Hatari: Je, hili sio bao la mkono?

Hatari: Je, hili sio bao la mkono?

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,202
Reaction score
99,941
Miezi michache iliopita kuliripotiwa kukamatwa kwa BVR machines huko mikoani na week chache zilizopita kuna waliokamatwa tena machine hizo maeneo ya Mwenge Dar es salaam.

Wasiwasi wangu; kama kuna hizo machine zilizokamatwa je haiwezekani kuwepo na machine nyingi zaidi ambazo zimetumika kwa kazi hio haramu bila kukamatwa?

Je, kuna uhakikisho gani kuwa Vitambulisho hivyo havipo mtaani kwa baadhi ya watu?

LAKINI

Kuna majina mengi sana ya watu ambao tumejiandikisha na majina yetu hayapo kwenye list ya Wapiga kura ya NEC na kwa taarifa zilizozagaa mtaani ni kwamba NEC itaruhusu watu ambao wana vitambulisho hivyo lakini majina yao hayapo kwenye list iliyotolewa na NEC kupiga kura.

Swali ni kwamba

Je, kwakua vitambulisho hivi havipo kwenye NEC systems (japo ni halali) si vitachanganywa na vitambulisho vile feki? na kwakua hakuna mfumo tena wa uhakiki je huoni kuwa NEC wataingiza majina mengine mengi ya watu FEKI kupiga kura FEKI zenye mwelekeo wa kum-favor mgombea fulani?

Mimi binafsi nimekubali kushindwa, naomba NEC nao wasiruhusu watu kupiga kura ambao majina yao hayapo pale kwenye List ili kulinda uwezekano wa vitambulisho vile feki kuingizwa kwenye matumizi haya haramu. VINGINEVYO
NEC watoe maelezo mashine zile haramu ziliishia wapi na mashine zile zilizotumika zilihifadhiwa wapi hadi leo hii.
 
Hivi data za majina zinapoteaje kwanza.....majina yameandikwa kwenye form ...hata mfumo wa computer...mbona kama kuna usanii hiv...hiv wa tz tunaweza nn lakin hata kuweka record vizur hatuwezi.....
Mabadiko kiukwel lazima .....
 
Endeleeni kujiuliza maswali. Wenzenu tumeshafanya maamuzi. Magufuli ndiye Rais wetu
 
Hivi data za majina zinapoteaje kwanza.....majina yameandikwa kwenye form ...hata mfumo wa computer...mbona kama kuna usanii hiv...hiv wa tz tunaweza nn lakin hata kuweka record vizur hatuwezi.....
Mabadiko kiukwel lazima .....
Maswali yenu yakiisha tukutane kwenye ballot box
 
Tume ingekuwa huru tungesema waangalie namba ya mwisho ya vitambulisho vyao au wa-base kwenye jina, picha na namba za vitambulisho.
 
Magufuli hawezi pata 30% ya total votes...!!! Mtakuja niambia..!! Watu wagumu sana kujua nini kinaendelea ktk uchaguzi huu... kazi ushabiki tu..!!

CCM watu 90% hawataki hata kuisikia..!!
 
Magufuli hawezi pata 30% ya total votes...!!! Mtakuja niambia..!! Watu wagumu sana kujua nini kinaendelea ktk uchaguzi huu... kazi ushabiki tu..!!

CCM watu 90% hawataki hata kuisikia..!!
Mpwa wakati tukiwa na IMANI hio ni lazima tuchukue hatua na sio kuchekelea ushindi ambao bado hauko mikononi mwetu
 
Maswali yenu yakiisha tukutane kwenye ballot box

2157554521065238871
 
Endeleeni kujiuliza maswali. Wenzenu tumeshafanya maamuzi. Magufuli ndiye Rais wetu

Hivi hakuna namna Moderator kumblock huyu mtu lizabon pamoja na faizafox manake wamezidi kuandika -----!
 
Tumeshamaliza kazi.Rais ni Magufuli.alindwe vizuri.hila nyingi.hata hao wanaingilia misafara yake ni hola kwa kumuogopa.
 
Mzee jamaa wanahangaika sasa wameajiri vijana na kuwaweka hostel za chuo cha afya muhimbili iliyopo masaki ndio wanapiga simu kumchafua Lowasa
 
Mzee jamaa wanahangaika sasa wameajiri vijana na kuwaweka hostel za chuo cha afya muhimbili iliyopo masaki ndio wanapiga simu kumchafua Lowasa

Inauma na kukera sana sana Tanzania hakuna Democracy kama tunavyojidai
 
Back
Top Bottom