Hapa CCM inahitaji pongezi kwa kuenzi demokrasia

kipara kipya

JF-Expert Member
May 2, 2016
14,128
16,100
amani iwe kwenu

Hapa lazima tuipongeze ccm na serikali yake kwa kuienzi demokrasia
kama ccm ingekuwa haienzi demokrasia watu fulani fulani tusingewasikia wakishutumu serkali ilihali wakiwa ndani ya chama

Na ndugu mwenyekiti ameonyesha kukomaa kisiasa sasa,tofauti kubwa na ule upande wa pili wa wale kasuku wa kukariri na nyumbu au nzi wafuata mizoga,maana wao wamebanwa hawana pa kumkosolea mwenyekiti hata kama anafanya makosa ya wazi

Leo demokrasia ilioenziwa na ccm tunaweza kuhoji mtu na akarudishwa,tuna uwezo wa kumtukana rais tutakavyo tuna uwezo wa kumtukana Rc bila woga na bado tukawa salama bila rabsha ewe mwenyezi mungu mzidishie busara rais wetu huyu

Sidhani kama hili lingewezekana kama nyumbu wangechukua nchi ingekuwa hakuna uhuru wa kujieleza wala kuhoji mifano ipo!

Na nchi ingetafunwa kiasi cha kutisha

Tumshukuru mungu kwa kutuepusha na balaa la nzige sasa nchi ipo salama nasi pia tupo salama tuna uwezo wa kutembea bila kudai ulinzi!

Aksanteni
 
Back
Top Bottom