Godbless Lema awapokea watu watatu waliotembea kwa miguu kutoka Mwanza kuja Arusha kumtia moyo

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,242
34,903
Unamkumbuka kijana Benjamin wakati wa Azimio la Arusha? Aliyetembea kwa miguu kutoka Arusha kwenda Dar kuunga mkono Azimio la Arusha akafia mkoani Kilimanjaro baada ya kuugua maleria kali? Aliitwa shujaa wa Azimio. Matembezi ni moja ya mambo yanayoweza kufikisha ujumbe wa kishujaa juu ya jambo fulani.

Hali hiyo ndiyo imesababisha vijana watatu wa mkoani Mwanza, kufunga safari kutokea Mwanza kwenda Arusha KWA MIGUU wakitembea, na kufanya DUA Maalumu njiani ya kumuombea Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe.Godbless Lema, baada ya kukaa gerezani kwa muda mrefu.

Vijana walianza safari tarehe 02/03/2017 ikiwa ni siku moja tu kabla ya Mhe.Lema kuachiwa kwa dhamana. Lengo la kufanya maandamano hayo ya umbali mrefu wa takribani kilomita 1,000 ilikua kumsalimia Mhe.Lema katika Gereza kuu Arusha (Kisongo), na kutuma ujumbe wa kishujaa kwa watawala juu ya kutokukubaliana na uonevu aliofanyiwa Lema. Lakini kabla ya kumaliza safari yao Lema akawa ameshapata dhamana.

Walimshukuru Mungu na kuona amejibu Maombi yao, lakini hawakukatisha safari yao. Takribani siku 17 sasa wanatembea usiku na mchana kufika Arusha, wakilala masaa machache kwenye maeneo ya shule wanazokutana nazo njiani.

Kwa sasa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe.Godbless Lema Amesha wapokea watu hawa watatu Muda huu nyumbani kwake.
 

Attachments

  • IMG-20170319-WA0070[1].jpg
    IMG-20170319-WA0070[1].jpg
    115.8 KB · Views: 49
  • IMG-20170319-WA0069[1].jpg
    IMG-20170319-WA0069[1].jpg
    186.1 KB · Views: 46
  • IMG-20170319-WA0072[1].jpg
    IMG-20170319-WA0072[1].jpg
    119.6 KB · Views: 46
  • IMG-20170319-WA0071[1].jpg
    IMG-20170319-WA0071[1].jpg
    98 KB · Views: 47
Unamkumbuka kijana Benjamin wakati wa Azimio la Arusha? Aliyetembea kwa miguu kutoka Arusha kwenda Dar kuunga mkono Azimio la Arusha akafia mkoani Kilimanjaro baada ya kuugua maleria kali? Aliitwa shujaa wa Azimio. Matembezi ni moja ya mambo yanayoweza kufikisha ujumbe wa kishujaa juu ya jambo fulani.

Hali hiyo ndiyo imesababisha vijana watatu wa mkoani Mwanza, kufunga safari kutokea Mwanza kwenda Arusha KWA MIGUU wakitembea, na kufanya DUA Maalumu njiani ya kumuombea Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe.Godbless Lema, baada ya kukaa gerezani kwa muda mrefu.

Vijana walianza safari tarehe 02/03/2017 ikiwa ni siku moja tu kabla ya Mhe.Lema kuachiwa kwa dhamana. Lengo la kufanya maandamano hayo ya umbali mrefu wa takribani kilomita 1,000 ilikua kumsalimia Mhe.Lema katika Gereza kuu Arusha (Kisongo), na kutuma ujumbe wa kishujaa kwa watawala juu ya kutokukubaliana na uonevu aliofanyiwa Lema. Lakini kabla ya kumaliza safari yao Lema akawa ameshapata dhamana.

Walimshukuru Mungu na kuona amejibu Maombi yao, lakini hawakukatisha safari yao. Takribani siku 17 sasa wanatembea usiku na mchana kufika Arusha, wakilala masaa machache kwenye maeneo ya shule wanazokutana nazo njiani.

Kwa sasa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe.Godbless Lema Amesha wapokea watu hawa watatu Muda huu nyumbani kwake.


Hahaha CCM wakitoa mguu chadema ndo wanakanyaga, msisahau lkn pia kufanya reforms ndani ya Chama, mumtoe Mumyani Mbowe!
 
Hizo siasa nazifananisha na za Mzee mmoja kufuatwa na wachungaji na masheikh Ili agombee uraisi mwishowe akaukosa... Wakati huo Lema amefuatwa na watu Hao watatu Dr Ndungulile kwake kigamboni anatarajia kufungua kivuko kipya chenye Jina la MV KAZI
 
Wao badala ya kukaa wafanye shughuli ya kuwaingizia kipato wanahangaika na Lema..Lema ni political businessman..hilo jumba unaloliona kalijenga kupitia siasa..so unapodili na wanasiasa inabidi ujiongeze kidogo..alimsema sana lowasa na kumtukana..leo kiko wapi?? Ipo siku ataudhiwa chadema ataenda ccm..maana hatukujua kama lowasa ipo siku ataiacha ccm..kwa wanasiasa wa sasa inahitaji umakini kuwashabikia maana hujui aliwazalo kichwani
 
Back
Top Bottom