Haya yanatuangusha Chadema

haya hatujaanza kuyasema leo lakini viongozi wetu wametia pamba masikiono . Tungekuwa hata na redio ingetosha kuweka kipindi cha kuelimisha wananchi kuhusu sera za chama hata haya tunayolalamika kuwa viongozi wameshindwa kupeleka sera vijijini lisingekuwepo maana wanakijiji wangesikia sera kupitia redio ya chama
Zamani akina j mnyika walikuwa wanapita hapa jf na kujibu baadhi ya hoja siku hizi wameridhika hawajali tena sisi ni sawa na kelele za mlango hazimyimi mwenyenyumba usingizi.
 
thinking very carefully.
SIUNGI MKONO
RADIO NA TV kwa chama chochote nchini.
kwa mazingira ya kidemokrasia NI ISHARA MBAYA SANA.
1.tutakosa balance ya habari.
2.kwa sasa tunataka kuongeza wafuasi,wale ambao ni ccm na vyama vingine tunawahitaji ila hawawezi kabisa kuangalia tv yetu wakiwa tayari wanatuchukia kama chadema wengi tulivyoacha kuangalia taarifa za habari TBC kwa sababu ni chombo kinachoegemea upande mmoja.
3.kikubwa ni kupigania uhuru wa vyombo vya habari ili viwe huru na viwe na balance ya habari,LEO hii MWANANCHI&ITV vimeunganisha watanzania wote na habari zote zinasomwa&kutazamwa na watu wa pande zote na hata mimi nasoma habari za CCM ila habari za ccm UHURU siwezi kusoma.
NIAMBIENI CCM mpaka sasa wamefaidikaje na gazeti LA UHURU,haliuziki hata kama limeandika ukweli,na limekuwa mzigo kwa kuingizia CCM hasara badala ya faida na hata wana ccm wenyewe ni wachache wanaolinunua mana hakuna uhakika wa kukuta habari zote ktk mitazamo yote ya hasi na chanya
4.TUNAHITAJI PIA KUKOSOLEWA
 
Nashukuru kwa mawazo na uzi huu, mie nadhani chama si viongozi ni sisi wenyewe, Nadhani tuweke kwenye mipango yetu ya muda mfupi, mrefu, na muda wa kati. Kwa kweli naanimini viongozi wetu naamininni wasikivu waelewa na wako tayari kwa mageuzi. Mie naamini tuanzishe mfuko rasmi ambao tutachangia wenyewe na kisha tuwaachie majukumuviongozi wetu na wao walichukue wazo hili na kuliweka kwenye mkakati kiasi wanapokutana na marafiki zetu wa ndani na nje ya nchi basi wafikishe maombi ya chama chetu kwa ajili ya kuwafikia wananchi wengi na hasa wa vijijini kuwaeleza sera, mikakati na mipango ya baadaye ya kuwakomboa kutoka kwenye minyonyororo ya Mafisadi. Hata wakati wa Ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika Nyerere alitumia Radio Tanzania wakati huo na ndio msingi wa kuwepo kituo kilichojulikana kama external service of Radio Tanzania DSM.
Nawasilisha,
 
Pamoja na wanachi wengi kukipenda CDM bado wengine tunaona kuna mapungufu ambayo yanaweza kuboreshwa zaidi kabla ya 2015. Mfano msisitizo wa kuwa na mising mingi iwezekanavyo nchi nzima.
Sioni sababu viongozi wa kitaifa kwenye mikutano yao mingi wanakikandia chama tawala tunataka watupe mbinu za kufungua matawi na mising kila mahali na jinsi ya kuelezea sera za chama kwa wananchi. Msisitizo wa vikao ngazi zote hasa wakati wa kipindi hiki cha uchaguzi. Mimi nasema hivyo kwa sababu sisikii yakisisitizwa na viongozi wakuu na huku tuliko tuna shauku lakini hatuna uongozi unaoelekea kutuweka sawa kupambana na chama tawala.

Nina imani kuna namna ya kupenyeza sera za chama kutoka juu hadi chini bila kuptia vikao vya hadhara! Wakati ni sasa.
Big up mleta uzi.
 
Kama hayo yasemwayo kweli, basi yote dugu moja hakuna mkombozi wa kweli

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

Mnyika siku hizi anajibu hoja za Ridhiwani. Hana time na vidampa. Ndio maana hakujibu hoja za elimu yake mpaka alipoulizwa na Ridhiwani.
 

Lengo letu sote ni kuuondoa mfumo mbovu wa utawala kwa hiyo juhudi ziongezwe kila pahala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…