Hatari ya kushindwa kuihangaisha akili yako ikusaidie kuujua ukweli

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
21,544
31,461
HATARI YA KUSHINDWA KUIHANGAISHA AKILI YAKO IKUSAIDIE KUUJUA UKWELI

WALE WANAOLALAMIKA WAMEONEWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA WAMEZINGATIA HAYA?

1 . Kama majina yake yatatofautiana kati ya majina aliyojaza kwenye fomu na majina aliyojiandikisha kwenye daftari. Angalia kanuni ya 13 (e) Uk. 152

2. Endapo mdhamini hataandika majina matatu na cheo katika vyama. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (d) Uk. 10-11

3. Jina alilojaza wakati anachukua fomu lifanane na lililopo kwenye fomu ( dispatch book vs forms). Angalia kanuni ya 17 (1) Uk. 153

4. Mgombea arejeshe fomu mwenyewe na kusaini. Angalia kanuni ya 17 (2) Uk. 153

5. Majina ya mdhaminiwa yafanane na ya mgombea yaliyojazwa kwenye fomu. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (a-d) Uk. 10-11

6. Fomu ya kiapo iwe halisi iliyotolewa na msimamizi msaidizi na ishuhudiwe na msimamizi msaidizi ngaz husuka. Angalia kanuni ya 16 (e) Uk. 152

7. Fomu zijazwe na mhusika lazima ziwe zimesainiwa. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (e&f) Uk. 10-11

8. Fomu zishuhudiwe na ngazi ya chini ya chama itakayobainishwa na chama. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.1 & 14.2 (a) Uk. 10-11

9. Ambaye hajajiandikisha hana sifa ya kuwa mgombea. Angalia kanuni ya 13 (e)Uk. 152, ilinganishe na Kanuni ya 16 (d) Uk. 152 na Kanuni ya 14 (a) Uk. 152

10. Aliyejiandikisha mara mbili atakuwa amepoteza sifa ya kugombea au kupiga kura. Angalia kanuni ya 14 (b)Uk. 152

11. Lazima aeleze shughuli halali inayomwingizia kipato na endapo atabainika kudanganya atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 15 (d)Uk. 152

12. Atakayeomba nafasi zaidi ya moja kwenye fomu moja atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 17 (1) & (5) Uk. 152-153

13. Nafasi anayoomba ionekane mpaka kwenye fomu ya kiapo. Angalia kanuni ya 17 (1)Uk. 153 isome sambamba na Kanuni ya 16 (e) Uk. 153

14. Fomu zijazwe kwa ukamilifu. Angalia kanuni ya 17 (2) Uk. 153

15. Eneo la uraia ajaze uraia siyo nchi mfano: Mtanzania na siyo Tanzania. Angalia kanuni ya 17 (1-5) Uk. 153-154

16. Usahihi wa maeneo kwa mujibu wa GN mfano chankobe akiandika chakobe atakuwa amepoteza sifa maana eneo hilo litakuwa halipo ktk GN. Angalia kanuni ya 15 (e) Uk. 152 & Kanuni ya 17 (1-5) Uk. 153-154.

17. Mwombaji aeleze anaomba nafasi ipi na wapi mfano nafasi anayoomba mwenyekiti wa Kijiji cha Kagera vinginevyo atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 15 (e) Uk. 152

18. Fomu ijazwe taarifa inayohitajika tu, kuwepo kwa maandishi au michoro isiyohitajika hilo ni kosa. Angalia kanuni ya 17 (5) Uk. 154

19. Mgombea arejeshe fomu zote mbili kinyume na hapo hana sifa. Angalia kanuni ya 17 (2), (3) na (4) Uk. 153-154

20. Kama mgombea ameomba nafasi mbili unaweza kumteua nafasi moja. Angalia kanuni ya 17 (1)& (5) Uk. 153-154

21. Mgombea akiwa na ajira, wadhifa au uteuzi wowote katika mihimili ya Serikali atakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Anagalia kanuni ya 16 (f)Uk. 153

22. Ikiwa Mgombea alichukua fomu na hakurejesha atakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Angalia Kanuni ya 17 (2), (3) na (4)

23. Mgombea ambaye hatadhaminiwa na ngazi ya chini ya Chama chakeatakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Angalia mwongozo wa uchaguzi sehemu 14.1 na 14.2 (a)

Kabla ya kulalamika kukatwa majina, jiridhisheni kwa kila hatua kama mmekidhi vigezo na masharti sio kulalama....☝🏾🙏🏾
Source: JAMII FORUM

JIBU: SASA AKILI INAPOZINGATIA...

