Hatimaye sasa sanaa ni ajira

Hatimaye sasa sanaa ni ajira

ItsMi

Member
Joined
Sep 13, 2021
Posts
66
Reaction score
31
Vijana hii ni fursa nyingine tena. Kwa kuwa Kipindi kirefu kilichopita wasnii waliokuwa wakifanya sanaa zao na kuziuza au pengine kuuziwa na madalali huku wakiambulia patupu pasipo kuipata haki yao ya msingi lakini hivi sasa taasisi inayohangaikia hakimiliki za wasanii (cosota) pamoja na basata ikiungwa mkono na sekta zingine za kiserikali wameweza kuanzisha mpango mkakati wa kuwalipa mirahaba wasanii wanaofanya kazi za sanaa nchini.

Hivi sasa wamekua vitani bega kwa bega na wasanii kuhakikisha haki za wasanii hao zinapatikana kwa kuwalipa kinachowastahili Ikiwa kama faida wanayoipata mara baada ya kazi zao kutumika na baadhi ya Vyombo vya habari na burudani lengo kubwa likiwa ni kumshika mkono msanii kumnufaisha na kile ambacho ni jasho lake ambalo hapo mwanzo lilimwagika pasina kumpatia manufaa aliyostahili zaidi ya hapo.

Hivyo nitoe pongezi kwa Cosota na basataa pamoja na serikali kwa ujumla wake ambao ndio wamekua wakilihangaikia swala hili kwa kulipa kipaombele swala hili na hatimae limefanikiwa na tayari wasanii wanaanza kunufaika.
Hivyo kwa wale wazazi waliodhani sanaa hailipi na kuwakataza vijana wao kujihusisha na sanaa niseme tu kwamba sasa ni wakati wa mabadiliko yaliyosubiriwa kwa miaka mingi kwenye nyanja ya sanaa na utamaduni.

Ni ombi langu kwamba waruhusu vijana wao pale inapobidi waweze kufanya vile vikubwa vilivyo ndani ya uwezo wao kwa kuwa ni vipaji mungu amewapa tuzidi kuwashika mikono na kamwe tusiwakatishe tamaa.
Asanteni
 
Ponografia NI Sanaa pia, mbona yule Amba Nini mnamsimanga na kumpa mikiki mizito yeye na mumewe?
Hapana ponografia haiwezi kuwa sanaa kwa kuwa haihusishi usanifu wowote ila Unajua huwa tumetofautiana kuna watu wanamalezi mabaya wengine mazuri hivyo wapo wanopamba mambo machafu kwa kuwa walipata malezi mabaya na hata wale wanaokuwa wakilaani vitendo vibaya hawa nao wako upande mwingine wa malezi bora... Hivyo ponographia ni athari ya kupenda ngono aipatayo mtu kulingana na mazingira atokako... Pia sanaa ni kazi ya ubunifu ambayo hutumia akili nyingi ili kukamilika kwake

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom