Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 213
- 357
01
Naikumbuka vema ile siku. Alinipigia simu, nami nikaipokea kwa bashasha na furaha tele. Huyu alikuwa mpenzi wangu, mwanamke aliyenipa raha mara nyingi. Hellen.
'Mambo vipi mpenzi? Uliona email niliyokutumia? Nilikujulisha kuwa narejea nchini, lakini sijapata tena nafasi ya kucheki kama ulijibu. Kuna mambo fulani fulani yalitokeza na kukatisha mawasiliano. I miss you babe!' niliongea kwa sauti ya furaha. Kawaida, mimi hutabasamu kabla hata ya kusikia sauti ya Hellen, yaani ile nikiona kwenye kioo cha simu yangu jina 'Hellen', basi moyo wangu hufukuta kwa fukuto la furaha, hata kama ningekuwa na huzuni, mie huisahau mara moja hadi pale nitakapomaliza mazungumzo. Na ni kweli kuwa jina lake kwenye simu yangu nimelihifadhi hivyo hivyo kavu kavu, "Hellen" isipokuwa tu mbele yake kuna "Hr 301". Kwa wanachuo wanaelewa hili hutokea sana hasa kwa vile mnapopangiwa seminar na kazi za makundi unasevu namba za watu mnaoshiriki hizo kazi pamoja. Na kwa vile chuoni mnakuwa watu wengi, utalazimika kutafuta namna ya kutofautisha majina. Si ajabu ukawa na Hellen kumi kwenye simu yako, na kama hujaweka ubini, ni dhahiri kuwa utahitaji kuwatofautisha kivyovyote vile. Hii ndio hupelekea mtu kuseviwa Vick cheusi, au Vick mzaramo nk. Hellen Ni mpenzi wangu, lakini jina lake sijalisevu kwa zile mbwembwe za 'my love', au 'Honey' au 'laaziz kama ilivyo kawaida ya wapenzi. Unawezajiuliza kwa nini, siyo! Nitakufahamisha hapo baadaye, lakini yeye Hellen anajua kwa nini jina lake nimelisevu kavu likifuatiwa na HR 301.
Sasa basi, naweza kusema, ingawa tupo kwenye mahusiano kwa miezi takribani minne sasa, lakini ukiniona navyotabasamu kumuona Hellen, basi unaweza kukokotoa na kupata jawabu la uongo. Ndiyo, la uongo. Utajua tu kwamba huyu jamaa, ndiyo kwanza kamuona huyu binti na amemzimikia kinoma. Kawaida, pumbazo langu la kwanza nilipokutana na Hellen mara ya kwanza miezi mitano iliyopita, basi limekuwa likibaki hivyo hivyo hata sasa baada ya miezi hii yote kila napomuona. Aisee! Huyu binti kajua kunishika. Mie zuzu wallah!.
Basi, turejee kwenye simu. Baada ya kupigiwa naye na kujitetea kabla hata hajasema kitu, nilisubiri kwa hamu niisikie sauti ya mpenzi wangu, ambayo kuisikia pekee, hunipatia burudani nafsini mwangu.
'Niliiona email Derick, na nimeshaijibu. Uko wapi?' Hellen alizungumza kwa sauti tulivu. Sauti ambayo sikuizoea. Haikuwa na ule uchangamfu wa siku zote. Najua haikuwa nao, japo alijaribu kuongea kwa kuniigizia. Namjua mpenzi wangu bwana huwezi kunidanganya kitu. 'Hellen wangu ana shida gani jamani!'. Nilijiuliza. Ah, sikuvumilia kubaki najiuliza tu, nikaamua kuondoa hilo dukuduku moyoni mwangu.
