Haya mapenzi ya namna hii ni shida.........

Haya mapenzi ya namna hii ni shida.........

Gwesefe

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
682
Reaction score
382
Nilikuwa na demu tukiishi mkoa fulani bhana, sasa akapata kakazi fulani Dar kumbe alipofika huko akapata mchepuko mwingine na kuanza kuzuga yaani baby nimekumiss mara yaani utanikuta kama ulivyoniacha.

Siku ya siku nikatinga mjini ghafla tukaonana tukapiga story ila akawa mtu wa wasiwasi fulani, simu hapo kaweka silence anasomea sms pembeni nikagundua janja yake.........., katika kumbana akakubali kuwa amekuwa akitembea na mkaka mmoja mwezi wa tatu sasa ila alimueleza ukweli kuwa yupo na mimi, kwa hiyo kumbe hata night nikipiga simu anapokea bila shida maana jamaa anajua anakausha tu.

Mi nikaamua kumpiga chini akamueleza mchepuko wake kuwa nimeachana na jamaa yangu baada ya kugundua na msaliti kwa hiyo nitakuwa na wewe tu peke yako, jamaa na yeye katafakari baada ya wiki moja akamuita akamuambia na mimi tuachane tu maana nilikukuta na mtu wako.

Cha ajabu baada ya huko nako kula cha mbavu eti anarudi kujiombesha msamaha. Jamani suala kama hili linakaaje au na mimi nimfanye mchepuko kwa sasa?
 
Kapimeni kwanza mfahamu afya zenu, baada ya hapo mnaweza kuingia phase II ya love drama.
 
Halmashauri ya kichwa chako inasemaje kuhusu hili?
 
akimpata mwingine atakufanyia yaleyale. Historia hujirudia
 
Mkuu niifowadie mimi huyo demu wako niendeleze kuanzia pale ulipoachia! teh teh teh!
 
kama bado moyo wako wampenda anzen upya tu, ila kupima afya kwanz ni muhimu....
 
Kama unampenda nenden mkapime afya zenu mkiwa poa endelea naye maana unaonekana unampenda bado una room kwa ajili yake that's why umekuja hapa tukusaidie ushauri.
 
Kama unampenda nenden mkapime afya zenu mkiwa poa endelea naye maana unaonekana unampenda bado una room kwa ajili yake that's why umekuja hapa tukusaidie ushauri.

Hofu yangu ni kwamba kama ule mchepuko wake ulimwacha baada ya kuambiwa kuwa njia kuu kashaachia ngazi, wakirudiana tena mchepuko nao c utarudi tena? cos hakuachwa kwa sababu hapendwi bali kwa sababu aliachana na njia kuu yake.
 
Back
Top Bottom