Hii ndio kazi ya Upinzani

Hii ndio kazi ya Upinzani

Void ab initio

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2015
Posts
5,723
Reaction score
5,662
Katika kashfa zote zifuatazo, hakuna hata moja ambayo iliwahi kuibuliwa na kuchanganuliwa na CCM.... Zote zimeibuliwa na vyama vya upinzani na kambi rasmi ya upinzani bungeni... Tuzitazame kidogo, jiulize... Ipi ambayo haujawahi kuisikia, tutakufafanulia kwa uzuri..

(.., kabla sijataja kashfa hizo, ningependa kufahamu, ni kashfa ipi yenye sura ya ubadhirifu na ufisadi ambayo iliwahi kuibuliwa na CCM!!?)

DOWANS.. LUGUMI .. RICHMOND.. ESCROW... RADAR TANGOLD.., TOKOMEZA.. MFUKO WA COMMODITY IMPORT SUPPORT.. KIWIRA.. KAGODA... UJANGILI.. EPA.. UDA... DEEP GREEN.. BUZWAGI.. UUZWAJI WA FUKWE.. UKWEPAJI KODI.. MISAMAHA YA KODI.. MABEHEWA MABOVU.. MABILIONI YA KIKWETE.. UNUNUZI WA NYUMBA YA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI ITALY.... UNUNUZI WA MAJENGO PACHA YA B.O.T.. LOLIONDO GATE... CHAVDA NA MASHAMBA YA MKONGE.. PEMBE ZA NDOVU KWENYE NDEGE YA RAIS WA CHINA.. HATI FUNGANI.., UUZWAJI NYUMBA ZA SERIKALI.. MIKATABA MIBOVU..

uchafu wote tumeufahamu kupitia uwepo wa vyama vya kisiasa vya upinzani....., bila uwepo wao, kamwe usingesikia hata neno IPTL na kufahamu nini maana ya DOWANS...

..., Unasema kazi ya upinzani nchi hii haujawahi kuiona.. Labda umeamua kujificha kwenye kivuli chako mwenyewe, hivyo umeamua kujidanganya na kufurahia uongo wako mwenyewe..

kazi ya upinzani kwa jibu rahisi ni kukosoa, kushauri, kuelekeza na kutoa njia mbadala za namna ya kufikia kilele cha maendeleo katika nchi au taasisi husika...

Kushika DOLA ni lengo maalum la chama chochote cha siasa...

(tusichanganye mambo mawili haya.., kushika dola na kazi ya chama cha upinzani)....

Anaesema kwamba huu ni mwisho wa upinzani nchini...anajidanganya mwenyewe.., ni sawa na mtu anaepiga ngoma mwenyewe na kuamua kucheza ala za muziki anazozipiga mwenyewe....

Hakuna mwisho wa upinzani kwenye nchi ya kidemokrasia yenye vyama vingi ndani yake...

Kama unafikiri kazi ya upinzani ni kupongeza chama tawala.., unajidanganya hadharani....

Mpinzani kazi yake kubwa ni kukosoa serikali na kutoa 'Alternative way' katika ushauri stahiki...

Ukiona chama cha siasa cha upinzani kinapiga makofi kwenye kila ambalo linafanywa na serikali.., hiko chama.., kinastahili kufunga ofisi zao na kufutwa katika dawati la usajili...

.., Katika mfumo wa vyama vingi kuna udhibiti wa uendeshaji wa serikali, watu hupanga namna gani sahihi ya kuendesha nchi yao.... Katika mfumo wa chama kimoja, watu wa chama hicho huamua namna ya kuendesha nchi kwa matakwa yao binafsi..,

..., Watu wanatoa maoni na wanapaswa wasikilizwe na pia mchango kutoka vyama vya upinzani unatakiwa uchukuliwe katika kufanya uamuzi kuhusu uendeshaji wa nchi na kuwaletea wananchi maendeleo.

Mfano huu unaweza kuonyesha vizuri tofauti kati ya mfumo wa chama kimoja na vyama vingi.... (nchi ya China ni nchi ya kijamaa ambayo ina chama kimoja, chama cha kikomunisti, ni tofauti na Tanzania, hapa kuna vyama vingi vya kisiasa, mfumo rasmi wa kidemokrasia wenye vyama vingi vya kisiasa)...

Tunahitaji siasa ngumu za harakati zilizojaa mikakati kwenye tawala nyingi ambazo kimsingi hazihitaji kukosolewa.. Ambazo zinajificha nyuma ya nguvu ya dola... Nashukuru kwa upinzani kuendelea kuimarika kila uchwao.. SERIKALI IMARA INATOKANA NA UPINZANI IMARA ULIOSTAWI...

Nitakuja kuendelea baadae na kipande cha mwisho kwenye maandishi yangu haya....

