Gilead Teri: Uwekezaji Kwenye Sekta ya Uzalishaji Umeongezeka Kwa asilimia 542% miaka 4 ya Rais Samia kutoka 1.6T (2020) Hadi 10.6T (2024)

Gilead Teri: Uwekezaji Kwenye Sekta ya Uzalishaji Umeongezeka Kwa asilimia 542% miaka 4 ya Rais Samia kutoka 1.6T (2020) Hadi 10.6T (2024)

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
79,084
Reaction score
84,978
Takwimu zinaonyesha ongezeko kubwa la uwekezaji katika miradi ya sekta ya uzalishaji kati ya mwaka 2020 na 2024. Mwaka 2020, thamani ya uwekezaji katika sekta hiyo ilikuwa dola za Marekani milioni 635.852. Kufikia mwaka 2024, thamani hiyo ilifikia dola milioni 4,079, ikiwa ni ongezeko la dola milioni 3,443.148 sawa na asilimia 542.

Ukuaji huu mkubwa wa uwekezaji unatajwa kuwa kiashiria cha mazingira rafiki ya sera za uwekezaji zilizowekwa na Serikali ya Awamu ya Sita. Ongezeko hilo limechangia kuongezeka kwa mapato ya Serikali pamoja na kukuza uchumi wa Taifa.

1752137475155.png
====

My Take
Haters wa SSH Watapata tabu sana maana namba za Samia zinatisha sana haijawahi tokea maana Kila kitu amefaulu zaidi ya 100%.

Ni hivi hakuna force itakayomtoa zaidi ya iliyomuweka so wengine msipoteze mda na kueneza chuki na propaganda za kipuuzi.

Pia soma Gilead Teri: 2024 TIC imevunja rekodi zote za Uwekezaji ikiwemo ya mwaka 2012 kwa kusajili miradi 901 ya Trilioni 19. Ampa Rais Samia maua yake | JamiiForums Gilead Teri: 2024 TIC imevunja rekodi zote za Uwekezaji ikiwemo ya mwaka 2012 kwa kusajili miradi 901 ya Trilioni 19. Ampa Rais Samia maua yake
Screenshot_20250710-120238.jpg
 
Nataka kuona mfumuko wa bei ukishuka, kipato cha Mtanzania wa kawaida kikiongezeka, na bidhaa zinazozalishwa hapa zikipunguza uagizaji kutoka nje, siyo kusikia trilioni kwenye ripoti huku umasikini ukiendelea mitaani.
Yaani wewe ndio kichekesho,hivi Tanzania Kuna mfumuko wa bei kweli?

Hakuna hata mwaka mMoja Inflation rate imewahi fikia 5% Kwa miaka zaidi ya 10 iliyopita.

Nenda BoT ukaone kama haya hayapo 👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DL642I0tCrc/?igsh=MXJnMnlxMmZvZDQ5Mg==
 
Halafu hizi asilimia za mtaani na zinazofundishwa shule ni tofauti?
Nakumbuka Mwalimu wa Hesabu alikuwa anasema kuwa asilimia haziwezi kuzidi Mia Halafu sahivi huwa nakutana hadi na asilimia alufumoja😀
Leta formula aliyokufundishia tufanye hesabu.
 
Ulivyo mjinga na usiye na akili unaishi kwa takwimu kuliko uhalisia wa maisha ya watanzania walio wengi hapa nchini.
Wewe ndio mjinga Kwa sababu hujui kipimo Cha hicho unachoongea.

Kwa Lugha nyingine unataka bei za 1961 ziwepo 2025.

Mpaka hapo usijadili neno inflation kama hujui jinsi linavyopimwa.
 
Wewe ndio mjinga Kwa sababu hujui kipimo Cha hicho unachoongea.

Kwa Lugha nyingine unataka bei za 1961 ziwepo 2025.

Mpaka hapo usijadili neno inflation kama hujui jinsi linavyopimwa.
Hali ya maisha haiwezi kupimwa kwa takwimu peke yake. Hata kama inflation iko chini, gharama za maisha kwa watu wa kawaida bado ni changamoto kubwa.

Huelewi wapi wewe chawa kiziwi?
 
Takwimu zinamsaidia nini maskin wa kule Tandahimba ama jobless wa makuyuni ama nzega huko...takwim za kwenye makaratasi ila uhalisia nchi Ina tabaka kubwa la MASIKINI WENGI wanaonyonywa na mafisadi na mapapa kutoka.usiasani
 
Hali ya maisha haiwezi kupimwa kwa takwimu peke yake. Hata kama inflation iko chini, gharama za maisha kwa watu wa kawaida bado ni changamoto kubwa.

Huelewi wapi wewe chawa kiziwi?
Gharama za maisha kama zipi ikiwa basic necessities zinapatikana Kwa bei nafuu? Mfano Chakula na mavazi.

Hizo gharama zako unazozisema ni zipi?
 
Takwimu zinamsaidia nini maskin wa kule Tandahimba ama jobless wa makuyuni ama nzega huko...takwim za kwenye makaratasi ila uhalisia nchi Ina tabaka kubwa la MASIKINI WENGI wanaonyonywa na mafisadi na mapapa kutoka.usiasani
Huyu chawa hawezi elewa kitu kwa sababu anaishi kwa takwimu kuliko uhalisia wa maisha ya watanzania walio wengi hapa nchini.
 
Takwimu zinamsaidia nini maskin wa kule Tandahimba ama jobless wa makuyuni ama nzega huko...takwim za kwenye makaratasi ila uhalisia nchi Ina tabaka kubwa la MASIKINI WENGI wanaonyonywa na mafisadi na mapapa kutoka.usiasani
Takwimu ndio kipimo Cha ulikotoka na kuliko .

Hizi takwimu zinaonesha kiwango Cha umaskini kimepungua na ndio maana vifo vya Watoto wadogo bimeoungua,vifo vya kina mama vimepungua na life expectancy imeongezeka.

Una swali jingine? Au wewe ulitaka Serikali imgawie pesa huyo maskini wa Tandahimba au?

Mwisho Tandahimba sio maskini kama ulivyokaririshwa, maskini wako Kagera.
 
Gharama za maisha kama zipi ikiwa basic necessities zinapatikana Kwa bei nafuu? Mfano Chakula na mavazi.

Hizo gharama zako unazozisema ni zipi?
Mfuko wa unga, lita ya mafuta, hata sabuni si kama zamani. Ukiona havikugusi, shukuru Mungu, sio kushupaza shingo kupinga vitu ambavyo ni halisi kabisa kwenye maisha ya watanzania wengi hapa nchini.
 
Mfuko wa unga, lita ya mafuta, hata sabuni si kama zamani. Ukiona havikugusi, shukuru Mungu, sio kushupaza shingo kupinga vitu ambavyo ni halisi kabisa kwenye maisha ya watanzania wengi hapa nchini.
Vyote hivyo vimefanyaje? Nimekuuliza unataka bei za 2015 ndio ziwepo 2020?

Zamani ulikuwa unalipa ada ya shule ya msingi Hadi sekondari,Leo unalipa?
 
Back
Top Bottom