Hakikwanza
JF-Expert Member
- Dec 11, 2010
- 4,043
- 1,012
Jamani ndugu zangu wa Tanzania hali ya umeme ni tete hapa Njombe mkoa mpya kwa jina, umeme unakatwa mara kwa mara pasipo hata taarifa kwa watumiaji. Hivi sasa wamekata umeme na hatujui hatma ya huu ukataji wa leo ni nini? Hivi kuna kupata maendeleo hii nchi? Umeme bei juu bado unakatika katika, tena bila taarifa. Jamani CCM na serikali yake ni balaa tupu.