Habari Wakuu,
Yaani inapotokea mvua katika jijila Dar es Salaam ni kama adhabu kwa wakazi wa Mwanagati kuanzia kipande cha Kwa Mparange mpaka kituo Cha mwisho cha daladala Cha Mwanagati. Barabarani mbovu na haipitiki kwa urahisi.
Daladala zinalazimika kupandisha nauli, na Hata baadhi ya wamiliki magari wanalazimika kupaki magari yao, kuyaepusha kuharibika kwa hali ya barabara hii.
Safari ya nusu saa unalazimika kutumia saa zima kwa sababu magari yanatembea kwa kunyata.
Mbunge na viongozi wote tunaomba muangalie tatizo hili! Ukizingatia sasa Mbunge wa huku ni Waziri wa Ardhi tumatumaini barabara hii itafanyiwa kazi maana tuliambiwa bajeti tayari imetengwa. Mbunge Jerry Silaa tunaomba isiwe story kama za Vijiweni.
Hizi hapa chini ni baadhi ya picha ya hali ilivyo.