MUNGU amlaze marehem mahali pema peponi inahuzunisha sana jaman! polen sana! Naomba kuwaleteeni hiki kisa cha kusikitisha; ilikuwa mwaka jana jamaa yangu na rafiki yangu tulisoma naye o'level huko mara katika harakati za maisha alikuja dsm sasa huo mwaka jana alikuwa na biashara ya butcher na kijana mmoja katika kukosa uaminifu wakadhurumiana na mdhumiwa akiwa rafiku yangu anaitwa frenk warioba. Sasa mkakati ukaundwa na huyo mshirika wake akaitwa na rafiki yake maeneo ya ving'ung'uti kuwa akamlipe pesa yake aliondoka tabata akamuaga mke wak
Da pole sana kaka mi ilinitokea Sinza siku moja kwenye lodge moja hivi. Nilikuwa na Shem wenu ndani ya chumba tukagombana coz ma gal alikuwa anawivu sana.
Baada ya kugombana nikabidi mi nisepe zangu nikaona hamna dalili ya kupata mzigo hapa but kipindi naondoka Shem wenu alikuwa yupo anaoga.. Mi nipo njiani nakaribia pale meeda nikaona kundi kubwa la watu km 10 hivi wananifata na kuita mwizi mwizi mi nikashangaa vp. Ghafla namuona mlinzi wa lodge anasema kuna demu mmoja Anasema umemwibia pochi yenye laki 2..watu baada ya kusikia hivyo wakaanza kunipiga mdogo mdogo kwamba lazima tukuchome wewe, watu wakawa wanaongezeka na kipondo kinaongezeka yani sipati hata muda wa kujitetea.
Mara gafla akatokea jamaa mmoja tulipiga naye mzumbe chuo amani Mimi mtu huyu namjua twendeni turudi lodge Kwa huyo binti aliyeibiwa, basi tukarudi watu kama 20 ivi hapo nishapigwa sana jamani.. Tukafika guest house pale, Dada wa reception akasema yule msichana kaondoka sasa hivi kafatwa na mwanaume akiwa na gari..kuhusu pochi kumbe kaiona ilikuwa chini ya mto. Sitoisahau that day
Habari wakuu...
Jana mwanajamii mwenzenu ilibaki kidogo tu ni rest in peace kutoka kwa wananchi wenye hasira Kali. Ilikuwa kwenye daladala...kama mnavyojua wana JF usafiri wa umma tabu zake hasa nyakati za asubuhi.
Basi baada ya daladala kuingia kituoni watu tukaanza kugombania..hatimaye nikafanikiwa kuingia..lakini sikufanikiwa kupata siti....nilisimama na mdada Fulani hivi pembeni yangu huku akiwa amening'iniza mkoba wake upande Wangu..wakati tunaendelea na safari na hizi barabara zetu zilizo kwenye marekebisho. Ule mkoba ukawa unaning'inia kuniegemea mimi.
Sasa kuna mtu alikuwa anashuka kituo kinachofuata ikanilazimu kusogea mbele kidogo ili kumpisha mshukaji..kwa bahati mbaya wakati nampisha Yule mshukaji mabega yetu yakawa kama yanauvuta ule mkoba wa yule dada.
Kasheshe likaanzia hapo baada kunihisi mimi ndiye niliyekuwa nauvuta ule mkoba kwa makusudio ya kuiba..akaanza kunipigia makelele ya wizi. Jambo ambalo liliwapa hamaki abiria wengine wakaanza kunishambulia hadi konda alipoanza kunitetea kwa kuwa alilishuhudia. Na ukijumlisha na personality ...abiria wakaanza kunielewa kwamba sikuwa mwizi.
Ikanibidi nishukie kituo kinachofuata ili kuondoa nuksi...duh..kweli si kila anayekufa kwa wizi basi kaiba kweli..wengine wanasingiziwa tu...tuweni tunaposhambulia wezi....
Kuna kitu kinakutafuta mwombe Mola wako akusitiri
Am really sorry for the Man, bcoz he has got embarrased with his wife but at the other point, amejua ukweli pia.
