Haya: Zoezi la Uhakiki Lianze Mapema!

Haya: Zoezi la Uhakiki Lianze Mapema!

Mchokoo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,604
Ni kweli au ni ya kikombe cha babu? Ni hakika, au ni ya waliotelekeza watoto? Ni sawa, au ni ya kututoa kwenye ya msingi?

Kama ni kweli, na ni hakika, na ni sawa. Mimi napendekeza lianze zoezi makini kama lile la kupima samaki kwa lula.

Si kwa wanaotajwa pekee, bali iwe ni kwa kila mtanzania.
Kila mchukia maovu ukiwemo ushoga alazimishwe kuhakikiwa upya. Zoezi lisimamiwe kwa haki na kweli.

Kuanzia kwa wasioheshimika mpaka kwa waheshimiwa sana. Hata hivyo wao ndiyo wenye wajibu wa kuhakikiwa kwanza ili kulichangamsha zoezi zima.

Hima jamani, wote tuhakikiwe kama tuna halali au haramu.

Ikitokea limekubaliwa, wahakikiwa wasubiri vipimo ili waondoke na majibu yao.
Ni ushauri tu.
 
Ila tuache utani kuna watu nawaheshimu sana kama wasipochukua hatua kwa huyu Konki watanihuzunisha sana, lakini najiuliza tena inamaana wakapimwe ili wakitoka huko hospital wakae upandeupande kama rutty!?
 
Itakuwa ngumu,hivi; bwana yule alie tajwa mjengoni, amesha pimwa malinda? Nadhani aanze yee.
 
Back
Top Bottom