"Law of probability," inakataa kuwa katika makundi mawili mathalan yanajaza form zilizo sawa na wajazaji wa makundi hayo mawili wanafanana kwa kila hali katika sifa zao pakawa makosa yawe yanafanywa na kundi moja tu.

Hili kisayansi haliwezekani kabisa kwa asili 100.

Lakini tujaalie kuwa hili limewezekana ingawa sijui "control" gani itumike.

Tatizo litakuwa limehamia kwenye "Law of Probability," itabidi sheria hii yenyewe iangaliwe upya ili paweze kupatika maelezo na huu si utafiti mdogo.

Mtume SAW katufunza dua anasema "Allah nijaalie nilione jambo kwa dhahiri yake."

Tukithiri kuomba sana dua hii mengi yatakuwa hadhir kwetu.

Kwa ajili hii basi ya hayo niliyoeleza hapo juu hivyo vifungu vya sheria havina maana yeyote ikiwa utatumia, "Law of Probability," nikikusudia sayansi namba kutegua tatizo hili.

Kwa nini basi hayo yametokea?

Jibu ni kuwa kutakuwa na, "intervening cause."

Sasa hapa mwanasayansi uwanja ushafunguka atakapofikia kujua hili katika utafiti wake kitakachofuatia ni kutafuta sababu ya matokeo haya ya makundi mawili yaliyo na sifa sawa lakini moja lijitokeze na kuonekana hodari na hili lingine liwe "mbumbumbu," limesheheni watu wajinga hawawezi hata kujaza taarifa nyepesi za majina na anuani za nyumba zao wenyewe wanazoishi miaka na miaka.

Hawa "mbumbumbu," kwa miaka mingi wamekuwa viongozi katika jamii wakiwaongoza watu.

Hapa yanahitajika maelezo:

These concepts have been given an axiomatic mathematical formalization in probability theory, which is used widely in such areas of study as mathematics, statistics, finance, gambling, science (in particular physics), artificial intelligence/machine learning, computer science, game theory, and philosophy to, for example, draw inferences about the expected frequency of events. Probability theory is also used to describe the underlying mechanics and regularities of complex systems.[4]
 
Hili andiko limejitosheleza kabisa na wala halihitaji ubishi, Watanzania tujifunze kuwa na vichwa huru vinavyojikita kwenye fact ili kuondoa ubishani usio na maana..

Asante Sheikh Mohamedi Said kwa andiko hili...
 
Nategemea kuona majadiliano huru kupitia andiko hili la Sheikh wetu... Andiko hili liko huru na linahitaji akili huru kujadiliwa..

Binafsi kwangu haingii akilini wagombea zaidi ya 2000 kutoka vyama vingine waweze kujaza form vyema huku zaidi ya idadi hiyohiyo wa CCM waweze kujaza form tena wagombea wote ni watanzania kutoka Tanzania..
 
CHADEMA na ACT mtihani wa kujaza fomu umewashinda, sijui ni elimu ndogo au ujuaji mwingi, inafaa warudi shule

Sidhani kama hizo form zina cha ziada kiasi kwamba wengine washindwe kujaza na wa CCM waweze... Hapa tunahitaji basic sense kuelewa kitu..
 
HATARI YA KUSHINDWA KUIHANGAISHA AKILI YAKO IKUSAIDIE KUUJUA UKWELI

WALE WANAOLALAMIKA WAMEONEWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA WAMEZINGATIA HAYA?

1 . Kama majina yake yatatofautiana kati ya majina aliyojaza kwenye fomu na majina aliyojiandikisha kwenye daftari. Angalia kanuni ya 13 (e) Uk. 152

2. Endapo mdhamini hataandika majina matatu na cheo katika vyama. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (d) Uk. 10-11

3. Jina alilojaza wakati anachukua fomu lifanane na lililopo kwenye fomu ( dispatch book vs forms). Angalia kanuni ya 17 (1) Uk. 153

4. Mgombea arejeshe fomu mwenyewe na kusaini. Angalia kanuni ya 17 (2) Uk. 153

5. Majina ya mdhaminiwa yafanane na ya mgombea yaliyojazwa kwenye fomu. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (a-d) Uk. 10-11

