Kama kungekuwa na Utaratibu kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya na miji wanaomba kazi kupitia Halmashauri hizo na Wanajadiliwa na Madiwani husika kabla ya ajira kwa manufaa ya Halmashauri zenyewe basi kwa vyovyote halmashauri hizi zilizo chini ya Vyama vya upinzani lazima zingepata maendeleo makubwa.
Tatizo mara nyingi hao Wakurugenzi wanateuliwa na Waziri na mara nyingi wanapelekwa kwenye halmashauri za upinzani wale wenye hulka ya kuweza kupambana na madiwani. Kwa maana hiyo hawaendi kufanya kazi za maendeleo bali kusudio ni mapambano. Umefika wakati sasa Halmashauri zipewe mamlaka ya kupata Wakurugenzi wake kwa vigezo vitakavyo wekwa na sio kuletewa majizi na wale wanaokuja na ajenda zao ikiwemo ile ya lazima "kumtoa Waziri Mkuu na waziri Tamisemi" kwa fungu maalum