'Vipi dear, mbona umepoa hivyo mpenzi? Kunani tena darling. Eh mamii, are you sick mpenzi?' nililazimika kuhoji, ile furaha yangu ikiyeyuka kama donge la barafu kwenye joto kali. Aisee, sio siri, niambie habari gani sijui, lakini habari za huzuni hunibeba sana mimi. Nadhani, huu ni udhaifu kwangu mimi mtoto wa kiume, kuwa na hisia nzito sana au tuseme kutekwa kihisia kwa urahisi. Mimi ni mwepesi sana wa furaha na huzuni vile vile. Ndio maana najaribu kusoma soma masuala ya saikolojia, kunisaidia kuwatambua matapeli mapema. Si unafahamu matapeli wanacheza sana na hisia! Naam, matapeli buana wakikujua wewe ni mtu unayepata huzuni ukielezwa tukio la kuhuzunisha, wao ni wepesi sana kupita humo, wakakulisha habari ya msiba, ukajikuta unachangia nauli ya kwenda msibani kwa kuwaonea huruma, kutokana na matatizo chungu nzima watakayokuorodheshea.
Huzuni iliyokuwa moyoni mwangu kusikia tu ukosefu wa uchangamfu kwenye sauti ya Hellen, ungedhani nimepashwa habari za msiba.
'Siku hazilingani mpenzi, hata hivyo kiafya niko poa tu sema nimekumiss. Kama tunaweza kuonana itakuwa poa sana. Nahitaji tuongee!' Hellen alizungumza kwa utulivu ule ule.
'Ok dear, nipo Changanyikeni now. Nije au uje?' nilimtupia swali japo ilikuwa wazi kwamba alinihitaji niende. Kikawaida, akihitaji kuja kwangu, yeye huja baada ya kujibiwa message yake ya neno moja ambayo ni mimi tu naielewa 'Hr301'. Hiki ni kifupisho cha moja ya kozi ambazo zilitukutanisha mimi na Hellen miezi mitatu iliyopita. Usijali. Nitakuelezea. Najua unataka ujue ilikuwa vipi.
Itaendelea.
2
Kwa kawaida vyuoni, kozi huwa zinakuwa na majina ya vifupisho. Mfano hiyo Hr inasimama badala ya kozi inayoitwa 'human rights' (Haki za binadamu …) na hiyo 301, Sina hakika, lakini nahisi inamaanisha mwaka wa masomo. Maana kulikuwa pia hr 101 iliyofundishwa mwaka wa kwanza, hr 201 ilifundishwa mwaka wa pili. Hivyo nadhani kabisa hiyo ndio ilikuwa maana yake, yaani mwaka wa tatu.
Hellen yeye amesoma kozi ya Archaeology, na mimi nilisomea kozi ya Political Science and Public Administration. Kwa hiyo, tulikuwa kozi mbili tofauti kabisaa na ndiyo maana tulikuja kufahamiana mwaka wa tatu. Ajabu ni kuwa, kwenye semester ya pili ya mwaka wa Mwisho wa masomo yetu, mimi niliamua kuongezea kozi hii ya human rights, kama kozi ya ziada tu. Haikuwa lazima kuisoma, kumbe naye, aliamua kufanya hivyo tusijue kama ndio kitu kingetukutanisha.
Mimi ni mtu mmoja ambaye, napenda kubeba majukumu yangu kwa mikono miwili, tena kwa umakini wa kiwango cha juu kabisa. Na hii naweza kukudhihirishia kwa mambo ninayoamua kufanya, ni lazima nione yamekamilika, hapo ndio naweza kurelax. Sasa basi, kwenye hiyo kozi, nikajikuta nimepangwa semina moja na Hellen. Halafu tena, tukapewa group assignment (kazi ya kikundi) watu kumi, mimi na yeye tukiwa miongoni mwa wanakikundi.
Shida ikawa moja, wadau wote niliopangwa nao, ama walikuwa wapuuziaji wa mambo au walikuwa na mishe nyingine muhimu kuliko shule. Watu hawa, tulipokubaliana muda wa kukutana kwa ajili ya kujadiliana na kutafuta majibu ya kazi tuliyopewa, hawakuonekana. Nikajikuta peke yangu eneo la tukio. Bahati mbaya sana ilikuwa kwenye kikao hicho ndio tukabidhiane mawasiliano kwa ajili ya kupeana taratibu na yanayojiri mengine.
