Wadau Nahitaji sana kupata contacts za taasisi au kampuni binafsi inayoshughulika na kufanya soil analysis. Nahitaji SOil Analysis kwenye kipisi changu cha arshi kabla ya kuanza shughuli za kilimo. Mwenye contacts naomba aweke hapa.
Nashukuru sana mdau. hao ukipitia kwao mzunguko mrefu. Nimeshapiga Wizarani, na pia Tanganyika farmers association hakukua na msaada wa maana. nahitaji very specific contacts hasa kwa mdau ambaye tayari ameshafanya hichi kitu ama anafahamu kwa uhakika wahusika.
Nashukuru sana mdau. hao ukipitia kwao mzunguko mrefu. Nimeshapiga Wizarani, na pia Tanganyika farmers association hakukua na msaada wa maana. nahitaji very specific contacts hasa kwa mdau ambaye tayari ameshafanya hichi kitu ama anafahamu kwa uhakika wahusika.
kiongozi mimi sina contact za hao wataalamu, wapo tanga ila ni eneo gani la tanga sijui ila kwa urahisi uongee na hao watu wa kilimo watakupatia link na hicho kituo cha kilimo tanga otherwise pitia yelllow page book unaweza kupata au vitabu vya TTCL then tafuta hiyo taasisi ya kilimo ndio wenye bei rahisi katika uchunguzi wa udongo na watakupa ushauri zaidi lakini kama una pesa nzuri na issue ni just kufanya soil analysis basi kama upo dar unaweza enda Mkemia mkuu wa serikali au UDSM chemistry/botany department ama Kitengo cha Mazingira chuo cha Ardhi lakini tahadhari ya hizi taasisi sio specialist katika hilo eneo so you will not get a professional advise if you are in need of it.
Kama ukipata jamaa wa TACRI ( watafiti wa kilimo cha kahawa) au ukiwa na ubavu ukawapata SKU, shirika la kilimo Uyole unaweza pata majibu murua ya mahitaji yako.