6. Fomu ya kiapo iwe halisi iliyotolewa na msimamizi msaidizi na ishuhudiwe na msimamizi msaidizi ngaz husuka. Angalia kanuni ya 16 (e) Uk. 152

7. Fomu zijazwe na mhusika lazima ziwe zimesainiwa. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (e&f) Uk. 10-11

8. Fomu zishuhudiwe na ngazi ya chini ya chama itakayobainishwa na chama. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.1 & 14.2 (a) Uk. 10-11

9. Ambaye hajajiandikisha hana sifa ya kuwa mgombea. Angalia kanuni ya 13 (e)Uk. 152, ilinganishe na Kanuni ya 16 (d) Uk. 152 na Kanuni ya 14 (a) Uk. 152

10. Aliyejiandikisha mara mbili atakuwa amepoteza sifa ya kugombea au kupiga kura. Angalia kanuni ya 14 (b)Uk. 152

11. Lazima aeleze shughuli halali inayomwingizia kipato na endapo atabainika kudanganya atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 15 (d)Uk. 152

12. Atakayeomba nafasi zaidi ya moja kwenye fomu moja atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 17 (1) & (5) Uk. 152-153

13. Nafasi anayoomba ionekane mpaka kwenye fomu ya kiapo. Angalia kanuni ya 17 (1)Uk. 153 isome sambamba na Kanuni ya 16 (e) Uk. 153

14. Fomu zijazwe kwa ukamilifu. Angalia kanuni ya 17 (2) Uk. 153

15. Eneo la uraia ajaze uraia siyo nchi mfano: Mtanzania na siyo Tanzania. Angalia kanuni ya 17 (1-5) Uk. 153-154

16. Usahihi wa maeneo kwa mujibu wa GN mfano chankobe akiandika chakobe atakuwa amepoteza sifa maana eneo hilo litakuwa halipo ktk GN. Angalia kanuni ya 15 (e) Uk. 152 & Kanuni ya 17 (1-5) Uk. 153-154.

17. Mwombaji aeleze anaomba nafasi ipi na wapi mfano nafasi anayoomba mwenyekiti wa Kijiji cha Kagera vinginevyo atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 15 (e) Uk. 152

18. Fomu ijazwe taarifa inayohitajika tu, kuwepo kwa maandishi au michoro isiyohitajika hilo ni kosa. Angalia kanuni ya 17 (5) Uk. 154

19. Mgombea arejeshe fomu zote mbili kinyume na hapo hana sifa. Angalia kanuni ya 17 (2), (3) na (4) Uk. 153-154

20. Kama mgombea ameomba nafasi mbili unaweza kumteua nafasi moja. Angalia kanuni ya 17 (1)& (5) Uk. 153-154

21. Mgombea akiwa na ajira, wadhifa au uteuzi wowote katika mihimili ya Serikali atakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Anagalia kanuni ya 16 (f)Uk. 153

22. Ikiwa Mgombea alichukua fomu na hakurejesha atakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Angalia Kanuni ya 17 (2), (3) na (4)

23. Mgombea ambaye hatadhaminiwa na ngazi ya chini ya Chama chakeatakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Angalia mwongozo wa uchaguzi sehemu 14.1 na 14.2 (a)

Kabla ya kulalamika kukatwa majina, jiridhisheni kwa kila hatua kama mmekidhi vigezo na masharti sio kulalama....☝🏾🙏🏾
Source: JAMII FORUM

JIBU: SASA AKILI INAPOZINGATIA...

"Law of probability," inakataa kuwa katika makundi mawili mathalan yanajaza form zilizo sawa na wajazaji wa makundi hayo wawili wanafanana kwa kila hali katika sifa zao pakawa makosa yawe yanafanywa na kundi moja tu.

Hili kisayansi haliwezekani kabisa kwa asili 100.

Lakini tujaalie kuwa hili limewezekana ingawa sijui "control" gani itumike.

Tatizo litakuwa limehamia kwenye "Law of Probability," itabidi sheria hii yenyewe iangaliwe upya ili paweze kupatika maelezo na huu si utafiti mdogo.

Mtume SAW katufunza dua anasema "Allah nijaalie nilione jambo kwa dhahiri yake."

