Msaada jinsi ya kupata mawasiliano na raisi magufuli, nimeomba hivyo kwa sababu nataka nimkumbushe kuwa board ya mikopo ya elimu ya juu inatesa sana wanafunzi yaani kuna wengine mpaka leo hii hatujapata boom na mpaka mabinti wameanza ukahaba kwa kukopsa pesa za kujikimu na wengi wetu tumetoka familia duni hivyo mwenye mawasiliano na raisi magufuli plz msaada wake ni wamuhimu saana.
Mimi naona hakuna uhusiano kati kukosa boom na kuwa kahaba bali ni tabia mbaya na kukosa maadili. Kama wanafunzi muoneni mkuu wa chuo na kutoa malalamiko yenu.
mkuu napata wakati mgumu kuelewa jinsi wasomi mnavyopambanua mambo. Hivi unafikiri kila kitu mpaka ashughulikie rais?
Yaani muda uliotumia kuandika kitu ambacho hakitasaidia kutatua tatizo lako, ni bora ungeutumia kuomba ushauri ni namna gani utatengeneza pesa huku ukiwa chuo na kuepuka kutegemea loan board!
Nafikiri ifike mahali waasomi tuwe solutions to problems rather source of problems.
Ni hayo tuu.
We need to think outside the box
We unashangaa watoto kuwa makahaba? Kama hawana chakula, pesa ya accommodation na nauli unategemea nini? Hakuna free gift...hata Kikwete alisema ukitaka kula lazima uliwe ..