Kitu nilichokuja kubaini baadaye, ni kwamba wale wanakikundi wenzangu, kila mmoja kwa wakati wake, alikuwa anajidanganya kwamba ni yeye pekee hajahudhuria kwenye majadiliano, na hivyo kujitia moyo kwamba hakuna kitakachoharibika. Lo! Walijidanganya sana. Baada ya hali kuwa hivyo, basi nikalivalia njuga suala hilo mimi mwenyewe. Nikaanza kuandika kazi ile mimi mwenyewe kwa juhudi kubwa. Uzuri ni kwamba, kwa mfumo wa zile semina za chuoni, kwenye uwasilishaji hoja, angeweza kuteuliwa mmoja akatoa wasilisho lote kwa niaba ya kundi lote, huku wale wengine wakisaidiana naye kujibu hoja ambazo zingeibuliwa kwenye mjadala wa pamoja baada ya wasilisho. Ni kusema kuwa, niliamua kuwa jeshi la mtu mmoja.
Hali hii haikuwa ya kwanza kuwahi kutokea, nilikwishakutana na visa vya namna hii mara kadhaa tangu mwaka wa kwanza, sema hii ilitia fora. Awali nilikuwa nakutana na watu wachache au wengi, wakakosekana baadhi. Lakini hii ilikuwa mara ya kwanza wote kukosekana. Sikujali. Kwanza kabisa, mimi najijua, napenda sana kufanya uwasilishaji, hivyo hata kama ingekuwaje, tuseme kwa mfano angelichaguliwa muwasilishaji mwingine, bado ningelijiandaa kama vile mimi ndio muwasilishaji mkuu. Ndiyo. Kila mtu na ulevi wake bwana, na mimi wangu ulikuwa huu wa kupigiwa makofi na kupewa sifa kwa uwasilishaji bora na wahadhiri pamoja na wanachuo wenzangu. So, kusema kweli, nilijiandaa vema kwa nondo za uhakika.
Siku ya uwasilishaji, mimi nilienda kwenye semina kama kawaida kwa muda uliopangwa. Kumbe bwana, wale jamaa zangu, kwa kutaka angalau wapate point mbili za kujitetea nazo ikitokea wametakiwa kutoa hoja, waliwahi nusu saa kabla ili wakutane na wahusika wengine, wadandie points. Hali ikawa ngumu pale wote tisa walipojikuta hakuna hata mmoja aliyehudhuria kwenye majadiliano. Kimbembe kikawakumba. Wakaanza kuhaminika. Wajadiliane, waandike, wawasilishe, na bado kazi hiyo ilihitaji kukusanywa ikiwa imechapwa!. Walihaha si kidogo. Niliwakuta jamaa wameloa jasho wakihangaika.
Ilikuwa dakika tano hivi kabla ya muda wa wasilisho kufanyika. Dah! walikuwa wamejikatia tamaa vibaya sana. Mwanaume nikaingia kwa mbwembwe na kabrasha zangu kwenye backpack yangu, utadhani waziri wa fedha anaenda kusoma bajeti bungeni.
'Oya waungwana, muda wa kuingia kwenye semina huu. Vipi bado mnagaagaa na upwa?' Nikawauliza.
'Hivi si tupo wote wewe?' Aliniuliza jamaa mmoja anaitwa Stanley.
'Yeah man, twendeni tukawasilishe wazee!' niliwaambia.
'Vipi mwanangu uliandaa wasilisho?' akaniuliza tena.
'Haya ndio mambo niliyofuata hapa mlimani. Hebu njoeni hapa wadau, tuwekane sawa kabisa.' nilitamka kwa sauti kubwa yenye mamlaka. Najua kwa wakati huo walikuwa tayari kunisikiliza kwa hamu zote, si nimekuja kuokoa chombo kisiende mrama? Basi wakanisogelea wakiwa watulivu kama vifaranga walionyeshewa. Nikawaangalia nyuso zao zilivyotia huruma. Mwenyewe nikacheka sana kimoyomoyo.
