Haki ya maandamano.

Haki ya maandamano.

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,196
Reaction score
7,532
Hivi hakuna maandamano yeyote yaliyopangwa kufanyika mwezi ujao ili tuhudhurie maana naona mwezi huu kimyaaa! Any way natania tu wakubwa.

Leo tutafakari kidogo haki ya maandamano.

Ninavyofahamu mimi ni kuwa; haki yeyote ile ya mtu, huishia pale haki ya mtu mwingine inapoanzia. Unaweza kukosoa au kutukana hapa ukipenda.

Sasa hebu fikiria "Scenerios" zifuatazo:

1.Unarudi kazini usiku saa mbili umechokaaaa! karibu na nyumba yako kuna mtu anauza pombe, kafungulia mziki kwa sauti kubwaaaaa, halafu ukimwambia apunguze au audhibiti usisambae ili uweze kulala, anakuambia anachokifanya ni haki yake, halafu anaendelea mpaka saa nane usiku.Unajisikia je? je! unadhhani ni sawa? unajifunza nini kwa haraka?

2. Mwanao anaumwa sana, anaonekana anashindwa kupumua, umeshauriwa kumuwahisha hospitali maeneo ya mjini, umekopa hela umekodi taxi kumkimbiza, unafika njiani unakuta njia haipitiki, unauliza kuna shida ganilunaambiwa mbele kuna maandamano, mwanao anapoteza maisha.Unajisikia je! unatafsiri je dhana ya haki za watu?

3. Umechukua ka-mkopo benki baada ya kuomba ajira kwa miaka mitano bila mafanikio.Umeanza kuuza vinjwaji barabarani.siku moja watu wanavamia kakibanda kako wanakunywa vinjwaji vyote kwa hoja ya kuwa yalikuwa ni maandamano. Utatafsirije kinachoitwa haki ya kuandamana?

Nadhani kwa scenerio hizi chache sasa naweza kuuliza swali la msingi.Hivi ikiwa lengo la maandamano ni kufikisha ujumbe kwa watu fulani, hakuna njia nyingine inayoweza kutumika na ikafikisha ujumbe bila kuleta madhara kwa watu wengine ili haki ya mtu mmoja isiwe kizuizi na kikwazo kwa haki za wengine, au haki za kundi fulani zisiwe kikwazo cha haki za wengine?

KARIBUNI;

attachment.php

 
Post zako zinanifunza kitu kimoja tu katika msemo wa watu wenye hekima kuwa ''kisebusebu na kiroho papo''...........
 
Au kwa lugha nyingine, kwa nini ufikishaji ujumbe kwa njia ya mikutano ya hadhara, press conference na mikutano ya kawaida isiwekewe mazingira mazuri zaidi kama njia kuu za ufikishaji habari na maandamano yakawekewe mazingira magumu zaidi kwa kuwa njia hiyo ina hasara kubwa kuliko faida na wakati kundi moja linaitumia, linaathi haki za wengine?
 
mwambie mbowe hayo maneno aupasue!

others don't think about others.
 
Post zako zinanifunza kitu kimoja tu katika msemo wa watu wenye hekima kuwa ''kisebusebu na kiroho papo''...........

Haufikiri kwamba kama ungejadili mada ingekuwa poa zaidi kuliko kunijadili mimi hasa ukizingatia kuwa mada hainihusu kwa namna yeyote! samahani lakini kama nitakuwa nimekukwaza.
attachment.php

 
Mkuu heshima kuu kwako iwe mkutano wa hadhar iwe barua au simu au hata radio lengo ni ujumbe ufike kwa wakati lakin unanoga zaid na unachukuliwa hatua haraka kma umekuja kwa haraka pia; maandamano ndio njia sahih ya kufikisha meseji kwa haraka hasa kwa watawala dhalimu na makupe wenzao kama act; tlp;udp nk so tutaandamana mpaka mwisho kwani kwenye maandamano hatukuwahi kuiba cha mtu wala kuharibu cha mtu ; tunapita kwenye barabara zilizo tengenezwa kwa kodi zetu kaka
Haufikiri kwamba kama ungejadili mada ingekuwa poa zaidi kuliko kunijadili mimi hasa ukizingatia kuwa mada hainihusu kwa namna yeyote! samahani lakini kama nitakuwa nimekukwaza.
attachment.php

 
Vijana wa kitanzania tupo tupu sana kichwani sijui shida ni nini..!? Eti hapa ni mtu kakaa kuleta mjadala wa kijinga kama huu na ukute anajiona GT..
 
