Hakuna cha Diamond wala Ali K, Shikamoo LINEX

Hakuna cha Diamond wala Ali K, Shikamoo LINEX

Msamiati

R I P
Joined
Mar 6, 2011
Posts
1,063
Reaction score
700
Habari zenu Waungwana,

Nimeona Bora niseme chochote kumpongeza Linex. Amini usiamini tunapozungumzia International standard kwenye music LINEX ni next level.

Huyu jamaa angekuwa na kihelehele cha wakina Diamond kuwashobokea wakina Kusaga sijui wakina luge... Basi leo tungekuwa tunazungumza mengine. Yaani jamaa anajua kuandika anasauti Unique mimi naweza kumpambanisha hata na JOE PRAIZE wa South Africa.

Owesome singers siku zote Hata wakiimba lugha usiyoielewa Utaburudika, utafurahia na cha ajabu utaelewa ujumbe alioimba. Ndio uwezo wa ajabu aliofikia LINEX, Kama huamini sikiliza Nyimbo yake mpya inayoitwa KIMUGINA.

Nahisi kuna kundi kubwa la watu wasiojua music ndio maana hawakauki kutupigia kelele humu mara Diamond mara Timu alikiba, Hamjui Music, Linex Ni top singer Bongo kwa sasa.

Kunawasanii wazuri sana Hapa mjini ambao wanafanya super standard music kama wakina Barnaba, Christian Bella, Linex, Grace Matata, Maua sama Nk, Hamuwafungulii thread na kuwaanzishia timu, mnakuja kuwataja watu wasiojua mziki kama diamond. Sasa mimi ndio timu LINEX

"Usi ni katili utamu wa penzi lako, Hata kwa shingo upande sipo tayari uende zako" LINEX
 
Ningekuelewa kama usingewataja Diamond na Ali Kiba kwenye kusifu kwako!

Ungeeleweka, ila hapo unapambanisha.
 
Sawa, ila why a comparison between him, Diamond and Alikiba?

Sija-compare ila nimejaribu kuonesha mshangao. mashabiki wote kuwashupalia hao jamaa hapa jukwaani kila kukicha wakati binafsi sioni maajabu yoyote wanayoyafanya. wanamuacha mtu kama LINEX kaimba KIMUGINA Kilugha lakini nyimbo imeeleweka.

Na Ngalikihinja Nadhani umenielewa.
 
ile wa salima katunga nani maana uko safi sana na hasa wa kiafka bwana. I like the songo
 
Linex Linex Linex huyu jamaa karibu nyimbo zake zote huwez kosa kachanganya kikwao kidogo japo sikijui ila huyu jamaa anajua HESHIMA kwako LINEX.
 
Huyo Linnex mwenyewe unayemkubali anamkubali Diamond ndo maana kamshirikisha kwenye nyimbo zake mbili
 
Mtoa post mziki sio kujua kuimba tu pekee " bali ni hardworking nidhamu ya kazi " na uchu wa maendeleo " kuitunza " kuipaisha na kuilinda brand yako pia ... inawezekana linex akawa anajua kuimba kweli kama unavyosema " lakini amekosa hizo sifa nilizozitaja hapo Juu ...
Kitu ambacho kinamfanya akose credit toka kwa mashabiki na wadau wanaofuatilia huu mziki wa bongo fleva "..
 
Back
Top Bottom