Hawa Binadam wenzetu sijui wana utu au la!!!!

Twin_Kids

JF-Expert Member
Feb 25, 2016
3,684
5,637
Hali zenu wapendwa! Ni tumaini langu mu wazima wa afya.

Baada ya kuona ushauri wenu hapa JF, nimeona vyema nikawashirikishe mambo yanayoniumiza kichwa:

1. Nilimpata mwanamke mmoja tukaamuwa kuwa wapenzi na lengo la kuishi kama mke na mme.

Nilimtolea mahali, akawa ni mjamzito. Alidai kuwa ujauzito ni wangu, jambo ambalo sikupingana nalo na ndo nikaamua kumtolea mahali.

Alikuwa akibadilika mara kwa mara, ikafikia hatua nikaongea na ndugu yake mmoja, ndo nikagundua kumbe tunamsheya wanaume wawili.

Alikuja kukili mwenyewe kwamba ana mwingine, na ameshamwambia mimba ni ya kwake.

Mara alidai mimba yangu niilee, nikafanya hivyo mpaka mtoto ana miaka 3 sasa, ila cha ajabu sasa hivi hata picha ya mtoto nikiomba sipewi mtu anaishia mitini.

Huyu mtoto ni wangu niendelee kuhangaika hivo hivo au niachane nae tu!

Na je, vipi nikiacha na kwa badae naambiwa mwanao! Si ntakuwa nimemuumiza mtoto!

Nikizingatia nilivokua natafuta litoto la kike mwishoe ndo yamekuwa hayo!



2. Baada ya mda hapo kuachana na huyu mwanamke, nilikula tunda sehemu. Ilikuwa tarehe 1-01-2014.

Tarehe 25-09-mwaka huo, niliweza kuwasiliana na huyo mwanamama (hapo kati kati nasikia aliendaga Uganda na kupotezana) akaniambia ni mjamzito.

Nilimuuliza Hivi, mimba hiyo ni ya kwangu? Alijibu: Nadhani. Nilisubiri mtoto atazaliwa, hapo hela natoa, mpaka alikuja kujifungua tarehe 18-01-2015.



Nilichukulia poa tu, ila sasa, mwanamke kawa jeuri, safari za hapa na pale, cha ajabu anadai kabla ya kujifungua alikuwa amelogwa hivyo anaenda kupata dozi; kama kweli au la hayanihusu haya; shida yangu ni hii, hasa kwenu wale mliojaliwa kupata familia au wenye ujuzi na swala hilo; huyu mtoto atakuwa wangu?

Maana kila naeongea nae anadai mtoto hawezi kuishi tumboni mda wote huo!

Mpaka madaktari wa wanawake waliniambia hivo, nae anasisitiza mtoto ni wa kwangu; wakati mwingine ana kiburi sijapata kuona; anadai hata nisipojiskia kumsaidia niache mtoto atakuwa tu.

Naombeni ushauri wenu.
 
Ungependa ushauriwe kuhusu nini haswaa??!
Huo ndo ukweli;
Ushauli naohitaji
1) Kuna haja ya kuendelea kuwaza huyu baby-girl ambaye ana baba wawili? Je nikijitoa mwishowe mtoto akaja kunitambua kama baba ukubwani ntakuwa nimemtendea haki?

2) Huyu mtoto aliyezaliwa kwa muda wa mwaka na siku 18, mbali na kupima DNA, niendelee kulea au washikaji wamekula mi nalamba mikono na kuwalelea?
 
Mwanamke anakaa na mimba muda mrefu kama tembo!! Fanya mpango ukampime DNA,,halafu tafuta mwanamke mwingine anaefaa.
Mkuu, asante kwa ushauli, ila kusema ukweli nilishakoma. Kati ya hao watoto akipatikana mmoja au wote ntashukuru na ntalea, vinginevyo sina hamu na hawa binadamu. Nikishindwa ntanunuwa lakini kuweka akilini halitakaa litokee ndugu yangu. Nimeona mengi acha!
 
Mimba gani miezi 12? Au umekosea kuandika tarehe?

Halafu kama umekuwa mgawa mbegu? Kwani wewe ni Duly Sykes? Alijiita dume la mbegu
 
Huo ndo ukweli;
Ushauli naohitaji
1) Kuna haja ya kuendelea kuwaza huyu baby-girl ambaye ana baba wawili? Je nikijitoa mwishowe mtoto akaja kunitambua kama baba ukubwani ntakuwa nimemtendea haki?

2) Huyu mtoto aliyezaliwa kwa muda wa mwaka na siku 18, mbali na kupima DNA, niendelee kulea au washikaji wamekula mi nalamba mikono na kuwalelea?


1. KWA KUWA WAZAZI WA HAO WATOTO WAMEAMUA KUKUAMBIA WEWE NDIE BABA BASI MSHUKURU MUNGU UWALEE BILA KUJIHOJIHOJI. WATOTO HAWANA HATIA YOYOTE. WALIOKUELEZA KAMA WANAUJUA UKWELI NA KISHA KUKUUZIA KESI BASI HAO WATAIBEBA LAANA HIYO MBELE YA SAFARI.

2. IKIWA HUNA AMANI KABISA NA KUWAHUDUMIA WATOTO KWAKUWA HUNA HAKIKA NI WAKO ILI KUJIWEKA KATIKA UHAKIKA NENDA UKAWAPIME DNA UPATE AMANI.