Hivi ni kweli kila maandamano lazima yaishie kwenye fujo? Haiwezekani kuwa na maandamano ya amani?? Tuangalie pia kwa upande mwingine kwa nini kusiwe na utaratibu wa watu kuruhusiwa kuandamana kwa amani? Kwa sababu ilishasemwa maandamano ni haki ya kikatiba!
 
Au kwa lugha nyingine, kwa nini ufikishaji ujumbe kwa njia ya mikutano ya hadhara, press conference na mikutano ya kawaida isiwekewe mazingira mazuri zaidi kama njia kuu za ufikishaji habari na maandamano yakawekewe mazingira magumu zaidi kwa kuwa njia hiyo ina hasara kubwa kuliko faida na wakati kundi moja linaitumia, linaathi haki za wengine?[/QUOTE

Habari za jioni kaka, kwa bahati mbaya umezungumza maandamano kwa ujumla. Ulipaswa kusema ni maandamano ya aina gani maana hata makanisani huwa tunaandamana wakati wa ekaristi na huwa tunakuwa bugudha kwa watumiaji wengine wa barabara. Misafara ya viongozi pia huwa bugudha kwa watumiaji wengine wa barabara. Ama kama lengo lako ni kupotosha na kujenga taswira inayojaribu kujengwa na watawala kuhusu maandamano ya wapinzani. Lakini kama kweli una lengo la kuzungumzia maandamano ni lazima ungeshauri maandamano yawe ya amani na kufikisha ujumbe kwa njia ya amani. Nakumbuka enzi za Nyerere kabla ya vyama vingi tulikuwa tunaandama sana kuunga kauli mbiu za wakati huo na hata shughuli zilisimama kwa ajili ya maandamano hayo. Unajua ni kwa nini hali hiyo iliwezekana wakati huo? Ni kwa sababu tulikuwa tunawaza sawa au tulilazimishwa kuwaza sawa. Leo hii waliozoea maandamano ya kuwasifia wamekutana na maandamano yasiyowasifia bali ya tofauti. Kwa hiyo ninachokiona mimi hapo ni ulimbukeni tu wa kukutana na changamoto ya mawazo tofauti na ya kwako.

Hicho ndio ninachokiona kwenye maandamano haswa ya wapinzani especially cdm. Na kwa bahati mbaya ccm wameamua kulitumia jeshi la polisi kuwazuia hao cdm huku wakijua watakaidi na wao watumie kama kete ya wapinzani ni watu wa fujo. Ila nikuhakikishie nchi yoyote inayozuia maandamano ya amani ni lazima itakuwa ama hujenga utawala usiowajibika. Mara nyingi binaadamu ana tabia ya kuwa mtekelezaji bora iwapo anapata mashinikizo, lakini iwapo wananchi wanatumia miziki laini (blues) kuwawajibisha viongozi humo maendeleo mtayasubiri sana.
 
Vijana wa kitanzania tupo tupu sana kichwani sijui shida ni nini..!? Eti hapa ni mtu kakaa kuleta mjadala wa kijinga kama huu na ukute anajiona GT..

na bado aliye comment hapo kumkomoa mwingine anajiona yuko mtimilifu sana kichwani mwake...
 
na bado aliye comment hapo kumkomoa mwingine anajiona yuko mtimilifu sana kichwani mwake...

Tatizo kila mtu anamshangaa mwenzake jinsi alivyo wa ajabu.Kazi kweli
96fabf46a249348f7bcfd9897d9b4c76.jpg

 
Back
Top Bottom