POLE SANASi mjui aliyefanya kitendo hicho ila kuna rafiki yangu aliyekuwa karibu sana na jamaa huyo. Ila wakati wa mkasa unatokea yeye alikuwa bagamoyo kikazi. Mimi nilisimuliwa mwaka huu mwezi wa nne kuwa frenk alisha kufa kwa kupakaziwa wizi. Ila aliniambia aliyefanya hivyi sasa hivi amekuwa kama chizi hivi aluchanganyikiwa ivi. Kaka inauma sana.
Haya mambo yapo
(Kuna jamaa mmoja yangu Ismail Kyarumbika R.I.P.alifanyiwa hivyo huko Mombasa alipoenda kumdai kinguvu mdaiwa wake)
POLE SANA
ila Marehemu alitakiwa awaambie wale wanaompiga kuwa mbaya wake ni fulani na ANAMDAI HELA YA MAUZO YA NYAMA
naona Wasamaria wema wangemuelewa.
Lakini mara zote Marehemu huwa ana makosa
Ni wiki sasa imepita kuna kijana wa miaka 17 kauawa huku kimara mwisho njia ya bonyokwa millenium. Huyu kijana alijiingiza kwenye ufundi wa bodaboda baada ya wazazi wake kushindwa kumlipia ada. Siku ya idd tar 29/7/2014 marehemu aitwae lawrance alishinda nyumbani kwao tu maeneo ya mavurunza kimara, ilipofika saa kumi kuna kijana aitwae john alifika nyumbani kwa akina lawrance kwa lengo la kumuomba akamtebgenezee bodaboda. ilipofika saa moja jioni wakaanza safari kuelekea mahali bodaboda ilipo, kufika kule kijana lawrance akafanikiwa kutengeneza ile pikipiki sasa ile aijaribu akiwa amempakia john na kijana mwingine ambaye hakufahamika hatua chache mbele wakasikia mwizi mwizi, john na yule kijana mwingine wakafanikiwa kuruka na kutokomea, lawrance kwa vile alikuwa hajui chochote akabaki ameduwaa ndipo walipoanza kumshambulia, akafanikiwa kuwachomoka akaingia kwenye nyumba moja bodaboda wakaizunguka ile nyumba kwa vitisho kuwa mwenye nyumba asipomtoa watachoma nyumba, wakaanza kuvuta mafuta toka kwa bodaboda zao, mwenye nyumba akaingia woga ikabidi lawrance atolewe wa bodaboda wakamtia mikononi kila alimshambulia anavyotaka mpaka mauti yalipomfika kila mtu akakimbia zake, baada ya uchunguzi ikagundulika kuwa john ndie aliyeiba bodaboda na wamemuua lawrance asiekuwa na hatia
Mimi yalishawahi kunikuta mwaka 2008, natoka kwenye tamasha la kampuni flani ya simu mida ya saa moja jioni(ilikua ufukwe mmoja maarufu dsm) nashangaa kundi la vijana kama kumi hivi wanakuja mbio huku wakiniuliza " simu uliyoiba iko wapi" .
Kabla sijapata hata muda wa kujitetea tayari nilishapigwa ngumi mfululizo za tumbo na uso mpaka macho yamevimba kiasi cha kutokuona vizuri,
Walipoanza kunisachi nikawa kama nazuia kwa kuweka mikono mfukoni, nilipigwa visu vya mikono, uso, mgongoni na mkononi mpaka leo nina makovu makubwa ya kutosha.
Kisha wakachukua kila kitu huku wakiendelea kunishambulia kwa kelele za mwiziiiiii mwiziiii, hapo sasa raia wenye hasira zao wakamalizia hasira zao kwangu(ninachoshukuru ilikua beach hakukua na mawe wala tofali, hivyo kilikua kipigo cha ngumi, mateke na makuti,) nakumbuka mpaka nililishwa mchanga kama adhabu,
Kwa kweli Mungu ni mkubwa, kilichoniokoa hata siamini mpaka leo.
Nikipata muda nitarudi kuwapa mkasa mzima ni wa kuumiza sana.
Asubuhi njema wakuu.
habari mkuu, kulikoni ?mbona unamtakia mtu mambo hayo?R.I.P Mkuu!
kwa hiyo usipokwenda kanisani ndiyo unapigwa kwa kusingiziwa mwizi?!