Hii ndiyo sababu inayoweza kupelekea watu wengi kufa kwa COVID-19 katika nchi za Afrika

42774277

JF-Expert Member
Aug 24, 2018
6,833
8,811
Africa ndio sehemu ambayo kuna kundi la watu wengi ambao wanaumwa magonjwa yasiyoambukizwa.

Kwa taarifa za mwaka jana mwishoni 60% ya vifo vyo vinavyotokea Africa husababishwa na magonjwa yasiyoambukizwa, Yaani kwa lugha rahisi ya hesabu ni kwaka katika kila vifo 100 barani Africa, basi vifo 60 husababishwa na magonjwa yasiyoambukizwa.

Asilimia 60 ya vifo Afrika vinatokana na magonjwa

Kiuhalisia hizi figure zinatisha mno. Na ukija kuangalia utakuja kugundua katika hivyo vifo 60 asilimia kubwa ya hivyo vifo vinasababishwa na magonjwa ya moyo.

Magonjwa ya moyo huku Barani Africa yanasababishwa na sababu mbili kubwa.

1. Utaratibu mbovu wa ulaji wa chakula.

Africa huenda ndiyo sehemu ambayo ni ufahari mtu kuwa na kitambi au kuwa na mwili mkubwa. Hii husababishwa na watu kula ovyo.

Ulaji wa watu wengi wa Africa naweza kuufananisha na ulaji wa Nguruwe (Mliofuga nguruwe mnajua nguruwe wanakulaje). Ulaji mbovu wa chakula hupelekea mtu kuwa na uzito uliopitiliza (Obesity) na hivyo kupelekea mtu kupata magonjwa ya moyo.

2. Watoto wengi Africa huzaliwa wakiwa na matatizo ya moyo.

Inasemekana barani Africa kila mwaka watoto 10,000 huzaliwa wakiwa na matatizo ya moyo.

Hapo bado sijagusa watu ambao wana magonjwa mengine sugu ambayo yanawasumbua.

Kuna utafiti ulifanuika mwaka 2012 na Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete, waligundua kwamba robo 3 ya watanzania wanaugua magonjwa ya moyo. Je leo hii hali ikoje?

Kwa kifupi Africa kuna kundi kubwa tu la watu ambao wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali sugu. Hawa wote wapo kwenye risk kubwa sana ya kufa endapo wataambukizwa Corona.

Na huenda ndio maana mapema wiki hii UN walisema kwamba ndani ya wiki 3 zijazo Africa itegemee kichapo kikubwa sana kutokana na virusi hivi vya corona.

Hali inaweza kuwa mbaya kuliko ambavyo watu wengi wanafikiria.
 
.
Screenshot_20200404-101053.jpeg
 
Siyo lazima ukibaliane na nilichoandika.

Ila the truth ni kwamba wengi wanatembea huku ni wagonjwa...
Unafikir hii ngoma inadondosha wagonjwa tu!! Kuna nchi ulaya hazihesabu vifo vya corona kama ulikuwa na magonjwa mengine na daily wanarekodi vifo.
 
Boss hapo kwenye mlo kamili ungesema na Maji safi na Mazoezi.
 
Dr. anayehudumu kule Canada ndie kasema ukweli, kasema kuwa Covid 19 msidaganyane kuwa haitawapata kwa kunawa na kutumia vitakasa mkono na kuvaa mask.

Yeye kasema huu ugojwa hauepukiki isipokuwa kwa wale watakaojifungia ndani. Amewaomba Wacanada wamsaidie jambo moja tu ili asife na wasife na Corona nalo ni kujifungia ndani tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishindwa kujicontrol kwenye chakula basi kufanya mazoezi ni kazi bure. Na ndio maana watu wengi wanalalama kwamba wanafanya mazoezi lakini miili yao haipungui.
Boss hapo kwenye mlo kamili ungesema na Maji safi na Mazoezi.
 
Unafikir hii ngoma inadondosha wagonjwa tu!! Kuna nchi ulaya hazihesabu vifo vya corona kama ulikuwa na magonjwa mengine na daily wanarekodi vifo.
Nadhani hujanielewa nilichoandika. Nimekuambia mtu akiwa na magonja hayo niliyoyaelezea anakuwa kwenye risk kubwa ya kufa kwa corona.

Hata kama tutasema huyu mtu alikuwa na magonjwa mengine. Tutaangalia kilichomuua, kama respiratory system itafeli then akafa. Tutasema amekufa kwa corona.
 
Dr. anayehudumu kule Canada ndie kasema ukweli, kasema kuwa Covid 19 msidaganyane kuwa haitawapata kwa kunawa na kutumia vitakasa mkono na kuvaa mask.

Yeye kasema huu ugojwa hauepukiki isipokuwa kwa wale watakaojifungia ndani. Amewaomba Wacanada wamsaidie jambo moja tu ili asife na wasife na Corona nalo ni kujifungia ndani tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwamba mask na kunawa mikoni hakusaidii sina uhakika. Otherwise wahudumu wa afya kwenye nchi zilizoathirika wangekuwa kwenye hali mbaya sana.
 
Mitandao inazidisha hofu hivyo kufanya mioyo izidi kupanuka na kusinyaaa
 
Sahihisha Useme yakuambukiza na si yasiyoambukiza. Ulaya vifo vyao ni vya magonjwa yasiyoambukiza-non-infectious diseases. Sisi tunapukutika na infectious diseases mkuu 42774277
 
Nadhani hujanielewa nilichoandika. Nimekuambia mtu akiwa na magonja hayo niliyoyaelezea anakuwa kwenye risk kubwa ya kufa kwa corona.

Hata kama tutasema huyu mtu alikuwa na magonjwa mengine. Tutaangalia kilichomuua, kama respiratory system itafeli then akafa. Tutasema amekufa kwa corona.
Nimekuelewa...Nilikuwa naongezea tu.... Ila tambua kuna nchi hazifanyi kama hivyo unavyodai;ukiwa na magonjwa mengine ukifa hawakuhesabu.
 
Nadhani hujanielewa nilichoandika. Nimekuambia mtu akiwa na magonja hayo niliyoyaelezea anakuwa kwenye risk kubwa ya kufa kwa corona.

Hata kama tutasema huyu mtu alikuwa na magonjwa mengine. Tutaangalia kilichomuua, kama respiratory system itafeli then akafa. Tutasema amekufa kwa corona.
Nimekuelewa...Nilikuwa naongezea tu.... Ila tambua kuna nchi hazifanyi kama hivyo unavyodai;ukiwa na magonjwa mengine ukifa hawakuhesabu.
 
Dr. anayehudumu kule Canada ndie kasema ukweli, kasema kuwa Covid 19 msidaganyane kuwa haitawapata kwa kunawa na kutumia vitakasa mkono na kuvaa mask.

Yeye kasema huu ugojwa hauepukiki isipokuwa kwa wale watakaojifungia ndani. Amewaomba Wacanada wamsaidie jambo moja tu ili asife na wasife na Corona nalo ni kujifungia ndani tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu hata ukiwa ndani unanawa mikono kila mara, usijidanganye ukiwa ndani ndio usinawe wewe nawa tu kwani sh ngapi?

The best Medicine of Corona is to Stay Home.
 
Back
Top Bottom