dazu
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 365
- 76
Watanzania tuna kasumba mbaya sana ya kudharau vyetu na kutukuza vigeni tukiamini ni vizuri kuliko vyetu. Mbaya zaidi sasa hivi hata viongozi nao wanayo hii kasumba. Mwaka 1980 tuliposhiriki kwa mara ya kwanza na ya Mwisho AFCON tulikua na makocha wazalendo akina Joel Bendera. Mwaka 1993 tuliponyakua kombe la Challenge Timu yetu ya Taifa iliongozwa na wazalendo akina Mziray na Mkwasa. Serengeti boys ilipofuzu Africa miaka michache iliyopita (Kabla ya kuondolewa kwa kumchezesha Nurdin Bakari aliyedaiwa kuzidi umri wa miaka 17) ilikua na wazalendo akina Abdallah Kibaden na Sylivester Marsh. Mwaka huu Mzalendo mwingine Julio amekabidhiwa Ngorongoro Heroes, na mwendo wao tunauona kwenye kufuzu olyimpic, maana ni kama wametanguliza mguu mmoja kufuzu.
Inasikitisha Naibu waziri wa michezo haoni mchango huu wa wazalendo badala yake anaendeleza kasumba ya kupenda vigeni, na kumvunja moyo Julio kwamba Serikali ina mpango wa kutafuta kocha wa 'kigeni' katikati ya mafanikio haya ya mzalendo. Hivi kocha wetu lazima awe mgeni? Tujiulize Maximo amekaa miaka mitatu, kila siku tunapewa matumaini "Tumpe muda" huku analamba mshahara kibao. Fikiria tangu aondoke mpaka sasa hajapata timu ya kufundisha. Sasa amekuja Poulsen, hatuwezi kusema ndo kaleta kombe la challenge maana amekuta vijana walishaandaliwa. Mwenendo wa Timu yetu tunauona katika mashindano ya kimataifa. Nadhani kuna haja ya kujikomboa kifikra na kuamini kwamba Watanzania wanaweza pengine kuliko hao wageni wanaowachukua.
Inasikitisha Naibu waziri wa michezo haoni mchango huu wa wazalendo badala yake anaendeleza kasumba ya kupenda vigeni, na kumvunja moyo Julio kwamba Serikali ina mpango wa kutafuta kocha wa 'kigeni' katikati ya mafanikio haya ya mzalendo. Hivi kocha wetu lazima awe mgeni? Tujiulize Maximo amekaa miaka mitatu, kila siku tunapewa matumaini "Tumpe muda" huku analamba mshahara kibao. Fikiria tangu aondoke mpaka sasa hajapata timu ya kufundisha. Sasa amekuja Poulsen, hatuwezi kusema ndo kaleta kombe la challenge maana amekuta vijana walishaandaliwa. Mwenendo wa Timu yetu tunauona katika mashindano ya kimataifa. Nadhani kuna haja ya kujikomboa kifikra na kuamini kwamba Watanzania wanaweza pengine kuliko hao wageni wanaowachukua.