God is real

Mish Albert

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2015
Posts
657
Reaction score
582
Habari Wana Jamii intelligence
Mda mrefu kweli,nilitamani kuwe na Uzi ambao Watu watakua huru kutoa Ushuhudu Binafsi kuhusu uwepo wa Mungu katika Maisha Yao

Jinsi gani Mungu amewapigania mpaka walipo ivi Sasa au Ni Mikasa ipi waliowahi kuipitia inayowafanya kuamini uwepo wa Mwenyezi MUNGU katika ulimwengu huu
Hii pia itawasaidia ndugu wetu wengi waliopotezwa na fikra finyu za kutoamini Uwepo wa Mungu

Watu wa dini zote wanakaribishwa kutoa Ushuhuda wao Binafsi kuhusu uwepo wa Mungu(Personal revelation)
My take:

Huu sio Uzi maalum kwa ajiri ya mabishano yasio na msingi ya wale wanaodai "Kutokuwepo kwa Mungu"
Nauita Ubishi usio na msingi kwa sababu moja kuu....Kuna watu wanakana uwepo wa MUNGU kwa kusingizia kuwa hakuna ushaidi wowote wa kisayansi kuhusu Mungu

Sayansi ni Nini? na Ina nguvu kiasi gani Cha kuamua nini tuamini?

Wakana Mungu wengi hawafaham Kitu kimoja kuhusu sayansi
Sayansi ni falsafa(dhana tu) Kama falsafa nyingine

Kila mtu Ana falsafa yake kuhusu Maisha,Kuna wenzetu wa "Buddha" wanaamini nafsi haifi Bali huhama Hama katika miili tofauti tofauti kulingana na matendo yake(karma)

Kama walivyo "Buddha" Wanasayansi pia Wana falsafa Yao kuhusu ulimwengu....kuwa ulimwengu umeundwa na "Maada tu"(materialism)

Na hii Ndio falsafa nzima ya sayansi
Sasa falsafa dhaifu Kama hizo,haziwezi kuthibitisha chochote ambacho sio "maada" ikiwemo MUNGU

Pia sayansi na heshima yake yote,inaweza kuelezea 10% ya ulimwengu....90% zote hazifahamiki vipi Sasa inatwambia Mungu hayupo?(kwa maelezo zaidi "Google Dark matter &Energy")

ila Kama una swali lolote au Jambo lolote linalokupa mashaka kuhusu uwepo wa MUNGU na unataka kuelewa(sio kubishana) au Kuna hoja ya wakana Mungu ulioshindwa kuijibu waweza kuuliza na tukakusaidia kuijibu
Karibuni wanajamvi

#GOD IS REAL....
 
Issue nyingi Sana zimeshindwa kuthibitishwa kuhusu uumbaji wake kisayansi, kwa maana hiy, uumbaji wa dunia na ulimwenguni Kwa ujumla haujaweza kuelezewa Kwa mapana yake na sayansi Tu, kuna nguvu isiyoonekana imefanya yote haya tena Kwa usahihi mkubwa Sana pasipo kukosea chochote. Kila kitu kimepangwa kikapangika Kwa mahesabu makali, hiyo nguvu naiita Mungu mwenyezi mwenye enzi na mamlaka yote katika vyote vinavyoonekana na visivyoonekana Kwa macho ya nyama.a Aimidiwe milele, Amina.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuamini uwepo wa Mungu/akili iliyotokeza huu ulimwengu sio mpaka upate msaada fulani wa kimiujiza.
Kadhalika nje kabisa ya vitabu vyote vya dini mimi na wewe ndio vitabu vikuu zaidi kuliko hivyo vya maandishi.

Jiulize kidogo tu wewe hapo ulipo una miaka mingapi na hujawahi kupoa japo umeishi mazingira yenye baridi kali?

