Lord OSAGYEFO
JF-Expert Member
- Feb 19, 2021
- 3,086
- 4,881
Wadau kati ya katiba iliyopo na tume ya uchaguzi tatizo kubwa ni katiba iliyopo
Hata ikatokea Mh. Zitto kabwe akateuliwa kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi atake asitake lazima atatii maagizo ya boss wake aliyemteua siku ya kutangaza matokeo
Ninachotaka kusema katiba iliyopo ndio tatizo kubwa sana la nchi hii hivyo nilitarajia msajili wa vyama pamoja na zitto na wajumbe wao wangeanza kushughulikia suala la katiba mpya kwanza na sio tume ya uchaguzi masuala ya tume lazima yaanzie kwenye katiba kwanza
Km katiba iliyopo kuna kifungu kinasema
"Matokeo ya urais yakiisha tangazwa hayahojiwi popote"
Je, hiyo tume ya uchaguzi ya kina zitto na msajili wa vyama itakifutaje hiki kifungu bila kubadilisha katiba?
Watanzania ugomvi wetu ni katiba mpya suala la tume ya uchaguzi litafuata msajili na zitto msituvurugie suala la katiba mpya
Hata ikatokea Mh. Zitto kabwe akateuliwa kuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi atake asitake lazima atatii maagizo ya boss wake aliyemteua siku ya kutangaza matokeo
Ninachotaka kusema katiba iliyopo ndio tatizo kubwa sana la nchi hii hivyo nilitarajia msajili wa vyama pamoja na zitto na wajumbe wao wangeanza kushughulikia suala la katiba mpya kwanza na sio tume ya uchaguzi masuala ya tume lazima yaanzie kwenye katiba kwanza
Km katiba iliyopo kuna kifungu kinasema
"Matokeo ya urais yakiisha tangazwa hayahojiwi popote"
Je, hiyo tume ya uchaguzi ya kina zitto na msajili wa vyama itakifutaje hiki kifungu bila kubadilisha katiba?
Watanzania ugomvi wetu ni katiba mpya suala la tume ya uchaguzi litafuata msajili na zitto msituvurugie suala la katiba mpya