Hatari bunge la katiba!

Hatari bunge la katiba!

Kanuniya68

Senior Member
Joined
May 26, 2013
Posts
157
Reaction score
44
Kwa mujibu wa makubaliano yaliyo fikiwa wakati wa kupitisha kanuni juu ya nafasi ya mwenyekiti na makamu mkiti ni kwamba 'vigezo' vikuu ni pande mbili za muungano na jinsia!

Mimi ninadhani walipaswa kuongeza kigezo kingine,nacho ni 'kundi moja lisijaze nafasi zote pekee'. Kwa mfano, kama mwenyekiti ametoka CCM,basi makamu atoke kwenye makundi mengine na si CCM tena.

Hatari ninayoiona,ni utawala kuhodhiwa na 'kundi moja' ambalo ni CCM.,na hapa sina chuki na CCM,ila nataka 'kupanua' dhana ya uwakilishi sawa.
 
Kwa ujumla tunahitaji viongozi wazalendo tu bila kujali makundi. Anaweza kutoka kundi fulani na akawa mchumia tumbo tu
 
Mlikubali TShirt, Khanga, Kofia na Tujisenti twa 2,000/- na mkaaminishwa kwamba CCM itatawala milele, mkawapa "kura za kishindo!" Sasa CCM wanapotumia "ukishindo" huo ili kujustify mambo yao ndani ya Bunge Maalum la Katiba msilie! Yesu aliwahi kuwaambia Wanawake wa Kiyahudi kwamba wasimlilie yeye (Yesu), bali "wajililie wenyewe na Watoto wao!"
Kwa hiyo, mnaoililia CCM, kama mliichagua CCM, msilie bali jililieni wenyewe na watoto wenu!
 
kuna dalili ya mwanamama wa CCM kutoka zenji..kuukwaa umakamumwenyekiti...
 
Serikali zinazoongoza mchakato huu zote za CCM, Bunge Maalum la Katiba nalo tumelikabidhi CCM. Tusilalamike wala kunung'unika kwa yatakayotokea. Tumeyakubali wenyewe.
 
Back
Top Bottom