Naikumbuka vema ile siku. Alinipigia simu, nami nikaipokea kwa bashasha na furaha tele. Huyu alikuwa mpenzi wangu, mwanamke aliyenipa raha mara nyingi. Hellen.
'Mambo vipi mpenzi? Uliona email niliyokutumia? Nilikujulisha kuwa narejea nchini, lakini sijapata tena nafasi ya kucheki kama ulijibu. Kuna mambo fulani fulani yalitokeza na kukatisha mawasiliano. I miss you babe!' niliongea kwa sauti ya furaha. Kawaida, mimi hutabasamu kabla hata ya kusikia sauti ya Hellen, yaani ile nikiona kwenye kioo cha simu yangu jina 'Hellen', basi moyo wangu hufukuta kwa fukuto la furaha, hata kama ningekuwa na huzuni, mie huisahau mara moja hadi pale nitakapomaliza mazungumzo. Na ni kweli kuwa jina lake kwenye simu yangu nimelihifadhi hivyo hivyo kavu kavu, "Hellen" isipokuwa tu mbele yake kuna "Hr 301". Kwa wanachuo wanaelewa hili hutokea sana hasa kwa vile mnapopangiwa seminar na kazi za makundi unasevu namba za watu mnaoshiriki hizo kazi pamoja. Na kwa vile chuoni mnakuwa watu wengi, utalazimika kutafuta namna ya kutofautisha majina. Si ajabu ukawa na Hellen kumi kwenye simu yako, na kama hujaweka ubini, ni dhahiri kuwa utahitaji kuwatofautisha kivyovyote vile. Hii ndio hupelekea mtu kuseviwa Vick cheusi, au Vick mzaramo nk. Hellen Ni mpenzi wangu, lakini jina lake sijalisevu kwa zile mbwembwe za 'my love', au 'Honey' au 'laaziz kama ilivyo kawaida ya wapenzi. Unawezajiuliza kwa nini, siyo! Nitakufahamisha hapo baadaye, lakini yeye Hellen anajua kwa nini jina lake nimelisevu kavu likifuatiwa na HR 301.
Sasa basi, naweza kusema, ingawa tupo kwenye mahusiano kwa miezi takribani minne sasa, lakini ukiniona navyotabasamu kumuona Hellen, basi unaweza kukokotoa na kupata jawabu la uongo. Ndiyo, la uongo. Utajua tu kwamba huyu jamaa, ndiyo kwanza kamuona huyu binti na amemzimikia kinoma. Kawaida, pumbazo langu la kwanza nilipokutana na Hellen mara ya kwanza miezi mitano iliyopita, basi limekuwa likibaki hivyo hivyo hata sasa baada ya miezi hii yote kila napomuona. Aisee! Huyu binti kajua kunishika. Mie zuzu wallah!.
Basi, turejee kwenye simu. Baada ya kupigiwa naye na kujitetea kabla hata hajasema kitu, nilisubiri kwa hamu niisikie sauti ya mpenzi wangu, ambayo kuisikia pekee, hunipatia burudani nafsini mwangu.
'Niliiona email Derick, na nimeshaijibu. Uko wapi?' Hellen alizungumza kwa sauti tulivu. Sauti ambayo sikuizoea. Haikuwa na ule uchangamfu wa siku zote. Najua haikuwa nao, japo alijaribu kuongea kwa kuniigizia. Namjua mpenzi wangu bwana huwezi kunidanganya kitu. 'Hellen wangu ana shida gani jamani!'. Nilijiuliza. Ah, sikuvumilia kubaki najiuliza tu, nikaamua kuondoa hilo dukuduku moyoni mwangu.