NB. WAPO WAZAZI HASA WANAUME WALIOLEA NA WANAOLEA WATOTO WASIO WAO LAKINI MAMA WA WATOTO WANAJUA NA SI KWAMBA WAKO NA FURAHA LAA BALI KUNA NYAKATI MWANADAMU HUPITIA HUKOSA MAAMUZI KUTOKANA NA HULKA ZETU HIVO KUMSINGIZIA BABA YEYOTE KUWA MHUSIKA IKIWA ANA HAKIKA HUYO BABA ATAMUHUDUMIA NA KUMJALI MTOTO.
 
Mimba gani miezi 12? Au umekosea kuandika tarehe?

Halafu kama umekuwa mgawa mbegu? Kwani wewe ni Duly Sykes? Alijiita dume la mbegu
Siyo ugawa mbegu kaka! Kwa umri nilio nao sasa hivi (34) ulikuwa mda wangu kutafuta mweza. Bahati mbaya niliingia kusiko
 
mkuuu ww Great thnker tunashukur kwa ku share na sis
ila fanya kila linaliwezeokan kam vle kupim uli uondie was wasi kidha baki watot walio halal ule mwache aende zake hana madhara hyu wala usimfikile sanaa
 
mkuuu ww Great thnker tunashukur kwa ku share na sis
ila fanya kila linaliwezeokan kam vle kupim uli uondie was wasi kidha baki watot walio halal ule mwache aende zake hana madhara hyu wala usimfikile sanaa
Inapain sana ndugu yangu! Mi nilipo si rahisi hata lab ya DNA hatuna sisi, mi niliwahi kuwaza kitu kimoja! Wanawake wanapoenda clinic, si madaktari wanaweza jua mimba ina miezi mingapi? Nilitaka nikaende hospital alikokuwa akienda clinic nikaongee na wahusika, si file lake lipo! Nikiambiwa alizidisha ntakuwa mpole! Ila sasa, safari zake zinanitia wasiwasi, maana hapa kuna mengine sijataja ambayo wakati mwingine yananifanya niwe na mashaka nae
 
1. KWA KUWA WAZAZI WA HAO WATOTO WAMEAMUA KUKUAMBIA WEWE NDIE BABA BASI MSHUKURU MUNGU UWALEE BILA KUJIHOJIHOJI. WATOTO HAWANA HATIA YOYOTE. WALIOKUELEZA KAMA WANAUJUA UKWELI NA KISHA KUKUUZIA KESI BASI HAO WATAIBEBA LAANA HIYO MBELE YA SAFARI.

2. IKIWA HUNA AMANI KABISA NA KUWAHUDUMIA WATOTO KWAKUWA HUNA HAKIKA NI WAKO ILI KUJIWEKA KATIKA UHAKIKA NENDA UKAWAPIME DNA UPATE AMANI.

NB. WAPO WAZAZI HASA WANAUME WALIOLEA NA WANAOLEA WATOTO WASIO WAO LAKINI MAMA WA WATOTO WANAJUA NA SI KWAMBA WAKO NA FURAHA LAA BALI KUNA NYAKATI MWANADAMU HUPITIA HUKOSA MAAMUZI KUTOKANA NA HULKA ZETU HIVO KUMSINGIZIA BABA YEYOTE KUWA MHUSIKA IKIWA ANA HAKIKA HUYO BABA ATAMUHUDUMIA NA KUMJALI MTOTO.
Sorry bro,

Unajua hawa ndo wenye uelewa wa nani baba mtoto na wakati mwingine kwa manufaa yao binafsi wanawanyima haki watoto! Wa kwanza kwa asilimia furani, naweza sema wangu! Isuue ilitokea alipojifungua, nasikia kadi ya hospital aliandikwa baba anayekaa nae mbali na mi, ya pili aliandikwa mimi. Sasa issue ni kwamba sasa hivi hata picha ya mtoto nikiomba sipewi,
 
duuh!! acha nikae kimya tuu, maana nikichangia unaweza kuona kama nakutukana vileee.


HITIMISHO:
ila Unatuaibisha wanaume wenzako, ujinga ufanye wewe lakini aibu nione mimi:confused::confused:
 
duuh!! acha nikae kimya tuu, maana nikichangia unaweza kuona kama nakutukana vileee.


HITIMISHO:
ila Unatuaibisha wanaume wenzako, ujinga ufanye wewe lakini aibu nione mimi:confused::confused:
Ili usiaibike naomba hii post uivalie sunglasses
 
Wewe mwenyewe umefikia wapi? Ndio sisi tushauri maana kwa kweli inaonekana hata tukikushauri unaweza usitukubalie na ukaenda kwa hao hao wadada ukawauliza wanasema hivi eti ni sawa?
 
Huo ndo ukweli;
Ushauli naohitaji
1) Kuna haja ya kuendelea kuwaza huyu baby-girl ambaye ana baba wawili? Je nikijitoa mwishowe mtoto akaja kunitambua kama baba ukubwani ntakuwa nimemtendea haki?

2) Huyu mtoto aliyezaliwa kwa muda wa mwaka na siku 18, mbali na kupima DNA, niendelee kulea au washikaji wamekula mi nalamba mikono na kuwalelea?
Fanya upime DNA kuondoa utata
 
Back
Top Bottom