Socratic
JF-Expert Member
- Dec 18, 2014
- 568
- 308
Unakuta mtu amefariki. Watoto, wanafamilia, ndugu jamaa na marafiki wanalia na kuomboleza. Anatokea mtu anatoa nasaha kuhusu marehemu na mwisho anamalizia kwa kusema "Sisi tulimpenda Lakini Mungu alimpenda zaidi". najua ni kauli inayolenga kuleta faraja lakini tumeshafikiri kwa jicho la tatu kuhusu kauli hii?
Fikiria unamwambia mtoto mdogo ambaye mzazi wake aliyempenda sana amefariki kisha anaambiwa "Mungu alimpenda zaidi (Ndio maana amemchukua), tunajua hii inaleta fikra gani kwa yule mtoto? Na hata kwa watu wazima, ni kweli kuwa Mungu anawachukua wale anaowapenda zaidi? Ni kweli wanaofariki leo wamependwa zaidi na Mungu?
Hii misemo mingine inachanganya sana na pengine kupotosha.
Fikiria unamwambia mtoto mdogo ambaye mzazi wake aliyempenda sana amefariki kisha anaambiwa "Mungu alimpenda zaidi (Ndio maana amemchukua), tunajua hii inaleta fikra gani kwa yule mtoto? Na hata kwa watu wazima, ni kweli kuwa Mungu anawachukua wale anaowapenda zaidi? Ni kweli wanaofariki leo wamependwa zaidi na Mungu?
Hii misemo mingine inachanganya sana na pengine kupotosha.