Hakika changamoto ya ajira imekuwa kubwa na Maisha yanazidi kunibana

Dec 10, 2020
48
111
Nipo katika kipindi kigumu cha Maisha kwa sasa ambapo changamoto zimekuwa kubwa sana na zinanibana. Nina degree ya utawala, pamoja na uzoefu na ujuzi katika mauzo, masoko, ukusanyaji wa data, na uandishi wa miradi. Aidha, nina ujuzi kompyuta, na uzoefu wa miaka 7 kwenye kazi na rekodi nzuri.

Kwa miaka 9 iliyopita, nimekuwa nikifanya biashara lakini sijaridhika na matokeo. Mara nyingi, biashara inafilisika sasa najikuta nikiumia hasa kwa kuzingatia majukumu yangu kama baba wa familia na nategemewa hivyo nimeamua kuachana kabisa na biashara kwa sasa.

Ndugu zangu, ninawaomba msaada wenu. Kama mdau wa jamii forum, naomba uniunganishe na fursa za kazi ambazo unadhani zinakidhi sifa na uzoefu wangu. Hata kama sijaelezea kila kitu hapa, nina hakika kwamba nina uwezo wa kufanya kazi katika maeneo yanayofanana na ujuzi niliouelezea.

Nipo Dar es Salaam kwa sasa, lakini nipo tayari kufanya kazi popote nchini. Ninajiamini katika kuzungumza lugha ya Kiingereza na Kiswahili vizuri.
 
Pole sana, ajira ni ngumu. Kama bado unamtaji jaribu kupambania biashara jaribu biashara tofauti tofauti, au jaribu kilimo pia. Soko la ajira nchini ni gumu labda private sector. Ila kama serekalini utasubiri sana.
 
Nipo katika kipindi kigumu cha Maisha kwa sasa ambapo changamoto zimekuwa kubwa sana na zinanibana. Nina degree holder utawala, pamoja na uzoefu na ujuzi katika mauzo...
Umejua kujieleza mkuu.

Mungu akasimame na wewe na akufanyie wepesi kwenye kada ya ulio somea, lakini kwa kukushauri tu for your kids future..... jitahidi kuwashauri wasomee kada ambazo hata wakikosa ajira wanaweza wakajiajiri kwa mitaji ya knowledge
 
Ajira tamu inakupa comfort zone na security japo mimi sijawah kuajiriwa ila naelewa hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…