'Vipi dear, mbona umepoa hivyo mpenzi? Kunani tena darling. Eh mamii, are you sick mpenzi?' nililazimika kuhoji, ile furaha yangu ikiyeyuka kama donge la barafu kwenye joto kali. Aisee, sio siri, niambie habari gani sijui, lakini habari za huzuni hunibeba sana mimi. Nadhani, huu ni udhaifu kwangu mimi mtoto wa kiume, kuwa na hisia nzito sana au tuseme kutekwa kihisia kwa urahisi. Mimi ni mwepesi sana wa furaha na huzuni vile vile. Ndio maana najaribu kusoma soma masuala ya saikolojia, kunisaidia kuwatambua matapeli mapema. Si unafahamu matapeli wanacheza sana na hisia! Naam, matapeli buana wakikujua wewe ni mtu unayepata huzuni ukielezwa tukio la kuhuzunisha, wao ni wepesi sana kupita humo, wakakulisha habari ya msiba, ukajikuta unachangia nauli ya kwenda msibani kwa kuwaonea huruma, kutokana na matatizo chungu nzima watakayokuorodheshea.
Huzuni iliyokuwa moyoni mwangu kusikia tu ukosefu wa uchangamfu kwenye sauti ya Hellen, ungedhani nimepashwa habari za msiba.
'Siku hazilingani mpenzi, hata hivyo kiafya niko poa tu sema nimekumiss. Kama tunaweza kuonana itakuwa poa sana. Nahitaji tuongee!' Hellen alizungumza kwa utulivu ule ule.
'Ok dear, nipo Changanyikeni now. Nije au uje?' nilimtupia swali japo ilikuwa wazi kwamba alinihitaji niende. Kikawaida, akihitaji kuja kwangu, yeye huja baada ya kujibiwa message yake ya neno moja ambayo ni mimi tu naielewa 'Hr301'. Hiki ni kifupisho cha moja ya kozi ambazo zilitukutanisha mimi na Hellen miezi mitatu iliyopita. Usijali. Nitakuelezea. Najua unataka ujue ilikuwa vipi.
Itaendelea.
2
Kwa kawaida vyuoni, kozi huwa zinakuwa na majina ya vifupisho. Mfano hiyo Hr inasimama badala ya kozi inayoitwa 'human rights' (Haki za binadamu …) na hiyo 301, Sina hakika, lakini nahisi inamaanisha mwaka wa masomo. Maana kulikuwa pia hr 101 iliyofundishwa mwaka wa kwanza, hr 201 ilifundishwa mwaka wa pili. Hivyo nadhani kabisa hiyo ndio ilikuwa maana yake, yaani mwaka wa tatu.
Hellen yeye amesoma kozi ya Archaeology, na mimi nilisomea kozi ya Political Science and Public Administration. Kwa hiyo, tulikuwa kozi mbili tofauti kabisaa na ndiyo maana tulikuja kufahamiana mwaka wa tatu. Ajabu ni kuwa, kwenye semester ya pili ya mwaka wa Mwisho wa masomo yetu, mimi niliamua kuongezea kozi hii ya human rights, kama kozi ya ziada tu. Haikuwa lazima kuisoma, kumbe naye, aliamua kufanya hivyo tusijue kama ndio kitu kingetukutanisha.
Mimi ni mtu mmoja ambaye, napenda kubeba majukumu yangu kwa mikono miwili, tena kwa umakini wa kiwango cha juu kabisa. Na hii naweza kukudhihirishia kwa mambo ninayoamua kufanya, ni lazima nione yamekamilika, hapo ndio naweza kurelax. Sasa basi, kwenye hiyo kozi, nikajikuta nimepangwa semina moja na Hellen. Halafu tena, tukapewa group assignment (kazi ya kikundi) watu kumi, mimi na yeye tukiwa miongoni mwa wanakikundi.
Shida ikawa moja, wadau wote niliopangwa nao, ama walikuwa wapuuziaji wa mambo au walikuwa na mishe nyingine muhimu kuliko shule. Watu hawa, tulipokubaliana muda wa kukutana kwa ajili ya kujadiliana na kutafuta majibu ya kazi tuliyopewa, hawakuonekana. Nikajikuta peke yangu eneo la tukio. Bahati mbaya sana ilikuwa kwenye kikao hicho ndio tukabidhiane mawasiliano kwa ajili ya kupeana taratibu na yanayojiri mengine.
