Hataki tusahau yaliyopita!!

Hataki tusahau yaliyopita!!

mahaba niue hayo. Yaani akise yeye msamaha uombe wewe lohhh.
 
mara nyingi anafanya yeye tunazungumza yanaisha, pia nikikosa tunazungumza yanaisha, lakini ya awamu hii alianza yeye nikaongea weee mpaka nikachoka, nilichoamua ni kua mimi nije kivingine kama sehem ya kumfanya alitambue kosa lake lakini amegoma na kuamua hivi alivyoamua.

kwa ufupi anapenda kuniburuza, sielewi ni kwa kua kanizidi miaka kadhaa au ni malezi ya kwao kuburuza mwanaume.

Sasa atapendaje kukuburuza kama wewe hupendi kuburuzwa?
 
mahaba niue hayo. Yaani akise yeye msamaha uombe wewe lohhh.

Yani mkuu, we acha tu. mimi nikikosa naomba msamaha yaishe tuendelee na safari, akikosa yeye kukubali kosa tu ni ishu. analeta zile za HAWA wa ADAM baada ya kula tunda aliulizwa umefanya nini badala ya kujibu alichofanya yeye akajibu "sio mimi ni nyoka alinidanganya nikala".
 
Sasa atapendaje kukuburuza kama wewe hupendi kuburuzwa?

kweli sipendi kuburuzwa na kwa mda mrefu nimevumilia nikiamini kua katika mapenzi hamuwezi kufanana tabia ktk hatua ya awali na hivyo nikawa najipa moyo kua atabadirika siku moja lakini mpaka sasa hakuna dalili ya changes.
 
mi nilidhani wewe ni mwanamke, kumbe ni mwanaume/ yaani kosa afanye yeye msamaha uombe wewe?
duh!! duniani kuna wanaume soft copy kweli!
hahahahah kiwatengu umeniacha hoi kwa kicheko,kwahyo siye wanawake ndo tunatakiwa tuwe soft copy? Afu nyie hardcopy eh? Hujawah kukutana na mahaba niue nin?kwel mapenz hayana formular..!
 
mara nyingi anafanya yeye tunazungumza yanaisha, pia nikikosa tunazungumza yanaisha, lakini ya awamu hii alianza yeye nikaongea weee mpaka nikachoka, nilichoamua ni kua mimi nije kivingine kama sehem ya kumfanya alitambue kosa lake lakini amegoma na kuamua hivi alivyoamua.

kwa ufupi anapenda kuniburuza, sielewi ni kwa kua kanizidi miaka kadhaa au ni malezi ya kwao kuburuza mwanaume.

Labda kwa kua kakuzidi umri.
 
Mimi msichana nakushaur
Achana nae kwa maana mwanaume anayejitambua halii ovyo ovyo kwenye mapenz kashakuona zoba mwanaume kauli na maamuzi like president na msimamo

Ukishaona hivyo jua kashapata mwingine wewe unaona kosa dogo pengine kwake ni kubwa na kapata njia ya kukupiga chin...kata mawasiliano akikutafuta pouwa akiendeleza kuuchuna jua ushapigwa chini
 
kama ww ni jinsia ya ke usichoke wala usikate tamaa mbembeleze tu atarudi ila kama ww ni jinsia ya me mzee chapa lapa..
 
aaah wewe,najua ngumu but huna jinsi hebu mpotezee jumla uone.huwa wana sifa sana ukiwa mtu wa amani.huyo kajua we umekufa kwake sasa muonyeshe kuwa yeye ni mosquito spell after kubonya unakaa zako nje.

Hongera kwa kupenda kuomba msamaha 'asking for forgiveness doesnt mean your wrong its a symbol of valuing your relationshp than your ego'
 
Yani mkuu, we acha tu. mimi nikikosa naomba msamaha yaishe tuendelee na safari, akikosa yeye kukubali kosa tu ni ishu. analeta zile za HAWA wa ADAM baada ya kula tunda aliulizwa umefanya nini badala ya kujibu alichofanya yeye akajibu "sio mimi ni nyoka alinidanganya nikala".
duuhh, pole sana. Hapo si pakubaki mkuu, we kaza mwendo usonge mbele.
Wako wengi sana wenye tabia njema na watakao deserve your love. Daima mbele, nyuma mwiko mkuu
 
Back
Top Bottom