Ghost Workers.!,ghost workers..! Watumish hewa ni wakina nani?

Feb 27, 2016
109
138
Wana JF Salaam,

Kumekuwa na makosa makubwa ya jinai yakiendelea kutendeka na baadhi watumish wa umma wachache miongoni mwa idara wizara na hata office za mikoa na halimashauri za miji, kwa ujumla katika kila eneo serikalini,ambapo malipo ya mishahara hufanyika ama huandaliwa.

Pamoja na jinai hiyo kupewa jina la watumish hewa-"ghost workers" makosa hayo makubwa yanaweza kutafsiriwa kama"Kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu", "Wizi wa kuaminiwa" "Wizi" na "Fraud" najua mliobobea kwenye maswala ya sheria mnaweza makatujuza vizuri aina ya makosa ambayo waliohusika na kuandaa na kutenda kosa la kupokea mishahara hewa huku wakijua kabisa ni kinyume cha sheria na taratibu za nchi wametenda kosa gani, wanastahili adhabu gani.

Kwa taarifa za Mh.JPM jana hata nyumba kuu wapo na imeshaundwa "task force" kuwa nasua ili kunusuru upotevu mkubwa wa pesa za umma.Kulikuwa na kauli ya Mh.Rais wetu mpendwa kuwa alipotuma watu wake wakamletea taarifa kuna mtu mmoja peke yake serikalini alikuwa akilipwa mishahara ya watu 17 ambao ni watumishi hewa kila mwisho wa mwezi na pengine yapata miaka 15 mfululizo.

Sina hakika kama kipindi hicho kulikuwa na sheria hizi hizi na katiba hii hii au viongozi waliopita walikuwa wanatumia katiba yao peke yao.
Na pia sina hakika kama tulikuwa na viongozi wa nchi na pia kama kulikuwa na kiongozi mkuu wa nchi wa vipindi tofauti tofauti vya miaka mitano,mitano.ama kwa suala la ufuatiliaji wa ufujaji na ubadhilifu wa fedha za uma walikuwa wamelala usingizi mzito ule wa sindano ya nusu kaputi

Jamani msinishangae mimi muwashangae hao waliopita ambao walikuwa hawaoni hao"ghost workers" au ndiyo ilikuwa business as usual? Tangu uongozi wa kupokezana madaraka ulipoanza mwaka 1985 mpaka uongozi mpya mwaka 2015-16 mambo haya ndiyo yameibuka kwa kasi na kufanyiwa kazi. Sijui kama nchi ilikuwa inasubiri ipate Rais mzalendo wa kweli na mwenye uchungu na rasilimali za nchi hii na pia anaye-share pain na wananchi wake wanyonge na wa hali ya chini?

Kama takwimu za awali zilionyesha kulikuwa na wafanyakazi hewa zaid ya 1,300 nchi nzima,ambao waligharimu over one bilion ya pesa za wavuja jasho wa Tanzania.na jana Mh.Rais wetu mpendwa alitaja idadi iliyogundulika mkoa mmoja tu wa Shinyanga ni 45, waliolipwa mwisho wa mwezi huu watatu tu kiasi cha shilingi mil.333.9 kama niko sahihi.ambayo idadi hiyo hata hivyo ilitaka kufichwa na watu wasiokuwa na huruma na kukosa uzalendo wa nchi yao ambao nadhani walikuwa ni beneficiaries wa that particular offence.

MASWALI:
HIVI NDUGU ZANGU KAMA TUMEJUA IDADI YA WAFANYAKAZI HEWA.
MUDA AMBAO WALIKUWA WAKILIPWA MISHAHARA YA BURE,NA KIPINDI CHA NYUMA WALIKUWA WANASAINI KWENYE PAYROLL SHEET.SIKU HIZI WANAFUNGUA ACCOUNT NA KUWEKEWA KWENYE ACCOUNT ZAO KWENYE RESPONSIBLE BANKS.ESP.CRDB/NMB.


1.JE? TUMESHINDWA KUWAJUA WALIOANDAA MALIPO HAYO,WALIOPIGA DEAL KUANZIA HAZINA MPAKA WIZARA AMA IDARA,HALIMASHAURI AMA MKOA HUSIKA.WALIOPOKEA MALIPO HAYO?
2.JE? HIZO BANK WALIZOFUNGUA ACC. BILA HAO MAREHEMU AU RETIRED OFFICERS KUSAIN OPENING ACC.DOCUMENTS KUNAPICHA ZA NANI KWENYE ACC ZAO? WAKIWA WAMEKUFA HIZO BANK ZIMEFUATA KYC NA REGULATIONS ZA BOT? ILI KUTUNZA KUMBUKUMBU NA KULETA NIDHAMU KWANINI TUNAPOSEMA WATUMISHI HEWA 45 WASIORODHESHWE MAJINA YAO NA ANGALAU MUDA HUU WENGINE WANGEKUWA NA NDOO ZAO WAKIELEKEA KUPANDA MAGARI YA KIJANI?
3.JE? KWANINI TUENDELEE KUTAJA IDADI YA WATUMISH HEWA NA KIASI CHA HASARA WALIOISABABISHIA SERIKALI YETU LAKINI TUNAWAHESHIMU NA KUWAOGOPA HATUWATAJI NA KUJULIKANA NA KUCHUKULIWA HATUA MARA MOJA KAMA WANAVYOFANYIWA WATENDAJI WENGINE?
Wahusika tupeni majibu ya maswali haya
WATUMISHI HEWA NI WAKINA NANI?


UISHI MILELE RAIS WETU Dr.JPM ,Tunathubutu kusema kwa kasi hii baba mwaka 2020.si wapinzani wa ndani ya chama tawala wala wapinzani wa nje wasisimamishe mgombea mwingine. Nadhani unatosha....Ni hayo tu wana jf.
 
mkuu wizi huo sio wa mtu mmoja ni system imejumuisha watu kibao.mtu mmoja hawezi kufanikisha wizi kama huo kutokana na internal control procedure zilizopo kwenye malipo ya hela za serikali.wame collude kuhujumu taifa
 
Back
Top Bottom