Kitu nilichokuja kubaini baadaye, ni kwamba wale wanakikundi wenzangu, kila mmoja kwa wakati wake, alikuwa anajidanganya kwamba ni yeye pekee hajahudhuria kwenye majadiliano, na hivyo kujitia moyo kwamba hakuna kitakachoharibika. Lo! Walijidanganya sana. Baada ya hali kuwa hivyo, basi nikalivalia njuga suala hilo mimi mwenyewe. Nikaanza kuandika kazi ile mimi mwenyewe kwa juhudi kubwa. Uzuri ni kwamba, kwa mfumo wa zile semina za chuoni, kwenye uwasilishaji hoja, angeweza kuteuliwa mmoja akatoa wasilisho lote kwa niaba ya kundi lote, huku wale wengine wakisaidiana naye kujibu hoja ambazo zingeibuliwa kwenye mjadala wa pamoja baada ya wasilisho. Ni kusema kuwa, niliamua kuwa jeshi la mtu mmoja.
Hali hii haikuwa ya kwanza kuwahi kutokea, nilikwishakutana na visa vya namna hii mara kadhaa tangu mwaka wa kwanza, sema hii ilitia fora. Awali nilikuwa nakutana na watu wachache au wengi, wakakosekana baadhi. Lakini hii ilikuwa mara ya kwanza wote kukosekana. Sikujali. Kwanza kabisa, mimi najijua, napenda sana kufanya uwasilishaji, hivyo hata kama ingekuwaje, tuseme kwa mfano angelichaguliwa muwasilishaji mwingine, bado ningelijiandaa kama vile mimi ndio muwasilishaji mkuu. Ndiyo. Kila mtu na ulevi wake bwana, na mimi wangu ulikuwa huu wa kupigiwa makofi na kupewa sifa kwa uwasilishaji bora na wahadhiri pamoja na wanachuo wenzangu. So, kusema kweli, nilijiandaa vema kwa nondo za uhakika.
Siku ya uwasilishaji, mimi nilienda kwenye semina kama kawaida kwa muda uliopangwa. Kumbe bwana, wale jamaa zangu, kwa kutaka angalau wapate point mbili za kujitetea nazo ikitokea wametakiwa kutoa hoja, waliwahi nusu saa kabla ili wakutane na wahusika wengine, wadandie points. Hali ikawa ngumu pale wote tisa walipojikuta hakuna hata mmoja aliyehudhuria kwenye majadiliano. Kimbembe kikawakumba. Wakaanza kuhaminika. Wajadiliane, waandike, wawasilishe, na bado kazi hiyo ilihitaji kukusanywa ikiwa imechapwa!. Walihaha si kidogo. Niliwakuta jamaa wameloa jasho wakihangaika.
Ilikuwa dakika tano hivi kabla ya muda wa wasilisho kufanyika. Dah! walikuwa wamejikatia tamaa vibaya sana. Mwanaume nikaingia kwa mbwembwe na kabrasha zangu kwenye backpack yangu, utadhani waziri wa fedha anaenda kusoma bajeti bungeni.
'Oya waungwana, muda wa kuingia kwenye semina huu. Vipi bado mnagaagaa na upwa?' Nikawauliza.
'Hivi si tupo wote wewe?' Aliniuliza jamaa mmoja anaitwa Stanley.
'Yeah man, twendeni tukawasilishe wazee!' niliwaambia.
'Vipi mwanangu uliandaa wasilisho?' akaniuliza tena.
'Haya ndio mambo niliyofuata hapa mlimani. Hebu njoeni hapa wadau, tuwekane sawa kabisa.' nilitamka kwa sauti kubwa yenye mamlaka. Najua kwa wakati huo walikuwa tayari kunisikiliza kwa hamu zote, si nimekuja kuokoa chombo kisiende mrama? Basi wakanisogelea wakiwa watulivu kama vifaranga walionyeshewa. Nikawaangalia nyuso zao zilivyotia huruma. Mwenyewe nikacheka sana kimoyomoyo.