kamanda, mie pia ni mwanaCDM na bado nitaendelea kuwa hivyo pamoja na kwamba naona uongozi wetu wa chama umetuangusha ktk sakata la zito.
Chama hakifanyi kazi kama banda la wauza miwa.
Uongozi hufanya kazi kwa mujibu wa taratibu na kanuni.
Zitto amepewa tuhuma zake kwa mujibu wa taratibu hizo hizo
Amezijibu kama anavyodai, tusubiri sasa hatua itakayofuata.
Nilidhani ungekuwa na malalamiko kwa Zitto kuwa pamoja na taratibu zilizowekwa, bado Zitto anaongoza makundi ya wahuni kufanya fitna.
bila unafki uongozi hauna consisteny kabisa ktk jambo hili.
Consistency unayoitaka ni ipi mkuu
gastone? Ngoja nikukumbushe..
1. Chama kilinasa waraka wa mapinduzi haramu
2. Kikachunguza
3. Katika
VIKAO HALALI wahusika wa mapinduzi waliitwa, wakahojiwa, wakakiri, wakaomba kujiuzuru nafasi zao
4. Kikao kikaamua wavuliwe nyadhifa zao wabaki kuwa wanachama na wajieleze kwa nini wasivuliwe uanachama
5. Inasubiriwa wakae waamue baada ya utetezi wao kufika chamani.
Unaitaka Consistency ipi mkuu?
- chama hakijawahi kutoa ushahidi na vielelezo vya usaliti wa akina zito.
Ungesema hivi, kwako wewe, waraka wa mkakati wa mabadiliko sio ushahidi tosha wa usaliti wa akina Zitto ningeheshimu maoni yako. Lakini kusema chama hakijatoa ushahidi wa usaliti wa Zitto ni matusi kwa Chama, ni kejeli kwa viongozi wa chama na ni dharau kwa wafuasi wenye nidhamu kwa chama. Unataka ushahidi upi zaidi ya huo mkakati wa kufanya mapinduzi ya uongozi wa Chama?
- dr slaa aliwahi kukaririwa kufunga mjadala huu - hii ilibaki kuwa kauli rasmi ya chama.
Ilitegemewa kuwa Team ya wafuasi wa Zitto wangeheshimu kauli hii ya katibu mkuu. Lakini pia hata Zitto mwenyewe tulitegemea angekuwa mfano kwa wafuasi wake kuheshimu kauli ya katibu mkuu. Lakini nadhani na wewe unaona wanavyofanya Zitto na team yake..Kosa sio kauli ya Slaa, Kosa ni matendo na response za team ya Zitto na Zitto mwenyewe.
- dr slaa, mbowe na hata lema wamesikika majukwaani wakimnanga zito.
Huu ni uongo. Ni ishara ya kutojiamini. Baada ya Zitto kuvuliwa nyadhfa zake, hakuna hata mmoja aliyemnanga Zitto. Labda useme kunanga ni kufanyaje lakini wao kama viongozi walikuwa wakitoa ufafanuzi wa nini kilitokea kwenye kamati kuu. Hakuna mahala Zitto amelalamika kunangwa na hao viongozi. Sasa kama Zitto mwenyewe hajalalamika wewe umeona wapi Zitto akinangwa?
baadae zito nae anaanza ziara mkoani kigoma lakini kwa upande wake inaonekana ni makosa.
Zitto hajakatazwa kutembelea waliompa kura. Na hakuna kiongozi wa Chadema atakayemkataza kufanya hivyo. Kwanza katiba haimzuii Zittop kufanya anachofanya. Wanaosema Zitto anafanya makosa wanazo sababu nyingine. Ngoja nikusaidie baadhi ya hizo sababu
1. Ziara za Zitto zinaratibiwa kwa ukaribu sana na vijana waliofukuzwa Chadema na kuhamia CCM
2. Ziara za Zitto zina malengo ya kuwauzia mgogoro wake binafsi watu wa kigoma. Kwamba ionekane kuwa Zitto ameadhibiwa kutokana na Ukigoma wake na sio UHUNI wake.
3. Ziara za Zitto sio za kujenga Chama. Ukiacha Kigoma kaskazini kwa wapigakura wake, Zitto "ameandaliwa" ziara za Kasulu na wilaya zingine za kigoma ambapo Slaa alipita siku za karibuni. Hatujengi chama kwa staili hiyo.
4...
5....
....
sasa wengine tulio huru tunahoji - kwa nn hakuna haki na usawa ndani ya chama?!
Mkuu, haki ipi na usawa upi unaoutaka? Haki ipi Zitto ameikosa? Zitto ameteuliwa kuwa mlezi wa kanda ya Magharibi, Alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Amekuwa Naibu Kiongozi wa kambi ya Upinzani, Amekuwa Waziri kivuli wa fedha. Zitto alifukuzwa na Samwel Sitta Bungeni bunge lililopita, Chama kilimbeba, kilizunguka nae, kilifanya nae mikutano nk. Zitto alisitisha uteuzi wa wagombea ubunge wa Chadema kwenye jimbo la Pinda kisirisiri tena akiwa peke yake bila kushauriana na viongozi wenzake. Chama kilimheshimu kama naibu katibu mkuu ingawa hakufata utaratibu na ilikuwa kinyume cha kanuni kama kiongozi. Hatukuona ukisifia busara za Chama nyakati zote hizo. Ila Zitto na wahuni wenzie kuandaa mkakati wa kukiua chama kwa kufanya mapinduzi ndio unalilia usawa na haki? Acha unafiq wewe
kwa nn tusifikiri kwamba kwa mtiririko huu zito anahujumiwa ndani ya chama - haswa kwa kuwa dr slaa kama katibu mkuu wa chama jana amesikika akimhukumu as if mawazo yake ni sawa na ya wajumbe wote wa cc.
Zitto akikihujumu chama wewe unasema ni haki na usawa. Tuliowapa haki ya kutazama chama wanapofanya kazi yao unakuja na hoja za Zitto Kuhujumiwa.
Nikuulize, Zitto anahujumiwa ili iweje?
Ni faida gani Chama kitapata kikimhujumu Zitto?
Ni lini Chama kilianza kumhujumu zitto?
Na unayaona matendo ya Zitto kwenye chama ni sawasawa?
Jana Slaa ameonya, kuwa timu inayomshauri Zitto haimsaidii. Itasababishwa Zitto afukuzwe. Wewe unaona mchezo wa ile timu ni sawasawa ila kauli ya Slaa ni ya kumhujumu Zitto?