youngsharo
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 2,491
- 500
Nimekuwa nikijiuliza kwanini Ccm wanasema mbele kwa mbele?
katika kukaa kwangu vijiwe vya siasa hasa mimi napenda kukaa na makada wa ccm, na wengi wao wananitambua mimi kama mfuasi wa Ccm, na huwa nafanya hivyo ili kuwadadisi na kupata habari za ndani na zikiwepo nyingine za siri kabisa ndani ya chama.
Sitaki kusema tulianzia wapi lakini kutokana na maelezo yao nilipata tafsiri ya kauli yao ya "CCM MBELE KWA MBELE",
Wanamaanisha nini?
Ccm mbele kwa mbele inamaanisha Tusikumbuke ya nyuma, Tusikumbuke Uchafu Walioufanya, ila tuendelee kwenda mbele kwenye kina kirefu zaidi tukazamishwe.
wanataka tusahau Twiga kupanda ndege, tusahau mabilioni waliyobeba, tusahau walivyotuambia tupige mbizi, ila tu tusonge mbele.
Kwanini tusianzie nyuma ndo tusonge mbele? sasa basi huko mbele kwa mbele nendeni wenyewe na jahazi lenu, watanzania wameamka.
Tunataka kufanya mabadiliko hatuwezi kwenda mbele kwa mbele ilihali hatujui tuendako.
katika kukaa kwangu vijiwe vya siasa hasa mimi napenda kukaa na makada wa ccm, na wengi wao wananitambua mimi kama mfuasi wa Ccm, na huwa nafanya hivyo ili kuwadadisi na kupata habari za ndani na zikiwepo nyingine za siri kabisa ndani ya chama.
Sitaki kusema tulianzia wapi lakini kutokana na maelezo yao nilipata tafsiri ya kauli yao ya "CCM MBELE KWA MBELE",
Wanamaanisha nini?
Ccm mbele kwa mbele inamaanisha Tusikumbuke ya nyuma, Tusikumbuke Uchafu Walioufanya, ila tuendelee kwenda mbele kwenye kina kirefu zaidi tukazamishwe.
wanataka tusahau Twiga kupanda ndege, tusahau mabilioni waliyobeba, tusahau walivyotuambia tupige mbizi, ila tu tusonge mbele.
Kwanini tusianzie nyuma ndo tusonge mbele? sasa basi huko mbele kwa mbele nendeni wenyewe na jahazi lenu, watanzania wameamka.
Tunataka kufanya mabadiliko hatuwezi kwenda mbele kwa mbele ilihali hatujui tuendako.