Hatujui Uhuru wa vyombo vya habari utaruhusiwa lini

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,864
Hatujui kwa mfano uhuru wa vyombo vya habari utaruhusiwa lini au ndo imetoka hivyo, hatujui bunge litarudishwa live au ndo kwa heri, hatujui vyama vya siasa vitaruhusiwa kufanya mikutano yake au ndo vimefutwa, hatujui kama utaribu wa kisheria wa kuwajibisha watumishi utarudishwa au tutafuata huu wa mkulu anaotaka.

Hatujui kama utaratibu wa kuendesha serikali kisheria utarudishwa au kila siku tutasubiri saa 2 taarifa ya habari kujua leo wale wakubwa wawili wametoa amri gani. Hatujui kama tutanunua sukari kama ilivyokuwa kwa kumtuma mtoto kwa Mangi au tutaendelea kupanga mstari kwenye maroli.

Hatujui utaratibu wa wizara kujipangia matumizi kama utarudi au tutafuata huu wa mkulu kuamka asubuhi akasema hizi nazipeleka huku?
Mfumo huu wa kuchanganyikiwa utaisha lini?
 
Binadamu mwenzako anataka wewe uishi kama shetani hivi.

Yaani hiyo ni sawasawa na yule Jirani yako mchawi.

Kama ingelikuwa amri yake, angewatoa watu roho kabisa.
 
Binadamu mwenzako anataka wewe uishi kama shetani hivi.

Yaani hiyo ni sawasawa na yule Jirani yako mchawi.

Kama ingelikuwa amri yake, angewatoa watu roho kabisa.
Neno la msingi sana hili........ Only six thinking hats model can describe.
 
Binadamu mwenzako anataka wewe uishi kama shetani hivi.

Yaani hiyo ni sawasawa na yule Jirani yako mchawi.

Kama ingelikuwa amri yake, angewatoa watu roho kabisa.


Kwa kuonyesha msisitizo kawaambia polisi waanze wizi wa vipuri vya gari, ili ukitoka gharama ikiwa kubwa kuikarabati ukaiuze scraper utembee kwa miguu kama shetani
 
Kwa kuonyesha msisitizo kawaambia polisi waanze wizi wa vipuri vya gari, ili ukitoka gharama ikiwa kubwa kuikarabati ukaiuze scraper utembee kwa miguu kama shetani
Mkuu acha tu

Yaani nilidhani angeliagiza jeshi la polisi kuhakikisha wanawafikisha mahakamani hao watuumiwa/washtakiwa ili sheria ichukuwe mkondo wake.

Nchi inapoendeshwa bila utawala wa sheria ni matatizo matupu.

Halafu unaweza kutamani mwanadamu mwenzako apate matatizo/shida au adhurike kwa namna yoyote ile? Huo si ndio uchawi wenyewe kabisa?
 
Back
Top Bottom