DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Hali ya barabara Kibaha Mailimoja, Mitaa ya Kwa Mang’umbi hadi Tankini, leo Desemba 28, 2025, ni ya kusikitisha, mara nyingi mvua inaponyesha inakuwa haipitiki kirahisi na hivyo kusababisha kero kubwa kwa usafiri wa kila aina wakiwemo watembea kwa miguu.
Wananchi tunajiuliza, viongozi wapo wapi? Barabara hii ni muhimu kwa maisha ya kila siku, lakini changamoto inazidi kuongezeka, kila mwaka Viongozi wa Kibaha na Pwani kwa jumla wanatuahidi kuwa itaboreshwa na wakati mwingine kupitisha greda kuikwangua, baada ya hapo hakuna kinachoendelea, shida ilirudi wanaanza kufanya yaleyale ya kuikwangua na ahadi nyingi.
Soma: Kairuki: Nitahakikisha barabara za jimbo la Kibaha kujengwa kwa lami
Wananchi tunajiuliza, viongozi wapo wapi? Barabara hii ni muhimu kwa maisha ya kila siku, lakini changamoto inazidi kuongezeka, kila mwaka Viongozi wa Kibaha na Pwani kwa jumla wanatuahidi kuwa itaboreshwa na wakati mwingine kupitisha greda kuikwangua, baada ya hapo hakuna kinachoendelea, shida ilirudi wanaanza kufanya yaleyale ya kuikwangua na ahadi nyingi.
Soma: Kairuki: Nitahakikisha barabara za jimbo la Kibaha kujengwa kwa lami