Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,544
- 31,461
HATARI YA KUSHINDWA KUIHANGAISHA AKILI YAKO IKUSAIDIE KUUJUA UKWELI
WALE WANAOLALAMIKA WAMEONEWA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA WAMEZINGATIA HAYA?
1 . Kama majina yake yatatofautiana kati ya majina aliyojaza kwenye fomu na majina aliyojiandikisha kwenye daftari. Angalia kanuni ya 13 (e) Uk. 152
2. Endapo mdhamini hataandika majina matatu na cheo katika vyama. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (d) Uk. 10-11
3. Jina alilojaza wakati anachukua fomu lifanane na lililopo kwenye fomu ( dispatch book vs forms). Angalia kanuni ya 17 (1) Uk. 153
4. Mgombea arejeshe fomu mwenyewe na kusaini. Angalia kanuni ya 17 (2) Uk. 153
5. Majina ya mdhaminiwa yafanane na ya mgombea yaliyojazwa kwenye fomu. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (a-d) Uk. 10-11
6. Fomu ya kiapo iwe halisi iliyotolewa na msimamizi msaidizi na ishuhudiwe na msimamizi msaidizi ngaz husuka. Angalia kanuni ya 16 (e) Uk. 152
7. Fomu zijazwe na mhusika lazima ziwe zimesainiwa. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.2 (e&f) Uk. 10-11
8. Fomu zishuhudiwe na ngazi ya chini ya chama itakayobainishwa na chama. Angalia mwongozo wa uchaguzi kipengele cha 14.1 & 14.2 (a) Uk. 10-11
9. Ambaye hajajiandikisha hana sifa ya kuwa mgombea. Angalia kanuni ya 13 (e)Uk. 152, ilinganishe na Kanuni ya 16 (d) Uk. 152 na Kanuni ya 14 (a) Uk. 152
10. Aliyejiandikisha mara mbili atakuwa amepoteza sifa ya kugombea au kupiga kura. Angalia kanuni ya 14 (b)Uk. 152
11. Lazima aeleze shughuli halali inayomwingizia kipato na endapo atabainika kudanganya atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 15 (d)Uk. 152
12. Atakayeomba nafasi zaidi ya moja kwenye fomu moja atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 17 (1) & (5) Uk. 152-153
13. Nafasi anayoomba ionekane mpaka kwenye fomu ya kiapo. Angalia kanuni ya 17 (1)Uk. 153 isome sambamba na Kanuni ya 16 (e) Uk. 153
14. Fomu zijazwe kwa ukamilifu. Angalia kanuni ya 17 (2) Uk. 153
15. Eneo la uraia ajaze uraia siyo nchi mfano: Mtanzania na siyo Tanzania. Angalia kanuni ya 17 (1-5) Uk. 153-154
16. Usahihi wa maeneo kwa mujibu wa GN mfano chankobe akiandika chakobe atakuwa amepoteza sifa maana eneo hilo litakuwa halipo ktk GN. Angalia kanuni ya 15 (e) Uk. 152 & Kanuni ya 17 (1-5) Uk. 153-154.
17. Mwombaji aeleze anaomba nafasi ipi na wapi mfano nafasi anayoomba mwenyekiti wa Kijiji cha Kagera vinginevyo atakuwa amepoteza sifa. Angalia kanuni ya 15 (e) Uk. 152
18. Fomu ijazwe taarifa inayohitajika tu, kuwepo kwa maandishi au michoro isiyohitajika hilo ni kosa. Angalia kanuni ya 17 (5) Uk. 154
19. Mgombea arejeshe fomu zote mbili kinyume na hapo hana sifa. Angalia kanuni ya 17 (2), (3) na (4) Uk. 153-154
20. Kama mgombea ameomba nafasi mbili unaweza kumteua nafasi moja. Angalia kanuni ya 17 (1)& (5) Uk. 153-154
21. Mgombea akiwa na ajira, wadhifa au uteuzi wowote katika mihimili ya Serikali atakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Anagalia kanuni ya 16 (f)Uk. 153
22. Ikiwa Mgombea alichukua fomu na hakurejesha atakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Angalia Kanuni ya 17 (2), (3) na (4)
23. Mgombea ambaye hatadhaminiwa na ngazi ya chini ya Chama chakeatakuwa amepoteza sifa za kuchaguliwa. Angalia mwongozo wa uchaguzi sehemu 14.1 na 14.2 (a)
Kabla ya kulalamika kukatwa majina, jiridhisheni kwa kila hatua kama mmekidhi vigezo na masharti sio kulalama....☝🏾🙏🏾
Source: JAMII FORUM
JIBU: SASA AKILI INAPOZINGATIA...
"Law of probability," inakataa kuwa katika makundi mawili mathalan yanajaza form zilizo sawa na wajazaji wa makundi hayo mawili wanafanana kwa kila hali katika sifa zao pakawa makosa yawe yanafanywa na kundi moja tu.
Hili kisayansi haliwezekani kabisa kwa asili 100.
Lakini tujaalie kuwa hili limewezekana ingawa sijui "control" gani itumike.
Tatizo litakuwa limehamia kwenye "Law of Probability," itabidi sheria hii yenyewe iangaliwe upya ili paweze kupatika maelezo na huu si utafiti mdogo.
Mtume SAW katufunza dua anasema "Allah nijaalie nilione jambo kwa dhahiri yake."
Tukithiri kuomba sana dua hii mengi yatakuwa hadhir kwetu.
Kwa ajili hii basi ya hayo niliyoeleza hapo juu hivyo vifungu vya sheria havina maana yeyote ikiwa utatumia, "Law of Probability," nikikusudia sayansi namba kutegua tatizo hili.
Kwa nini basi hayo yametokea?
Jibu ni kuwa kutakuwa na, "intervening cause."
Sasa hapa mwanasayansi uwanja ushafunguka atakapofikia kujua hili katika utafiti wake kitakachofuatia ni kutafuta sababu ya matokeo haya ya makundi mawili yaliyo na sifa sawa lakini moja lijitokeze na kuonekana hodari na hili lingine liwe "mbumbumbu," limesheheni watu wajinga hawawezi hata kujaza taarifa nyepesi za majina na anuani za nyumba zao wenyewe wanazoishi miaka na miaka.
Hawa "mbumbumbu," kwa miaka mingi wamekuwa viongozi katika jamii wakiwaongoza watu.
Hapa yanahitajika maelezo:
These concepts have been given an axiomatic mathematical formalization in probability theory, which is used widely in such areas of study as mathematics, statistics, finance, gambling, science (in particular physics), artificial intelligence/machine learning, computer science, game theory, and philosophy to, for example, draw inferences about the expected frequency of events. Probability theory is also used to describe the underlying mechanics and regularities of complex systems.[4]