Hapa Tarime ving'ora vya ambulance vinalia kila saa

Hapa Tarime ving'ora vya ambulance vinalia kila saa

Ketoka

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2015
Posts
1,121
Reaction score
1,981
Sijawahi kuona hali hii tangu nizaliwe

Ving'ora vya ambulance zimekuwa vingi sana,kila baada ya saa moja ambulance inapita hasa hasa inatokea vijijini

Na Kwa mujibu ya watu wanaoishi Tarime vijijini wanasema misiba imekuwa mingi kuliko kipindi chochote yaani vifo vya ghafla vimekuwa vingi sana na watu wanaumwa kwa ghafla na misibani watu wanasongamana

Halafu viongozi wa wilaya wana magari ya serikali wamekaa kimya badala ya kupeleka elimu vijijini watu wajikinge na corona

Hata hapa mjini hali si shwari,ila ambulance zimelia kwa wiki hii,usiku na mchana na kila baada ya saa kadhaa
 
Poleni sana, kumbuka corona ipo na kisukari kipo kasema waziri wa afya
 
Mkuu hujui hali ya taifa ukisikia king'ora jua mgonjwa sasa hapo wakujua kuwa niwa tatizo la kupumua au haya ya kawaida ni doctor
 
Corona ya mitandaoni inatisha kweli tofauti na hali ilivyo kabisa
Kwaiyo ambulance ndio kipimo cha kuwa corona inaua sana,,!?
Sirens za ambulance zimekuwepo sana miaka ya hivi karibuni na hii ni kutokana na huduma hiyo kuboreshwa kwa kiasi kikubwa, leo hata vifo vya akina mama wakati wa kujifungua vimepungua na hii ni moja ya msaada mkubwa wa hizo ambulance,
Tuache ushabiki wa kiduanzi kwenye mambo serious,
Corona imekua corona ya Tweeter na JF tu kitaa sijaona hata kuku kufa kwa corona
 
Wewe unaongelea vijiji gani? Make na mimi nina ndugu kibao huko tarime, em tuweke wazi
 
Sijawahi kuona hali hii tangu nizaliwe

Ving'ora vya ambulance zimekuwa vingi sana,kila baada ya saa moja ambulance inapita hasa hasa inatokea vijijini

Na Kwa mujibu ya watu wanaoishi Tarime vijijini wanasema misiba imekuwa mingi kuliko kipindi chochote yaani vifo vya ghafla vimekuwa vingi sana na watu wanaumwa kwa ghafla na misibani watu wanasongamana

Halafu viongozi wa wilaya wana magari ya serikali wamekaa kimya badala ya kupeleka elimu vijijini watu wajikinge na corona

Hata hapa mjini hali si shwari,ila ambulance zimelia kwa wiki hii,usiku na mchana na kila baada ya saa kadhaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmeacha kunywa gongo?
 
Back
Top Bottom