Hii ingeweka kwenye timu zetu za kibongo, ingependeza sana!

netein

JF-Expert Member
Sep 20, 2019
281
479
Ukicheza kiurojourojo tunakufyeka mshahara!
Screenshot_2020-12-29-06-50-39.jpg
 
Kwa hiyo mfano Golikipa akiboronga akafungwa kizembe inabidi team nzima mkatwa mshahara? hii sio njia sahihi ya kuimprove performance ya team,huu ni uhuni na ujanja ujanja tu ambao hautakiwi kufumbiwa macho hata kidogo.
nadhan kuna criteria wameziweka, zinazofanya hii adhabu iwe na mashiko, ingekuwa hivyo wangekuwa wanamuadhibu mchezaji mmojammoja
 
Huo ni uhuni tu na haifai timu yoyote kuiga huo ujinga. Uwekezaji kwenye soka unahitaji uvumilivu sana, hapo kinachohitajika ni kuwapa wachezaji morali ya kufanya kazi kwa nguvu na wale wavivu ni heri kusitisha mikataba nao kabisa kuliko kuwakata mishahara.

Fatilia story ya Bury FC ya nchini England utajua soka ni uwekezaji unaohitaji roho ngumu sana.
 
timu za west Africa zinajielewa na ndiyo maana wanafika mbali ligi ya mabingwa.
Samahani mkuu me naonaga huo ukanda ni dhoofu tu tena bora ya Central Africa, kama hutojali ni team gani hizo zinazofika mbali ligi ya mabingwa
 
Bongo hii hata ukija, n Sawa na Bure tu
Pesa, zenyewe za kuwalipa wachezaj
Hawana sembuse hyo kukatwa mshahara
 
Horoya ni mojawapo..
Horoya hii ni ingizo jipya mkuu baada ya kuwekeza pesa ndefu hivi karibuni ndio wameanza kuvuna matunda ila kwa kipindi kirefu team zao hazina matokeo mazuri klabu bingwa ukitoa miaka ile ya Enyimba. Ila uko sahihi kwetu uswahili ni mwingi bado
 
Back
Top Bottom