Habari njema: Ama kweli Tanzania ni nchi ya neema - Utajili mwingine wa gesi wagunduliwa tena!


Ni kweli kabisa BAK. Hawa mafisadi wangeweka mbele maslahi ya taifa lao hiyo inawezekana kabisa na nchi yetu ingepeata maendeleo kwa kasi. Mbaya zaidi ni kuwa hata hizo share wanazopewa kwenye hayo makampuni pesa zao wanawekewa nje ya nchi na mwisho wa siku wanakufa na kuyaacha hayo matrilioni yakiendeleza nchi za wazungu. Mbaya sana hii. Mkapa aliuza madini yetu na Kikwete anaendelea kuyauza na gesi asilia pia, Mwinyi aliuza mbuga za wanyama ili hali wanafahau fika kuwa hata wakistaafu wanatunzwa na serikali mpaka kufa kwao, sijuwi wanataka hizo pesa zaidi za nini! Inashangaza sana hawa viongozi wetu wa kiafrika.
 
Reactions: BAK

Sawa kabisa mkuu.
Wanorwegian kwa asili ni watu waaminifu sana. Huko kwao wanaishi maisha ya haki sijawahi kuona. Kampuni yao ya StatOil ni mojawapo ya makampuni yanayofanya utafiti wa gesi na mafuta TZ na wangeweza kuipa share serikali ya 49 % na wao wakachukua 51% kama ilivyo huko kwao. Tatizo wakija huku kwetu wanakuwa corrupted na viongozi wetu. Niliwahi kusikia kuwa kuna mzungu mmoja alikuwa analalalimika kuwa si kwamba hawapendi kulipa kodi kweny uwekezaji mfano madini etc ila wanasema mwekezaji akija wa kutaka kutenda haki yaani alipe kodi na kiongozi asipewe mgawo ananyimwa leseni.
 
Ila wakija kwetu wakikuta hiyo nafasi yakuwapunguzia gharama wanaitumia ipasavyo. Mi nawaeelwa vema hawa watu. Mzungu ni mzungu tu ndugu. Usipokuwa na mapenzi na uzalendo na nchi yako usitegemee atakuja kukufundisha uwe mzalendo! They always seek for their permanent interest and not permanent friends of enemies!


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…