Umeshawahi kufikiri namna DNA inavyofanya kazi kwa usahihi na kuhifadhi taarifa zote sahihi kuhusu kiumbe kuliko mashine yoyote iliyowahi kubuniwa na mwanadamu?
Umeshawahi kufikiri vile mwili wako unavyofanya kazi za ajabu na za kuogofya?
Je, Ulishawahi kufikiri namna kuna magimba makubwa huko angani mara elfu kadhaa ya dunia, huku yakijiendesha kwa usahihi kabisa kuliko vyombo vyote vya usafiri vilivyowahi kutengenezwa na mwanadamu, tena magimba hayo yamejiendesha kwa miaka bilioni kadhaa bila kukosea?
Je, ulishawahi kufikiri namna mapenzi yalivyo matamu?

Wewe unadhani maada zilizojitengeneza zenyewe zinaweza kupanga zikakutane alafu zifanye kwichikwichi huku zikipata utamu unaoupata?

TAFADHALI KAMA UPO NA MTU YEYOTE HAPO HEBU MTAZAME KWA SEKUNDE KADHAA AU DAKIKA KADHAA.

Umeona nini?
Bila shaka umemwona mtu mwenye macho mawili mazuri sana yenye maajabu ya kuona na kutambua kwa kupitia ubongo ambao unatenda kazi kwa kutegemea kemikali nyingi sana ambazo hupatikana kwenye vyakula tunavyokula, pua yake inayovutia ambayo inaweza kutambua hadi aina ya chakula kilicho karibu au kinyesi na nk kwa kutegemea ubongo huohuo.
Pia umeona nywele zake nzuri, ngozi safi yenye hadi vinyweleo vya kutolea jasho.
Nyuzi zake ambazo zipo juu ya macho kidogo ambazo wanadamu wote tunazo na hazijawahi kubadilika zikaota mgongoni au nyuma ya shingo.

Kama unaweza hebu mwambie atembee, kisha jiulize tena kama kuna mashine tata kama tulivyo sisi ambayo inaweza kujileta tu yenywe pasipo na muundaji wake aliye na maarifa makubwa sana!

Je, ni jambo linalopatana na akili kwamba sisi tulitokea tu kwa kemikali kujikusanya zenyewe hadi kututokeza tukiwa na macho, masikio yenye kutambua hadi sauti ya adui yako, pua iliyokaa palepale, miguu yenye kucha zenye amri ya kuwa vilevile kupitia DNA ya mwanzo?

Mambo hayo yaweza kutokea tu kwenye kiwanda cha kisasa kilichoandaliwa na mbunifu makini

Kemikali zisingeweza kujikusanya zenyewe ziweke na amri au sheria ya upatikanaji wa mtoto kwa kungonoka watu wa jinsia tofauti huku DNA ikijigawanya pande zote mbili kwa kutembea na taarifa sahihi za pande zote kuanzia kwenye ngozi mpaka kwenye kucha, miguu, sauti kwa kiasi na mambo mengine mengi.

Hata kama inawezekana jambo hili lingekuwa vipi kwa viumbe tofautitofauti?

Tukubali tu kuna wajanja au mjanja aliyefanya haya hata kama hatumjui.

Mimi sio muumini wa dini yoyote ila siwezi sema haya mambo yamejiunda yenywe tu! Hapana

Kwahiyo maada zilijitokeza zenyewe, zikaunda magimba kila moja kwa namna yake huku zikijiunda zenyewe hadi kutokeza viumbe tata kama sisi?
Tena maada hizohizo zikaweka na sheria za kudumu kwenye mambo tata yanayoendelea ndani ya miili ya viumbe na kwenye ulimwengu kwa ujumla?

Kunae mtaalamu wa haya ila hatujui nae katokea wapi.