Martin Maranja Masese
Mwananchi wa kawaida
 
Hii wanaifuta hii!!!
Unawaumiza mabos waliomo humu na kama wangekujua live ungekoma, "wangekulimboka"
 
Tatizo kitu kinachowapofusha akili hawa ndugu zetu wanafikiri kwamba CCM ni chama chenye hati miliki hapa Tanzania.

Poor CCM.
 
Upinzani utakuwepo sana kwa maoni yangu kwa sababu kazi yao walioifanya nyuma tuliiona
But wawe na mikakati mazubuti ya kushika dola bila kuwausisha mashushu kama sumaye na mbatia
 
Kumtumia sumaye na mbatia alafu unasema mabadiliko ni kichefuchefu!!
 
Kwahio hiyo RICHMOND
Wapinzani walimuhusisha nani !?
Baada ya hapo kwanini hawataki kuzungumzia UFISADI?

Tuna vyama vya upinzani vinavyo ongozwa na Wanafiki,wazandiki na wachumia tumbo.

1469858490819-jpg.373214


Hawa sio wapinzani kwa maana ya wapinzani wanao itakia mema Tanzania Na Watanzania kwaujumla
Hawa niwapinzani kwa niaba ya Matumbo yao
 
Hii wanaifuta hii!!!
Unawaumiza mabos waliomo humu na kama wangekujua live ungekoma, "wangekulimboka"
let see tumeweka mtego kwa huyo pandikizi la ccm jf wakifuta tutakuja na nyuzi za kuuponda upinzani nao ufutwe.
 
Ttu kinachowapofusha akili hawa ndugu zetu wanafikiri kwamba CCM ni chama chenye hati miliki hapa Tanzania.

Poor CCM.
Sio kweli watu hawafikiri kuwa Ccm ina haki miliki ya Tanzania.

Tatizo nikuwa
Watanzania hawataki kuruka Mkojo na kukanyaga Kinyesi hapo tu.



"Nataka hao wanaotetea maandamano watangulie wao halafu wataona cha mtemakuni’"
 
Kwahio hiyo RICHMOND
Wapinzani walimuhusisha nani !?
Baada ya hapo kwanini hawataki kuzungumzia UFISADI?

Tuna vyama vya upinzani vinavyo ongozwa na Wanafiki,wazandiki na wachumia tumbo.

1469858490819-jpg.373214


Hawa sio wapinzani kwa maana ya wapinzani wanao itakia mema Tanzania Na Watanzania kwaujumla
Hawa niwapinzani kwa niaba ya Matumbo yao
tunaongozwa na wagonjwa
dkmagupombe.jpg
 
Kwahio hiyo RICHMOND
Wapinzani walimuhusisha nani !?
Baada ya hapo kwanini hawataki kuzungumzia UFISADI?

Tuna vyama vya upinzani vinavyo ongozwa na Wanafiki,wazandiki na wachumia tumbo.

1469858490819-jpg.373214


Hawa sio wapinzani kwa maana ya wapinzani wanao itakia mema Tanzania Na Watanzania kwaujumla
Hawa niwapinzani kwa niaba ya Matumbo yao
Zimepitwa na wakati
 
Ccm hata mtukane vipi Lowassa harudi ccm asilani semeni yite usiku mtalala
 
Tusifundishane woga demokrasia ina maana pana beyond chadema sisiemu hata kikiibuka chama chochote cha kisiasa ili mradi kimefuata sheria za nchi!
 
Kusema ukweli kama hawa kina motochini ndio vijana wa kuisaidia chama cha majipu. Basi ccm inafeli kuliko tunavyofikiria. watu wanatoa mada nzito Lumumba buku mbili wanaishia kutukana tu. Na siku zote ukiona mtu anashindwa kujibu hoja anaishia matusi huyo umemshinda.
 
Kwahio hiyo RICHMOND
Wapinzani walimuhusisha nani !?
Baada ya hapo kwanini hawataki kuzungumzia UFISADI?

Tuna vyama vya upinzani vinavyo ongozwa na Wanafiki,wazandiki na wachumia tumbo.

1469858490819-jpg.373214


Hawa sio wapinzani kwa maana ya wapinzani wanao itakia mema Tanzania Na Watanzania kwaujumla
Hawa niwapinzani kwa niaba ya Matumbo yao
walioafiki waseme ndiooo
 
Sio kweli watu hawafikiri kuwa Ccm ina haki miliki ya Tanzania.

Tatizo nikuwa
Watanzania hawataki kuruka Mkojo na kukanyaga Kinyesi hapo tu.



"Nataka hao wanaotetea maandamano watangulie wao halafu wataona cha mtemakuni’"
hapo sasa pagumu
 
Back
Top Bottom