Godbless J Lema
Arusha MP
- Sep 28, 2013
- 92
- 2,204
Heri ya Christmas kwa Mahabusu na Wafungwa wote.
Christmas mwaka Jana 2016 nilikuwa nimeshikiliwa kama mahabusu Geraza kuu Arusha kwa kunyimwa dhamana, tukiwa Gerezani tarehe kama hii Mimi na wenzangu tulikuwa tunaandaa sikukuu ya Christmas.
Leo ninawakumbuka rafiki zangu wengi niliokaa nao vizuri, Wengine wamefungwa na wengine bado wako mahabusu , kwa kweli zaidi namkumbuka sana Wakili Median Mwale ambaye amekuwa mahabusu kwa kipindi cha zaidi ya miaka sita. Siku hiyo ya Christmas baada ya ibada iliyoongozwa na Askofu Lebulu , tulifanya maandalizi ya kula chakula ambacho familia zetu zilituletea , tukiwa tunakula Wakili Mwale alisema, Mh Lema wewe utatoka , na Mimi na wenzangu na muomba Mungu Christmas inayokuja niweze kuwa nje, kwa bahati mbaya Wakili Median Mwale na rafiki zake bado wameshikiliwa Gerezani . Inauma sana kwamba Ofisi ya Dpp na Mahakama kwa zaidi ya miaka sita wameshindwa kumaliza shauri hili.
Kumweka mtu Mahabusu kwa miaka yote hii ni ukatili mbaya sana, kwa kipindi ambacho nimekuwa Magereza nimeweza kuelewa huzuni za familia na watuhumiwa, ndio sababu wakati Mh Rais alipowasamehe Wafungwa hasa wenye makosa makubwa nilimshukuru sana only kwa sababu najua huzuni ya kukosa uhuru.
Wakati Leo nina wakumbuka na kuwatakia heri ya Christmas njema mahabusu na Wafungwa wote Nchini ni muhimu watu wote mlioko kwenye vyombo vya sheria mjue kwamba wajibu wenu unapokosa utu na upendo maana yake ni kuumiza watu na kutesa watu mahali fulani .
Ninamuomba Mh Rais, aingilie kati suala la Wakili Median Mwale, kwa kweli huyu mtu inatosha kuwepo Magereza kwa zaidi ya miaka sita bila kuhukumiwa.
Dpp najua unajua kuna watu wengi wako Magereza kama Median Mwale,nguvu uliyopewa na sheria inapokosa upendo basi nguvu hiyo inakuwa ni ukatili .
Krismas Njema Mahabusu na Wafungwa wote Nchi nzima.
Godbless Lema (MB)
Christmas mwaka Jana 2016 nilikuwa nimeshikiliwa kama mahabusu Geraza kuu Arusha kwa kunyimwa dhamana, tukiwa Gerezani tarehe kama hii Mimi na wenzangu tulikuwa tunaandaa sikukuu ya Christmas.
Leo ninawakumbuka rafiki zangu wengi niliokaa nao vizuri, Wengine wamefungwa na wengine bado wako mahabusu , kwa kweli zaidi namkumbuka sana Wakili Median Mwale ambaye amekuwa mahabusu kwa kipindi cha zaidi ya miaka sita. Siku hiyo ya Christmas baada ya ibada iliyoongozwa na Askofu Lebulu , tulifanya maandalizi ya kula chakula ambacho familia zetu zilituletea , tukiwa tunakula Wakili Mwale alisema, Mh Lema wewe utatoka , na Mimi na wenzangu na muomba Mungu Christmas inayokuja niweze kuwa nje, kwa bahati mbaya Wakili Median Mwale na rafiki zake bado wameshikiliwa Gerezani . Inauma sana kwamba Ofisi ya Dpp na Mahakama kwa zaidi ya miaka sita wameshindwa kumaliza shauri hili.
Kumweka mtu Mahabusu kwa miaka yote hii ni ukatili mbaya sana, kwa kipindi ambacho nimekuwa Magereza nimeweza kuelewa huzuni za familia na watuhumiwa, ndio sababu wakati Mh Rais alipowasamehe Wafungwa hasa wenye makosa makubwa nilimshukuru sana only kwa sababu najua huzuni ya kukosa uhuru.
Wakati Leo nina wakumbuka na kuwatakia heri ya Christmas njema mahabusu na Wafungwa wote Nchini ni muhimu watu wote mlioko kwenye vyombo vya sheria mjue kwamba wajibu wenu unapokosa utu na upendo maana yake ni kuumiza watu na kutesa watu mahali fulani .
Ninamuomba Mh Rais, aingilie kati suala la Wakili Median Mwale, kwa kweli huyu mtu inatosha kuwepo Magereza kwa zaidi ya miaka sita bila kuhukumiwa.
Dpp najua unajua kuna watu wengi wako Magereza kama Median Mwale,nguvu uliyopewa na sheria inapokosa upendo basi nguvu hiyo inakuwa ni ukatili .
Krismas Njema Mahabusu na Wafungwa wote Nchi nzima.
Godbless Lema (MB)