Muulize huyo rafiki yake na demu wako kama hajawahi mtongozea boyfriend wake.Wakuu imekaaje hii? Nina girl wangu namwelewa sana mzuri nampenda. Sasa majuzi hivi ilikuwa ni Siku yake ya kuzaliwa. Basi ili kumfurahisha nikajichanga na kumfanyia ki party cha kiaina.
Iyo Siku ya party walikuwepo rafiki zake kadhaa na mmoja wapo ambapo nilimuliza akaniambia anaitwa Anna ( isn't real name). Basi party ilikwenda fresh na baadae kila mmoja aliondoka, wengine niliwapeleka mimi na gari kwa sababu ilikuwa night sana na mmoja wapo ni uyo Anna.
Baada kama Siku kadhaa nikiwa nae geto nilimuliza kama wale rafiki zake walifika salama, akajibu ndio. Nikamuliza na Anna je? Akajibu ndio lakini baada ya mda aliniuliza kama nimempenda Anna maana namulizia sana.
Me nikamjibu hapana sio kwa hivyo ulivyowaza. Kumbe yeye akawa serious zaidi na kwenda kumwambia Anna kuhusu mimi. Basi juzi ivi kabla ya sikukuu nikiwa mbishe, Anna kanitafuta kwa simu na kuniambia flani kasema unashida ya kuonana na mimi. Katika kuongea nikajikuta nimemuliza kama yuko tayari tuonane.
Akatiki basi jumapili tuka onana ..kiukweli uyu Anna ni mkali balaa kuanzia shepu mpaka sura yani ameiva kila idara. Tukapiga stories za hapa na pale kufahamiana nini.. badae sasa ndo nikamuliza kuhusu Jenipha( my girl, siyo real name) alimuambia nini.
Mtoto akaanza kutiririka Jenipha kamwambia mim nimwelewa sana na tangu ile Siku ya party nimemwona basi nimekuwa nikimuwaza. Mimi nikamuliza kama yuko single basi akajibu kuwa yuko single kwa zaid ya mwaka sasa.
Nikamuliza pia yuko tayari kuanza relationship akanijibu kama akipata mtu sahihi kwake yeye yupo ok na yupo tayari. Nikashindwa nimkatae vip maana hajui kama rafiki yake ni mpenzi wangu.
Kristmass alinialika na anakaa peke yake, nikashindwa kwa sababu nilikuwa na my girl Jeni. Japo dah! Niliumia kimtindo kukosa huo mwaliko. Sasa tangu juzi tuna chart nakurushiana picha wasap na nini ( sio picha za utupu) kama tuna anza kuwa close vile.
Sasa wakuu nauliza huyu girl wang alikuwa na lengo gani kwenda kumpanga mwenzake wakati yeye anajijua kuwa yupo? Ni mtego gani ananitegea apo? Na uyu Anna nashindwa nimkatae vip maana ni mzuri sana anatamanisha.
Wakuu nishaurini nipige kwa Uyu Anna halafu nimkatae au nimwambie tu ukweli kuwa aliyekutuma kwangu ni mpenzi wangu.?
Kama ni ndefu sana mtanisamehe wakuu, ni ukweli na siyo maneno ya kutungwa.
Nishauri.
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji3][emoji3][emoji3]Kama sijakuelewa....yani umemfanyia pati gf wako na akaalika rafiki zake nawe ukiwepo halafu Anna asijue kiwa Jenifa ni mpenzi wako???
Au alijua ni mjomba wa kufikia???
Nieleweshe
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama mimi ninavyotaka nikutongozee Yule black beauty wa Sinza bby [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hahahahaha nayo ni mawazo bro.Sharing is caring broo halafu kingine ladha ya nyama ya ndafu ni ileile broo we chagua moja either A au J maana kwa mwendo huo utamaliza dunia nzima ila pia nahisi birthday ya anna inakaribia hapo ndo uelewe maana ya sharing is caring baada ya hapo anna atakuunganisha na july (not real name)
Kama nakuona vile unavogeuzwa birthday party sponser broo hata serikali ndo hivo zinavoendeshwa ni kwa kutumia pesa za wahisani yaan wawekezaji kama ww!!!!!!
Poa mkuu ..nikishamweka sawa nitakutupia mpira umalize..Ollachuga Oc
Hata mimi nimempenda Anna mpange aje kwangu wewe ubaki na Jennifer!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hii issue ya ukweli Sema labda nmeshindwa kuelezea fresh.."wengine niliwapeleka mimi na gari kwa sababu ilikuwa night sana na mmoja wapo ni uyo Anna.
Baada kama Siku kadhaa nikiwa nae geto nilimuliza kama wale rafiki zake walifika salama, akajibu ndio. Nikamuliza na Anna je? Akajibu ndio"
Bila shaka hili ni PICHA LA KIHINDI
Ndiyo maana mwishoni unatulazimisha tuamini, pumbaf* saaana!! #ShuleZifunguliweTuu
Inaezekana nategwa mkuu..Watu unawapeleka wewe na gari alafu unamuuliza mwingine km wamefika salama...
Cha kushukuru ni kuwa nimeupitia uzi wako tu...
Ila maswal ya kisee km haya ni ujinga wa kutokujua kufanya maamuzi.
Unaomba ushauri gani sasa hapa?
Sent using Jamii Forums mobile app
dah ulitisha Sema ulikua na fujo sanaHapo wanataka wakuchune Wakudange tuu,hakuna kitu kama hicho.Hiyo kitu ilinitokea wayback pamoja na kula tuhela twangu sikufanya ajizi nilipita nao.Baada ya kukutokea purukushani (mmoja alikuta mwenzie yupo geto anatundikiwa drip) ndiyo ukawa mwisho .
Sent using Jamii Forums mobile app
Nahisi kajua ila kama anakaushia vile..Ili kuwa kwenye safe side mwambia anna unadate na jenipha ili ukija kumla kusiwe na kusema umenidanganya
Mkuu hakuna kilichotungwa apo.Ushauri wangu una kipaji cha utunzi,vipi ukifikiria utunzi wa hadithi za mapenzi kama shigongo au mtunzi wa movie?
Sawa bro but mshika viwili vyote anaeza himili, inategemea na jinsi gani ameshika..Kikubwa jiongeze "kisicho ridhiki hakiliki" huyo demu sijui Anna amekutamani kama jinsi wewe ulivyomtamani (hapo hakuna upendo wa moyoni) bali kuna upendo wa matamanio
Siku ukijikuta umemwacha demu wako kwa kisingizio hicho, hiyo dhambi haitokuacha salama, hayo mahusiano mapya hayatadumu na anguko lake litakuwa kubwa zaidi, tena zaidi la anguko lililopita,,,
"Mshika viwili vyote......."
Sent using Jamii Forums mobile app
Basi kama ni hivyo atakuwa na nia nzuri sana. Japo inashangaza mnooMwanamke wako ana mtu mwingine anaogopa akikuacha atakuumiza so anataka upate mtu ili hata akikuacha asikuumize sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Aha, nitamuliza mkuu.Muulize huyo rafiki yake na demu wako kama hajawahi mtongozea boyfriend wake.
Jino kwa jino
Sent using Jamii Forums mobile app
Si ndio mkuu, mfanyie kweli mchizi apone.Kama mimi ninavyotaka nikutongozee Yule black beauty wa Sinza bby [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Sent using Jamii Forums mobile app