Tukithiri kuomba sana dua hii mengi yatakuwa hadhir kwetu.

Kwa ajili hii basi ya hayo niliyoeleza hapo juu hivyo vifungu vya sheria havina maana yeyote ikiwa utatumia, "Law of Probability," nikikusudia sayansi namba kutegua tatizo hili.

Kwa nini basi hayo yametokea?

Jibu ni kuwa kutakuwa na, "intervening cause."

Sasa hapa mwanasayansi uwanja ushafunguka atakapofikia kujua hili katika utafiti wake kitakachofuatia ni kutafuta sababu ya matokeo haya ya makundi mawili yaliyo na sifa sawa lakini moja lijitokeze na kuonekana hodari na hili lingine liwe "mbumbumbu," limesheheni watu wajinga hawawezi hata kujaza taarifa nyepesi za majina na anuani za nyumba zao wenyewe wanazoishi miaka na miaka.

Hawa "mbumbumbu," kwa miaka mingi wamekuwa viongozi katika jamii wakiwaongoza watu.

Hapa yanahitajika maelezo:

These concepts have been given an axiomatic mathematical formalization in probability theory, which is used widely in such areas of study as mathematics, statistics, finance, gambling, science (in particular physics), artificial intelligence/machine learning, computer science, game theory, and philosophy to, for example, draw inferences about the expected frequency of events. Probability theory is also used to describe the underlying mechanics and regularities of complex systems.[4]
Viongozi wengi wa vyama vya upinzani wamejaa mihemuko na hawana umakini wowote! Ukweli mchungu ni kuwa bila semina elekezi watanzania walio wengi bila kujali Chama hawawezi kujaza fomu hizo bila maelekezo!
Sababu kubwa ni elimu duni ya Watanzania na mizaha katika mambo muhimu!
CCM wanao utaratibu wa kufanya semina kwa mambo muhimu kama haya.Vyama vya Upinzani hususani CHADEMA wao wamekalia siasa za mitandaoni na kukurupuka! Siasa za kudai mikutano ya hadhara na maandamano!
 
Nategemea kuona majadiliano huru kupitia andiko hili la Sheikh wetu... Andiko hili liko huru na linahitaji akili huru kujadiliwa..

Binafsi kwangu haingii akilini wagombea zaidi ya 2000 kutoka vyama vingine waweze kujaza form vyema huku zaidi ya idadi hiyohiyo wa CCM waweze kujaza form tena wagombea wote ni watanzania kutoka Tanzania..
CCM iliwekeza katika mchakato wa kuwapata wagombea kiasi kuna maeneo uchaguzi ulirudiwa. Isitoshe wateuliwa wa CCM walipewa msaada wa wanasheria kujaza hizo fomu.
 
Yaani wagombea wa CCM wooote wamepatia kujaza fomu na wakati huohuo wagombea wa upinzani wote wamekosea kujaza fomu! Ajabu nyingine ni kuwa hata wale wagombea wa upinzani waliofanikiwa kujaza fomu kwa usahihi, nao wamewekewa mapingamizi!

Halafu kinachoshangaza ni kuwa hawa wasimamizi wa uchaguzi ni kuwa kazi yao ilikuwa ni kutazama namna ya kuengua wagombea wa upinzani badala ya kusaidia warekebishe makosa ili demokrasia itamalaki na kuwapatia wananchi haki ya kuchagua.

Vv
 
Nasubiria matusi na kejeri kutoka ufipana any way rais kikwete aliwahi kusema chadema wanakiwanda cha uongo

State agent
 
Umeanza kuziishi propaganda za kitoto. Nyerere alituasa ukienda kuchota maji, yaliyo kwenye ndoo huwa ni sawa tu na yaliyobaki mtoni, ziwani
Viongozi wengi wa vyama vya upinzani wamejaa mihemuko na hawana umakini wowote! Ukweli mchungu ni kuwa bila semina elekezi watanzania walio wengi bila kujali Chama hawawezi kujaza fomu hizo bila maelekezo!
Sababu kubwa ni elimu duni ya Watanzania na mizaha katika mambo muhimu!
CCM wanao utaratibu wa kufanya semina kwa mambo muhimu kama haya.Vyama vya Upinzani hususani CHADEMA wao wamekalia siasa za mitandaoni na kukurupuka! Siasa za kudai mikutano ya hadhara na maandamano!
 
Back
Top Bottom