peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 16,029
- 26,231
Hali ya uchafu imeendelea kutisha katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Moshi, ikiwa ni pamoja na stand kuu ya mabasi, kituo cha afya Mbuyuni, soko la Mbuyuni, kata ya Kiborloni, Njoro, Pasua, Mboma Mbuzi, Soweto, Majengo, Mji mpya, Mawenzi, soko la memorial, na soko la kati.
Tukizingatia kipindi hiki ni cha mvua, hali hii ina hatarisha afya za wananchi kwani inaweza kupelekea magonjwa ya mlipuko na magonjwa ya matumbo kutokana na muingiliano wa uchafu na vyanzo vya maji.
Tunazitaka mamlaka zinazohusika na usafi kuchukua hatua za haraka kumaliza tatizo hili.
Suala hili limekuwa kubwa hasa baada ya Mkurugenzi wa Moshi Manispaa kutoa zabuni kwa watu wasio na uwezo na vitendea kazi vya kutosha, ambao wanafanya kazi chini ya kiwango kuliko hata kipindi ambacho halmashauri ilivyokuwa inakusanya taka yenyewe.
Uchakavu wa magari na hali za wakusanya taka vinaonesha jinsi wazabuni hawa hawana uwezo wa kukusanya taka.
Wito wangu ni kwamba, ikiwa Manispaa imeshindwa, itoe zabuni hii kwa Jeshi la Magereza ambao tuna imani watasaidia kumaliza tatizo hili.
Kwa kifupi, Mkurugenzi wa Moshi Manispaa ameshindwa katika majukumu yake; anatakiwa awajibishwe na ikiwezekana abadilishiwe kazi nyingine.
Kazi ya ukurugenzi imemshinda, na sasa mji umekumbwa na kipindupindu, ambapo tangu uhuru, mji huo haujawahi kuathirika na ugonjwa huo.
Tukizingatia kipindi hiki ni cha mvua, hali hii ina hatarisha afya za wananchi kwani inaweza kupelekea magonjwa ya mlipuko na magonjwa ya matumbo kutokana na muingiliano wa uchafu na vyanzo vya maji.
Tunazitaka mamlaka zinazohusika na usafi kuchukua hatua za haraka kumaliza tatizo hili.
Suala hili limekuwa kubwa hasa baada ya Mkurugenzi wa Moshi Manispaa kutoa zabuni kwa watu wasio na uwezo na vitendea kazi vya kutosha, ambao wanafanya kazi chini ya kiwango kuliko hata kipindi ambacho halmashauri ilivyokuwa inakusanya taka yenyewe.
Uchakavu wa magari na hali za wakusanya taka vinaonesha jinsi wazabuni hawa hawana uwezo wa kukusanya taka.
Wito wangu ni kwamba, ikiwa Manispaa imeshindwa, itoe zabuni hii kwa Jeshi la Magereza ambao tuna imani watasaidia kumaliza tatizo hili.
Kwa kifupi, Mkurugenzi wa Moshi Manispaa ameshindwa katika majukumu yake; anatakiwa awajibishwe na ikiwezekana abadilishiwe kazi nyingine.
Kazi ya ukurugenzi imemshinda, na sasa mji umekumbwa na kipindupindu, ambapo tangu uhuru, mji huo haujawahi kuathirika na ugonjwa huo.