Ndimi mvuvi halisi, Kila mvuvi analijuwa
Nivuwaye mikambisi, na papa wenye khatuwa
Wala sivui vingisi, mishipi huisumbuwa
Nimekwambiya elewa
Na nivuapo malema, huingia ndani ndani
Maji yangu ni ya pima, thalatha u thalathini
Na ndiyo ninayozama, lema nalibwaga tini
Uliza mimi n'nani?