Hakutakuwa na Kampeni za Uchaguzi Arusha ..

Hakutakuwa na Kampeni za Uchaguzi Arusha ..

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2007
Posts
4,132
Reaction score
1,580
Kwa mujibu wa tangazo la tume ya taifa ya uchaguzi lililochapishwa leo kwenye gazeti la Mwananchi ktk ukurasa wa 38 ni kuwa Tume imetangaza rasmi hakutakuwa na kampeni kwenye uchaguzi wa kata nne za Arusha ambao utafanyika tarehe 30.06.2013 , tangazo hili limetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi Taifa.

sehemu imesomeka, ' Tume inachukua nafasi hii kufafanua na kusisitiza kuwa kwa kuwa uahirishwaji huo ulifanyika siku ya uchaguzi na baada ya kufungwa kwa kampeni kwa ajili ya uchaguzi mdogo,basi hakutakuwa na kampeni kwa ajili ya uchaguzi huo mdogo katika kata hizo nne za Jiji la Arusha .Lililobaki ni kupiga kura tu siku ya tarehe 30.06.2013.

Nawasilisha .
 
janja hiyo,wanataka waanze kutembeza rushwa nyumba hadi nyumba bila bugdha..
 
huo uchaguzi hautafanyika ili meya aendelee kula bata hata yale mabom sababu ni hiyo hiyo
 
Uchaguzi hapa Arusha hautafanyika tarehe 30/06 kama wanavyosema! Soon tutasikia uchaguzi umeahirishwa kwa muda usiojulikana kwani bado usalama sio wa kutosha au watasema kuna ugeni (Barack Obama) ili waendelee kuila halmashauri!

Their end is near!
 
Uchaguzi hapa Arusha hautafanyika tarehe 30/06 kama wanavyosema! Soon tutasikia uchaguzi umeahirishwa kwa muda usiojulikana kwani bado usalama sio wa kutosha au watasema kuna ugeni (Barack Obama) ili waendelee kuila halmashauri!

Their end is near!
Jiandaeni kwa lolote , hakuna vita mbaya kama ambayo inakushitukiza ukiwa hujajiandaa utashindwa tu.....
 
Naamini hata kama uchaguzi utafanyike next year bila kampeni cdm itashinda tena kwa kishindo, watu wa rchuga c kama wa iramba kwa nchemba, wengi wao waganga njaa na wafuata upepo wa mussa tindikali, lakin arusha hawako hivo... Cdm ushindi ni lazma no matter what.
 
Baadaye watasema: "kutokana na hali ya usalama wa mji wa Arusha kwa sasa, unatakiwa ukipiga kura urudi nyumbani kwako." Hata ile sheria inayosema unaweza kuwa umbali wa mita 100 wataikataa ili waibe kura
 
Baadaye watasema: "kutokana na hali ya usalama wa mji wa Arusha kwa sasa, unatakiwa ukipiga kura urudi nyumbani kwako." Hata ile sheria inayosema unaweza kuwa umbali wa mita 100 wataikataa ili waibe kura
kama yatakuwa hayo tabu itakuwa ileile
 
Back
Top Bottom