Godbless Jonathan Lema kuweka rekodi mpya Arusha Mjini

Godbless Jonathan Lema kuweka rekodi mpya Arusha Mjini

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Jimbo la Arusha Mjini, kadiri nijuavyo, halikuwahi kuongozwa na chama cha upinzani kwa vipindi viwili. Mbunge wa kwanza wa upinzani alikuwa Mhe. Makongoro Nyerere (aliyekuwa NCCR-Mageuzi) aliyelinyakua Jimbo hilo mwaka 1995 lakini baadaye ubunge wake ulitenguliwa na Mahakama.

Mbunge aliyemaliza kipindi chake cha 2010-2015 ni Godbless Jonathan Lema wa CHADEMA. Tayari ameshawatumikia wananchi wa Arusha Mjini kwa kipindi cha miaka mitano. Uchaguzi wa Arusha Mjini uliahirishwa hadi tarehe 13/12/2015 kufuatia kifo cha aliyekuwa mgombea wa ACT-Wazalendo, Marehemu Estomil Malla.

Mnamo tarehe 13/12/2015, Lema ataingia kwenye rekodi mpya kwa kuwa Mbunge wa kwanza wa upinzani kuiongoza Arusha Mjini kwa vipindi viwili mfululizo. Wabunge wa zamani wengine wa Arusha Mjini ni Mhe. Abdurahman Kinana na Felix Christopher Mrema.

Najua kuwa Mhe. Lema anaendelea kufuata katazo la wananchi wake wa Arusha Mjini waliomtaka asipige kampeni na asubiri tu ushindi wa kishindo. Kimahesabu, kura za Arusha Mjini zaweza kukipa chama kitakachoshinda kiti cha Mbunge wa viti maalum kwakuwa zaweza kuwa nyingi kuliko jumla ya baadhi ya majimbo.

Kila la heri G. J. Lema kwenye uchaguzi wako wa tarehe 13/12/2015.
 
Liwake, inyeshe, aje Kikwete, Magufuli, Salma ,binamu yake Salma....Lema Ni Mbunge wa Arusha 2015-2020
 
Subiri uchaguzi uishe ndio uongee, huyo lazima apigwe chini, watu wa Arusha wamechoka na vituko vyake.
 
Lema tenaaaaaaaaaaaa Arusha.Arusha bila lema haiwezekani.
 
MBUNGE haongozi jimbo.ni muwakilishi bungeni.viongozi ni Mkuu wa Mkoa,Wilaya na Kata
 
Mabadilikooooooooooooooooooooooooooo
 
Ana nyota kali sana huyo MTUMISHI wa watu wa ARUSHA MJINI, TZ in general !
 
Subiri uchaguzi uishe ndio uongee, huyo lazima apigwe chini, watu wa Arusha wamechoka na vituko vyake.
We unaongelea Arusha ipi? wenzio huku UKAWA wamebana kila kona, bao la mkono labda wakapigie chooni.
 
nakutakia kila la kheri Lema...CCM wala msijisumbue January hapo hata ukijaribu kuiba watakukata kischwa hao waa rusha..ohooo siyo mbumbu kama watu wa bumbuli wanadangnywa na umaarufu wa baako mla rushwa kufar! najua utasema leta ushahidi
 
Subiri uchaguzi uishe ndio uongee, huyo lazima apigwe chini, watu wa Arusha wamechoka na vituko vyake.

Wewe ndio umesema:what: Lema ndio mbunge wa Archuga, Mtake msitake nyie magamba..!!
 
Arusha ata aende nani ccm nendeni na kinana marais wote wanne na wabunge wote Wa ccm mlioshinda hawawezi pata ata robo ya kura za lema makamanda Arusha tunapata na kiti maalum
 
Back
Top Bottom