Help! Help ni Mdada wa Ki TZ

Help! Help ni Mdada wa Ki TZ

NATA

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2007
Posts
4,492
Reaction score
1,313


Dada analalamika boss wake hasafishi kinywa , na wanafanya kazi katika ofisi moja ambayo ni ndogo , Hivyo anateseka sana kwani boss akiongea tu basi harufu hiyo kwake na inasambaa chumba chote na kazi yake huyu dada inamtaka awe kwenye meza yake muda wote.

Huyu ni boss wake na nimkubwa kwake kiumri anatamani amwambie but anaogopa na anamuheshimu sana anashindwa aanzie wapi.

Boss anamke na watoto, sijui huyo mke naye anaogopa kumwambia.

Anatafuta ushauri afanyeje , na kazi anaitaka na muda mwingi wa siku anatumia kuwa katika ofisi hiyo. Pia angependa kujua kama kunamadhara yoyote yatokanayo na bad smelling gases inayotoka katika midomo ya mtu.
 
Ningekuwa mimi ningetafuta namba ya mke wake alafu natafuta line mpya namfahamisha mke wake kuhusu hali ya kinywa cha mumewe , ampeleke hospital au anunulie dawa kali na nzuri pamoja na mouth wash ya kusuuza mdomoni baada ya kupiga mswaki...etc

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Hii sasa inaitwa hazardous work au poor working environment?
Hii inakera sana wa TZ wengi hawapendi kusafisha kinywa hasubuhi, sasa ukiwa ndani ya daladala umekaa jirani na mtu wa design hiyo utatamani uruke dirishani !
 
Ningekuwa mimi ningetafuta namba ya mke wake alafu natafuta line mpya namfahamisha mke wake kuhusu hali ya kinywa cha mumewe , ampeleke hospital au anunulie dawa kali na nzuri pamoja na mouth wash ya kusuuza mdomoni baada ya kupiga mswaki...etc

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Anavyodai huyu dada ni kwamba tatizo inaonekana huyu boss maswala ya mswaki kwake hayana umuhimu ni smart kutwa katinga suti safi but harufu ya kwa mdomo!
 
Pk ni mkombozi ...nunua weka mezani, then mkaribishe boss ... Utapata unafuu kidogo!!!
Full story huyo boss nikumuona daktari wa meno!
 
Pk ni mkombozi ...nunua weka mezani, then mkaribishe boss ... Utapata unafuu kidogo!!!
Full story huyo boss nikumuona daktari wa meno!

Tatizo analoliona huyu dada ni kwamba huyo boss hapendi kusafisha kinywa, kwani kunasiku ambazo ni chache sana anakuwa fresh, lkn muda mwingi anakuja na viporo vyake mdomoni.
 
Hii sasa inaitwa hazardous work au poor working environment?
Hii inakera sana wa TZ wengi hawapendi kusafisha kinywa hasubuhi, sasa ukiwa ndani ya daladala umekaa jirani na mtu wa design hiyo utatamani uruke dirishani !

Hapa itabidi aombe hardship allowances.
 
Mhh, labda hajijui

Kwani yeye hasikii hiyo harufu maana dada anadai ikiwashwa air condition chumba kizima kinanuka na hasa kama jana alitia matingasi!
 
Ningekuwa mimi ningetafuta namba ya mke wake alafu natafuta line mpya namfahamisha mke wake kuhusu hali ya kinywa cha mumewe , ampeleke hospital au anunulie dawa kali na nzuri pamoja na mouth wash ya kusuuza mdomoni baada ya kupiga mswaki...etc

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

itakuwa anatumia ugolo huyo
 
ok pole,mnunulie mouth wash kama zawadi na meseji itakua imesend, au labda ana ugonjwa, au si kinywa kinachotoa harufu lbd
 
mwambie afunge alarm ofisinii boss akija tu alarm inaanza kuimba "kaswaki, kaswaki, rudi nyumbani baba kaswaki".
 
dunia ya sasa boss hasafishi kinywa kweli inawezekana ni mgonjwa harufu inatoka tumboni sio kinywani mshauri aende hospitali
 
Hii sasa inaitwa hazardous work au poor working environment?
Hii inakera sana wa TZ wengi hawapendi kusafisha kinywa hasubuhi, sasa ukiwa ndani ya daladala umekaa jirani na mtu wa design hiyo utatamani uruke dirishani !

helooo?
 
duh ndo maana huwa nachelea kufikiria habari za kuajiriwa hii nini sasa?
 
si kwamba hapigi mswaki la!
ni mgonjwa na hajijui kama anatoa harufu kinywani
amwambie tu ili jamaa aende hosptl!
 
haya masuala hatar xana,hv inteview haya mamb n non concern
 
Back
Top Bottom