Hii mimba vipi?

Ni mimba changa sana ina mwezi mmoja na siku kadhaa tu,na si mimba yangu ya kwanza,napata maumivu makali sana chini ya kitovu nikipumzika leo kesho mtindo mmoja,na kizazi kimeshuka kwa kiasi fulani mara nyingi kinaguswa tunapokuwa tunalea kiumbe,nimejaribu kuongea na watu wawili watatu kila mtu anasema lake.
Mwingine anasema sio dalili nzuri mimba inaweza ikachoropoka hii hali isipodhibitiwa(Kuonana na daktari) mwingine anasema hii ni hali ya kawaida itapotea yenyewe wala sihitaji kumeza hata panadol za kutuliza maumivu,mwingine anasema alipokuwa na mimba ya mapacha alikuwa na dalili hizo .Sasa nikaona si vibaya nikaja kwenu Wataalam wa jukwaa hili mnisaidie tafadhali.
[/QUOT
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom