wasimamizi wa halmashauri.
Tuungane kutokomeza ulevi Rombo pamoja na wilaya nyingine ambazo zimeshamiri kwa ulevi kwani ulevi unaathari kubwa kwa jamii na Taifa kwa ujumla kutokana na kuathiri shughuli za kijamii pamoja na vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa letu. TOGETHER WE CAN
 
8cdf3357060d3796afbf7c78c4e2d974.jpg
Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro ni moja kati ya wilaya zinazoongoza kwa ulevi hapa Tanzania ikiwa pia ni wilaya inayoongoza kwa kuwa na aina nyingi ya pombe za kienyeji duniani kote. Ukiachana na kinywaji chao cha mbege ambacho ndicho kinachojulikana zaidi kama pombe yao ya kienyeji, zipo pia aina nyingine nyingi za pombe kama kisesei, kimorali, kiboboso, sifa, na nyingine nyingi. Wananchi wa wilaya hii wamejikita zaidi katika matumizi ya pombe badala ya kufanya kazi za kuwaingizia kipato na waathirika wakubwa wa pombe katika wilaya hii ni vijana ambao kutwa kucha hutumia muda wao kwenye mambo ya ulevi. Licha ya kuchukuliwa hatua mbalimbali za kutokomeza ulevi wilaya hapa hatua hizo zimegonga mwamba na hii ni kutokana na kuwa viongozi wa wilaya hii ndio vinara wa kutengeneza pombe hizi na haohao viongozi hupewa rushwa na watu ili kuruhusu matumizi ya pombe hizi haramu ikiwemo chang'aa. Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro bwana mek sadick pamoja na mkuu wa wilaya ya Rombo waliwahi kulikemea sana suala hili la ulevi pamoja na kuwashutumu viongozi kwa kuruhusu jambo hili kuendelea kushamiri katika wilaya hii. Na moja kati ya maeneo yanayoongoza kwa ulevi katika wilaya hii ya Rombo ni pamoja na Samanga,. Ubetu, Kahe, Lesoroma pamoja na Msinga yakiwa ndiyo maeneo vinara ya ulevi katika wilaya hii. Hivyo basi kama serikali ina nia thabiti ya kupunguza na kutokomeza ulevi katika wilaya hii haina budi kuanza na viongozi wa wilaya hii kwani wao ndo vinara wakuu kuanzia balozi wa nyumba kumi, wenyekiti wa mitaa pamoja na wasimamizi wa halmashauri. Tuungane kutokomeza ulevi Rombo pamoja na wilaya nyingine ambazo zimeshamiri kwa ulevi kwani ulevi unaathari kubwa kwa jamii na Taifa kwa ujumla kutokana na kuathiri shughuli za kijamii pamoja na vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa letu. TOGETHER WE CAN

MKUU,
GHARAMA ZA MAHARI ZIPOJE KWA SASA HUKO?

KWA MAZINGIRA YALIVYO
UPO UWEZEKANO WA KUPATA MKE KWA BUKU 8 HUKO?

NIJUZE FASTA MKUU.
 
Inasikitisha. ...MOLA aingilie kati kwa kweli hamna jinsi. ..
 
Duh! kumbe wakiwa kwao wako hivyo mbona wakija huku wako tofauti sana na wanachapa kazi!!!!!
 
Kweli mkuu
Hebu turudi nyuma na kuangalia wachaga tulikosea wapi? Huu si ulevi bali ni mapepo yanayo taka kuangamiza vizazi vyetu . ..kwani kilicho waponza RED INDIANS marekani NI WHISKY. ..kina mama wa kichaga tuache kuuza pombe ya aina yeyote na TUMWANGUKIE MWENYE ENZI MUNGU. ..tutubu dhambi zetu zote chini ya miguu ya MOLA kila mmoja kwa imani yake. ..HAKIKA MWENYE ENZI MUNGU ATATUREHEMU VIZAZI VYETU MILELE. ..
 
99.9999% ya warombo ni wanywaji pombe, more than 50% ni walevi.
 
Wewe acha ku paint Rombo eti hawafanyi kazi wanakunywa tu, wanaokunywa sio wote na watu wa Rombo ni kati ya wafanyakazi wakubwa nchi hii, hii inajithibitisha Rombo na miji amabayo Warombo wapo..
Nenda Rombo watu walivyojenga nyumba, kusomesha watoto, kujenga madarasa na zahanati alafu unasema hawafanyi kazi??
Kuanzia Arusha, Morogoro, Dar na kwingineko kuna mitaa inayoitwa Rombo, kutokana na influence ya watu wa Rombo sehemu hizo, unadai Rombo hawafanyi kazi wanakunywa tu


Wanakunywa pombe ndio ila sio wavivu

Halafu wewe ndio ulianzisha hii thread?

Maajabu ya wilaya ya Rombo-Kilimanjaro
 
Back
Top Bottom