Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,605
- 1,957
Wadau
Benki inapokua inafilisiwa, Deposit Insurance Board (DIB) ambayo ipo kwa mujibu wa kifungu cha 36 na 37 cha Sheria Na. 5 ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, hufanya utaratibu wa kuwalipa wateja amana zao.
Members wa bodi hiyo ni Gavana wa BOT (Mwenyekiti), Makatibu Wakuu wa Hazina wa Tanzania Bara na Visiwani, na Wajumbe wengine watatu ambao huteuliwa na Waziri wa fedha ambao ni wajuzi na wabobezi k atika masuala ya kibiashara, utaalamu au taaluma na wenye tabia na mwenendo mzuri na uzoefu ktk sekta ya zinazohusiana.
Bodi hutoa malipo ya awali kwa wateja wote ambayo kiwango cha kuanzia huwa Tsh milioni moja na nusu. Hii ni kwa mujibu wa tangazo la Serikali Na. 198 la mwaka 2010.
Kwa wateja ambao kiwango cha amana zao wakati wa ufilisi ni chini ya na hakizidi tshs 1.5m hao watalipwa amana zao zote kulingana na kiasi walichokuwa wameweka.
Kwa wateja ambao kiwango cha amana zao kitakuwa kimezidi 1.5m hawa kwanza watapokea hiyo 1.5m kama malipo ya awali kisha kiasi kilichobakia watalipwa baada ya mali zote za benki kuthaminishwa na kufilisiwa.
Ni wajibu wa yeyote anayeidai benki inayofilisika kuwasilisha maombi ya madai ukiambatanisha ushahidi wa nyaraka kwa hiyo bodi.Ili fedha ziweze kulipwa kutoka kwenye "protected deposit" ya bodi ambayo vyanzo vyake vya fedha hutokana na michango ya kila mwaka kutoka kwenye hayo mabenki nk.
Ikifikia hatua ya liquidation na kuteuliwa kwa mfilisi bodi itachukua au kupokea kiwango kilichozidi kutoka kny assets za benki kilichofidiwa kwa depositors. Hii kiutaalamu tunaiita "subrogation right".
Hivyo kiwango cha 1.5m ni kiwango cha awali na sio kiwango cha mwisho,baada ya kulipwa 1.5m ,unaandika maombi ya madai ukiambatanisha nyaraka zote kwa board ambapo utalipwa pesa zako zote kupitia protected deposits.
Chanzo: Maelezo kutoka Wataalamu wa Fedha/ Uchumi
Benki inapokua inafilisiwa, Deposit Insurance Board (DIB) ambayo ipo kwa mujibu wa kifungu cha 36 na 37 cha Sheria Na. 5 ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, hufanya utaratibu wa kuwalipa wateja amana zao.
Members wa bodi hiyo ni Gavana wa BOT (Mwenyekiti), Makatibu Wakuu wa Hazina wa Tanzania Bara na Visiwani, na Wajumbe wengine watatu ambao huteuliwa na Waziri wa fedha ambao ni wajuzi na wabobezi k atika masuala ya kibiashara, utaalamu au taaluma na wenye tabia na mwenendo mzuri na uzoefu ktk sekta ya zinazohusiana.
Bodi hutoa malipo ya awali kwa wateja wote ambayo kiwango cha kuanzia huwa Tsh milioni moja na nusu. Hii ni kwa mujibu wa tangazo la Serikali Na. 198 la mwaka 2010.
Kwa wateja ambao kiwango cha amana zao wakati wa ufilisi ni chini ya na hakizidi tshs 1.5m hao watalipwa amana zao zote kulingana na kiasi walichokuwa wameweka.
Kwa wateja ambao kiwango cha amana zao kitakuwa kimezidi 1.5m hawa kwanza watapokea hiyo 1.5m kama malipo ya awali kisha kiasi kilichobakia watalipwa baada ya mali zote za benki kuthaminishwa na kufilisiwa.
Ni wajibu wa yeyote anayeidai benki inayofilisika kuwasilisha maombi ya madai ukiambatanisha ushahidi wa nyaraka kwa hiyo bodi.Ili fedha ziweze kulipwa kutoka kwenye "protected deposit" ya bodi ambayo vyanzo vyake vya fedha hutokana na michango ya kila mwaka kutoka kwenye hayo mabenki nk.
Ikifikia hatua ya liquidation na kuteuliwa kwa mfilisi bodi itachukua au kupokea kiwango kilichozidi kutoka kny assets za benki kilichofidiwa kwa depositors. Hii kiutaalamu tunaiita "subrogation right".
Hivyo kiwango cha 1.5m ni kiwango cha awali na sio kiwango cha mwisho,baada ya kulipwa 1.5m ,unaandika maombi ya madai ukiambatanisha nyaraka zote kwa board ambapo utalipwa pesa zako zote kupitia protected deposits.
Chanzo: Maelezo kutoka Wataalamu wa Fedha/ Uchumi