Mkuu Mashauri, hili linawezekana kabisa hata nchini kwetu kama hao (mafisadi) walio madarakani wangeweka maslahi ya Tanzania na Watanzania mbele badala ya kununuliwa kwa kupewa shares chache katika makampuni hayo na hivyo kuwaachia wachukuaji wachukue 96%/97% na kutuachia sisi kiduchu tu na mashimo chungu nzima na huku wamechafua vyanzo vingi vya maji katika maeneo yenye rasilimali.