Kuuliza mtaalamu wa haya yote alibuniwa na nani ni sawa siku moja tutengeneze robot lenye uwezo wa kuhoji, alafu lituhoji nini chanzo chetu/yaani tulianzaanzaje hadi tukawepo hapa duniani....bila shaka hatutoweza kumpa jibu la uhakika robot wetu. Hivyo swali hilo tunapaswa tukae kimya kwanza mpaka tutakavyojiongeza zaidi kimaarifa mara makumi kadhaa!
Tuujue kwanza ulimwengu A-Z, tumjue muundaji wake vyema ndipo tumuulize kwa upole alipotokea

Sitaki maswali kwakuwa hata mimi nina maswali kuhusu uwepo wetu na vitu vingine humu ulimwenguni.
 
Nina imani hata Kiranga anapinga uwepo kamili wa huyu Mungu wa kuambiwa, ila akilini mwake anakataa katakata kwamba ulimwengu na vyote viujazao vilijileta vyenyewe tu
 
Mungu anapigania watu kivip ?
 
Nimewahi kwenda theatre Mungu is real na yupo nasi everywea
 
Tupe kisa,Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app

Ukiona nyuso za watu wanaoingizwa theatre story za maumivu waliyonayo ambapo baada ya dakika kadhaa anakwenda kupasuliwa kichwa au mguu utajua kuwa Mungu yupo nao na baada ya kutolewa wakiwa hajitambui au wanaojitambua nusu kisha baadae hupata ahueni ya maumivu utajua Mungu ndiye muweza wa kila kitu kwani hutoa furaha na huzuni kwa yoyote ampendae..May God bless us all
 
Wewe uliwahi kuingizwa theater?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwaiyo kama ukiona walioingia na maumivu wamefia huko theatre then utasema Hakuna Mungu au inakuwa vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu yupo, mpangalio Wa vitu duniani unadhihirisha ivo. Hivi jua na mwezi vilijitokeza tu vikikaa pale? Miti ijitokeze tu we upate chakula na dawa? Ukiangalia proportional ya human body etc Jinsi ulivyoumbwa kwa mpango Bado Huamini.? MUNGU YUPO. kama Kuna vitu hauvioni ktk maisha yako haimaanishi Mungu hayupo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera mleta mada.

Mungu amekupigania kwa kiasi kikubwa katika nyakati mbali mbali

Je nani alikua adui katika hiyo vita?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama na wewe ni mkufunzi wa Hivi Vitabu vya mwarabu na mzungu...
Itakua nikupoteza muda kukiliza na ukatoa majibu uliyokaririshwa na your religion masterz
 
Leo nimefurah sana baada ya kuona hi maada binafsi mi huwa naamini uwepo wa mungu na sio kanisa
salam Kanisa wako mpendwa katika bwana
 
Hayo ndo maswali nadhani kila mmoja wetu ujiuliza kila siku, nami naongeza, ilikuwaje tukawa na lugha tofauti wakati chimbuko letu ni moja? imekuwaje tukawa na wanyama rafiki kama mbwa, paka, kuku, mbuzi, bata, ng'ombe nk. je hao wanyama walikuwa walikuwa polini wakavutiwa na maisha ya binadamu ndo wakaja kuishi na binadamu? au mwanadamu alistuka tu akawaona pembeni mwake?
 
Kama na wewe ni mkufunzi wa Hivi Vitabu vya mwarabu na mzungu...
Itakua nikupoteza muda kukiliza na ukatoa majibu uliyokaririshwa na your religion masterz
Good point! Kama unafuata hv vitabu vya waarabu na wazungu itakuwa ni kupoteza muda kupata majibu sahihi. Swali kwako... Mungu yupo ama hayupo? Au unamaoni gani nje na hapo kuhusu mijadala inayohusu kuamini na kutokuamini uwepo wa Mungu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanaamini hivyo kwa kuwa na mizizi ya ufahamu wao wa kimawazo waliokuzwa nao sawia toka wadg kwa imani tofauti za kidini,kuna watu mfano hai wadzabe hata wapate athari ya ukubwa upi awawezi tambua kuna uwepo wa mungu wawapo kwny majonzi yeyote,makuzo ya kiimani ndo chanzo cha yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…